
Taarifa
kutoka jeshi la
polisi kanda maalum
ya Dar es
salaam , zinaarifu kuwa tukio
hilo lilitokea February mosi
saa nane na
nusu usiku maeneo
ya Chanika Kimwani , ambapo moto
ulizuka ghafla katika
nyumba ya Theresia
Pius (45) na
kuteketeza vitu vyote
vilivyokuwemo ndani ya
nyumba hiyo pamoja
na kumuunguza mwanamke
huyo.
Aidha taarifa
zinaeleza kuwa
mwanamke huyo aliyefariki,
enzi za
uhai wake aliachwa
na mmiliki wa
nyumba hiyo hadi
atakaporejea , hivyo wakati tukio
hilo likitokea mmiliki
wa nyumba hiyo
hakuwepo.
Hata
hivyo chanzo cha
kuzuka kwa moto
huo bado hakijafahamika na
jitihada za kumtafuta
Theresia Pius ili
kupata taarifa zaidi
zinaendelea.
Sambamba
na hayo , hakuna mtu
aliyekamatwa juu ya
tukio hilo na
maiti imehifadhiwa hospitali
ya Taifa muhimbili
huku upelezi ukiendelea.
Na Kenneth John wa , Dar-es-salaam
0 comments:
Post a Comment