Tuesday, 4 February 2014

MKASI,KISU,MASHINE YA KUTOBOA ARDHI VYA SABABISHA KIFO DAR.


Na Kenneth John Dar
Mwanaume  mmoja  aliyefahamika  kwa  jina  la  Masoud  Jaffar  (30)  ambaye  kazi  yake  ni  kuchimba  mashimo,  amefariki  dunia  baada  ya  kuangukiwa  na  kifusi.

Taarifa  kutoka  jeshi  la  polisi  kanda  maalum  ya  Dar  es  salaam  zinasema  kuwa,   February  3   majira  ya   saa  kumi  na  mbili  na  dakika  ishirini  jioni    huko  barabara  ya  Mandela ,   eneo  la  kurasini  Baraza  la  maaskofu , mtoa  taarifa   Said   Ally   Nayeka (35)   ambaye  ni  mkazi  wa  Buza  kwa  lulenge   na  pia  ni  Operator   Ravji  Construction  Ltd  alilieleza   jeshi  la  polisi   kuwa   akiwa  na  wenzake   mara  baada  ya  kumaliza  shughuli  ya  kutoboa  mashimo  ya  kupitishia  bomba  za  gesi  chini  ya  barabara  ya  Mandela,  kwa  bahati  mbaya  walisahau  mkasi,kisu  na  mashine  ya  kutoboa  ardhi   ndani  ya  mashimo  hayo  waliyokuwa  wakichimba  na  ndipo  Masoud  Jaffar  aliingia   ndani   ya  shimo  ili  kutoa  vitu  hivyo.

Na  akiwa  bado  ndani  ya  shimo  ghafla  aliangukiwa  na  kifusi  cha  mchanga   na  kufunikwa  na  hatimaye  alifariki  dunia  papo  hapo.

Aidha  taarifa  zinaendelea  kusema  kuwa  kifusi  hicho  kilianguka  baada  ya  mtikisiko  wa  lori  lililopita  karibu  na  shimo  hilo  ambalo  namba  zake  hazikufahamika .

Maiti  ilifukuliwa  na  mwili  wake  umehifadhiwa  hospitali  ya  Temeke    huku  upelelezi  ukiendelea.

Na  katika  tukio  lingine  lililotokea  maeneo  ya  Boko  beach  wilaya  ya  kinondoni,  imekutwa  maiti  ya  mtoto  mchanga  anayekadiriwa  kuwa  na  umri  wa  siku  1 .

Ambapo  kwa  mujibu  wa  jeshi  la  polisi  kanda  maalum ya  Dar  es  salaam  maiti  ya  mtoto  huyo  mchanga  ilikutwa  ikiwa  imeviringishwa  nguo  na  mtu  asiyefahamika .
Maiti  imehifadhiwa  hospitali  ya  Mwananyamala  na  hakuna  aliyekamatwa ,upelelezi  unaendelea.

Related Posts:

0 comments: