Wednesday, 12 February 2014

MBUNGE MSINGWA AMTOLEA UVIVU WAZIRI NYALANDU



mbunge  msigwa akizungumza  na  wanahabari leo 

mwandishi  Kenneth John wa   Dar
.........................................
Kutokana  na  hivi  karibuni  gazeti  la  Daily  Mail  linalochapishwa  nchini  Uingereza  kuripoti  kuhusu  biashara  haramu  ya  pembe  za  ndovu,inayokadiliwa  kuwa  soko  la  shilingi  trilioni  19  za  Kitanzania,Waziri  wa  maliasili  na  utalii  mhe  Lazaro  Nyalandu  alinukuliwa  na  vyombo  mbalimbali  vya  habari  akikanusha  taarifa  za  chapisho  hilo  na  huku  akisema  kuwa    zilikuwa  na  mlengo  wa  kuichafua  Tanzania.

Hivyo  kutokana  nakukanusha  kwa  waziri  Nyalandu  juu  ya  taarifa  hizo  imepelekea  waziri  kivuli  wa  wizara  hiyo  ambaye  pia  ni  msemaji  mkuu  wa  kambi  ya  upinzani  Mhe,Mch  Peter  Msigwa  kuibuka  na  kusema  kuwa  waziri  Nyalandu  amesahau  kuwa  Tanzania  imejichafua  yenyewe   kwenye  taswira  ya  kimataifa  kutokana  na  biashara  hiyo  haramu  ya  pembe  za  ndovu.Na  kuongeza  Nyalandu  anasahau  ulimwengu  wa  sasa  ni  wakiteknolojia  ambao  taarifa  mbalimbali  juu  ya  biashara  hiyo  haramu  pamoja  na  mauaji  ya  tembo  zimesambaa  kila  mahali  hasa  katika  vyombo  vya  habari  vya  ndani  na  nje  ya  nchi .

Kutokana  na  hali  hiyo  Mch  Msigwa  amesema  kuwa  anashangazwa  na  waziri  kutumia  nguvu  nyingi  katika  kupangua  tuhuma  dhidi  ya  serikali  hasa  katika  kushindwa  kwake  katika  kuangamiza  biashara  hiyo  haramu,Huku  akisitiza  takwimu  za  serikali  zinaonyesha  mwaka  2010   tembo  elfu  kumi  waliuwawa  Tanzania  pekee  ambapo  ni  sawa  na  wastani  wa  Tembo  thelathini  na  saba  kwa  siku.Aidha  Msigwa  ameendelea  kubainisha  hivi  sasa  Tanzania  ina  Tembo  laki  moja  na  hamsini  hadi  laki  moja  na  sabini  na  kwamujibu  wa  takwimu  hizo  Msigwa  amesema  kunauwezekano  mkubwa  endapo  ifikapo  mwaka  2017  hadi  2018  nchi  inaweza  kuwa  haina  tembo  hata  mmoja,Hivyo  Msigwa  akasema  kutokana  na  takwimu  hizo anashaangaa  kusikia  waziri  akidai  kuwa  serikali  inachafuliwa  wakati  takwimu  zinaonyesha  hali  halisi  ya  kuendelea  kwa  biashara  hiyo.
Aidha  Mch, Msigwa  ameongeza  kuwa  mara  nyingi  waziri  amekuwa  akinukuliwa  na  vyombo  vya  habari  akisema  mtandao  wa  ujangili  unafahamika  na  ni  mpana  na  unauhusisha  watu  wenye  nguvu  za  pesa  na  huku  akiwaomba  wanaojihusisha  kuachana  na  biashara  hiyo  mara  moja. Hivyo Msigwa  akasema  anachoona  hapo  kwa  waziri  Nyalando  ni  kama  anawabembeleza  watuhumiwa  huku  akijua  fika   wanavunja  sheria.
Pamoja  na  hayo  ameendelea  kusema  kauli  hizo  za  waziri  Nyalandu  zinaonyesha  dhahiri  kuwa  kuna  watu  ambao  hawaguswi  na  sheria  na  wapo  juu  ya  sheria.

Hata  hivyo  Mch  Misigwa  amesema  kuwa  kauli  hizo  zinaendelea  kuonyesha  kuwa  mtandao  huo  umekuwa  ukiogopwa.
“Majibu  haya  waziri  yanadhihirisha  kuwa  mtandao  huu  unaolalamikiwa  na  kuogopwa  ndio  unaohusisha  Ikulu,wanasiasa, watumishi  wa  serikali,maafisa  wanyamapori,maafisa  usalama,Polisi,  wanajeshi  pamoja  na  wanyabiashara  wakubwa  ambao  wamekuwa  wakijihusisha  na  serikali  ya  CCM”Alisema  Mch,  Msigwa.

Akiendeendelea  kufafanua  Mch  Msigwa  amesema  kitendo  cha  kukamata  kwa  shehena  za  meno  na  pembe  za  ndovu  hakumaanishi  kuwa  waziri  anafanya  kazi  kwani  tembo  wanakuwa  tayari  wamekwisha  uwawa .

 Halikadharika  Mch,  Msigwa  amesema  kuwa  serikali  makini  haiwezi  kumbembeleza  jangili  na  hali  hiyo  inaonyesha  serikali  bado haipo   makini  juu  ya  suala  hilo.

Sambamba  na  hayo  pia  amebainisha  baadhi  ya  tuhuma  ambazo  serikali  ya  Tanzania  ilituhumiwa  na  Gazeti  la  Daily  Mail  lakini  hazikutolewa  ufafanuzi  na  Waziri  Nyalandu.

Tuhuma  hizo  amesema  ni  pamoja  na  watu  waliokaribu  na  mhe  Rais  Kikwete  wanahusika  katika  biashara  ya  meno  ya  tembo  ndio  maana  serikali  yake  imekuwa  haichukui  hatua  stahiki  katika  kukabiliana  na  jambo  hilo,na  tuhumu   nyingine  ni  ile  ya  ndege  iliyomleta  Rais  wa  China  kuondoka  na  shehena  ya  meno  ya  tembo  ambayo  ilipakiwa  na  maafisa  waliokuwamo  kwenye  ndege  hiyo, halikadharika  na  tuhuma  ya   kuwa  CCM  serikali   yake  ni   wanufaikaji  wakubwa  wa  mradi  huu   kutokana  wanatafuta  fedha  kwaajili  ya  uchaguzi  mkuu  ujao  na  ndio  maana   hawachukui  hatua  kwa  wahusika  ambao  wanajulikana  kwa  majina  na  wapo  mitaani  wakiendelea  na  biashara  hiyo  haramu.

Na  kutokana  na  tuhuma  hizo  Msigwa  amemtaka  Nyalandu  kuondoa  ukimya  na  kujibu  tuhuma  hizo  kwa  vielelezo  na  si  kwakuhisia  na  kusema   hizi  ni  taarifa  za  uongo  pasipo  kuonyesha  taarifa  za  ukweli.

Pamoja  na  yote   Mch,  Msigwa  ameendelea  kusema  kuwa  serikali  bado  haijachukua  hatua  za  kuridhisha  katika  ujangili,na  kuongeza  kuwa  bado  kunahali  ya  kulindana  na  bado  hatua  za  makusudi  hazijachukuliwa  kwaajili  ya  utatuzi  wa  tatizo  hili.

Related Posts:

0 comments: