RPC Mungi
NA DIANA BISANGAO WA , IRINGA
Watu
wawili wafariki dunia mkoani Iringa katika matukio matatu tofauti
likiwemo la mkazi wa kijiji cha Mkombwe kata ya Mafinga tarafa ya Ifwagi
wilaya ya Mufindi bibi Tunu Mohammed (105) kuungua na moto wa kibatari
chumbani kwake.
Akizungumza na mtandao huu ofisini
kwake leo Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha
kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 23 januari majira ya
saa 5:45 usiku.
Kamanda
Mungi alisema chanzo cha moto huo ni baada ya kibatari alichokuwa
akitumia bibi Tunu kuangukia kitandani na kuanza kuunguza mashuka na
blanketi huku yeye akiwa usingizini.
Wakati
huohuo huko maeneo ya pori la kijiji cha Msuluti kata ya Magulwila
tarafa ya Mlolo wilaya ya Iringa mtu mmoja mwanaume Method Nyemba (17)
mchunga ng’ombe alikutwa amefariki baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba
ya mti.
Kamanda
Mungi alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 24 januari majira ya
saa 2:30 asubuhi ambapo marehemu alikutwa na majeraha ya kukatwa na kitu
chenye ncha kali maeneo ya miguuni, chanzo cha tukio hilo bado
hakijafahamika.
Mbali
na matukio hayo mawili, Kamanda Mungi alisema askari polisi wakiwa doria
huko maeneo ya Igumbilo kata ya Ruaha manispaa ya Iringa waliwakamata
raia wawili wa Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.
Mungi
alisema tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 24 januari majira ya saa 2
kamili usiku ambapo aliwataja majina yao ni Tagas Awali (29) pamoja na
Disele Ayeno (25), watuhumiwa hao wapo kituo cha polisi Iringa Mjini kwa
mahojiano Zaidi.
0 comments:
Post a Comment