HAFLA FUPI YA KUWAAPISHA MAWAZIRI WAPYA IKULU DAR LEO
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dr. Gharib Bilal wakiwa katika picha
ya pamoja na Mawaziri Mbalimbali wapya mara baada ya kuwaapisha kwenye
viwanja vya ikulu leo ambapo viongozi mbalimbali wa serikali na waalikwa
wamehudhuria na kushuhudia Picha na OMR
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akimpongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akiwa na
mkewe aliyewahi kuwa Miss Tanzania, Faraja Kotta na familia yake, baada
ya kuapishwa katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu
jijini Dar es Salaam, leo. Kulia kwa Makamu ni Naibu Waziri wa Fedha
Mwigulu Nchemba. Picha na OMR
Rais
Jakaya Kikwete, akimuapisha Adam Malima, kuwa Naibu Waziri wa Fedha,
katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es
Salaam, leo. Picha na OMR
Rais
Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri Mbalimbali
wapya na wanaohamia katika wizara nyingine mara baada ya kuwaapisha
kwenye viwanja vya ikulu leo ambapo viongozi mbalimbali wa serikali na
waalikwa wamehudhuria na kushuhudia Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Charles Kitwanga, kuwa Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya
Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR
Rais
Jakaya Kikwete, akimuapisha Amos Makala, kuwa Naibu Waziri wa Maji,
katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es
Salaam, leo. Picha na OMR
Rais
Jakaya Kikwete, akimuapisha Jenista Mhagama, kuwa Naibu Waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye
Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Dkt. Pindi Chana, kuwa Naibu Waziri wa
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, katika hafla fupi iliyofanyika
kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Mwigulu Nchemba, kuwa Naibu Waziri wa
Fedha, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini
Dar es Salaam, leo. Picha
Rais
Jakaya Kikwete, akimuapisha Juma Nkamia, kuwa Naibu Waziri wa Habari,
Vijana Utamaduni na Michezo, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye
Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Mahmoud Mgimwa, kuwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, leo. Picha na OMR
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo
VIOJA mbali mbali vimejitokeza wakati wa mawaziri wateule wa Rais Dr Jakaya Kikwete wakila kiapo baada ya naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi mbunge wa Peramiho mkoani Ruvuma Jenista Mhagama kulazimika kula kiapo kurudia kiapo mara tatu tofauti na wenzake ambao waliapa mara mbili kutokana na naibu waziri huyo kuchemka mara ya kwanza mbele ya Kikwete . Mbali ya Mhagama kuchemka na kuingia katika rekodi ya kurudia kiapo mara tatu pia naibu katubu mkuu wa CCM ambae ni naibu waziri wa fedha Bw Nchemba yeye alitinga katika viwanja hivyo huku akiwa kawaida na jezi za timu ya Taifa tofauti na wengine ambao walifika wakiwa wameulamba suti vikali . Hata hivyo wapembuzi wa mambo wanadai kuwa kuchemka kwa Mhagama katika zoezi hilo ni kutokana na kutokuwa na imani kama angeteuliwa kuingia kushika nafasi hiyo nyeti na unaibu uwaziri |
Monday, 20 January 2014
HOME »
» VITUKO KIAPO KWA MAWAZIRI WATEULE WA JK MMOJA ACHEMKA KUAPA IKULU DAR LEO
0 comments:
Post a Comment