………………………………………………………………………………
Asteria Muhozya,
Ujumbe
kutoka Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), umekutana na uongozi wa
Wizara ya Nishati na Madini ili kujadili masuala mbalimbali ya namna
sekta binafsi zinavyoweza kushiriki katika uchumi wa gesi na mafuta
nchini.
Ujumbe
huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Bw. Reginald Mengi na
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Bw. Godfrey Simbeye pamoja na
wawakilishi wengine wa Taasisi hiyo ulifika wizarani jana kukutana na
uongozi wa Wizara.
Aidha,
ujumbe huo ulipata nafasi ya kukutana na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati
na Madini Bw. Eliakim Maswi na baadhi ya Watendaji wa Wizara
wanaoshughulikia masuala ya Nishati, ambapo TPSF walipata fursa ya
kuwasilisha mapendekezo yao kuhusu namna ambavyo watashiriki katika
uchumi wa gesi.
Wakiongozwa
na Mwenyekiti wao, wajumbe toka TPSF walieleza nia yao ya kushiriki
katika uchumi wa gesi na kueleza mikakati ya namna watakavyoshiriki
ili sekta iweze kuwa na manufaa kwa Watanzania wote na hivyo kuongeza
pato la nchi na kufikia maendeleo tarajiwa.
Pamoja
na hayo, Mwenyekiti wa sekta binafsi Bw. Reginald Mengi alitumia fursa
hiyo kueleza kuwa, kikao hicho kimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano
ili nchi iweze kuweza kufikia kule Watanzania na Taifa linakotarajia
kufika.
“Naondoka
katika kikao hiki nikiwa na amani sana. Yaliyopita yamepita na
yamekwisha. Tunataka kufanya kazi pamoja na Wizara katika sekta ya gesi.
Tumekuja hapa kama Watanzania, tujue tutafanya kazi namna gani katika
sekta hii”. Alisema Mengi.
Kwa
upande wake, Katibu Mkuu Wizara hiyo Bw. Eliakim Maswi, aliushukuru
ujumbe huo kwa kufika katika mazungumzo hayo na kueleza kuwa, nia ya
Wizara na Serikali ni kuona Watanzania wote wanashiriki katika uchumi
huo. Aidha, aliongeza kuwa, Wizara inayachukua mapendekezo hayo na
kuahidi kuyafanyia kazi.
“Kwetu
sisi tunataka kuona watanzania wanashiriki katika uchumi huu. Tuko
tayari kufanya kazi na ninyi. Tufungue milango, tusaidiane huku
tukiendeleza utulivu na uvumilivu. Mimi na wataalam wangu tutayafanyia
kazi”. Alisema Maswi.
0 comments:
Post a Comment