Monday, 13 January 2014

TAARIFA YA TAHADHARI YA MVUA KUBWA NA UPEPO

220px-Coat_of_arms_of_Tanzania.svg
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA UCHUKUZI MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Simu: 255 22 2460735/2460706

FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056

Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM

Tovuti: www.meteo.go.tz

……………………………………………………..

Taarifa kwa umma: Kunatarajiwa kuwepo na upepo mkali, mawimbi makubwa na mvua kubwa.

Taarifa Na.

201401-03

Muda wa Kutolewa

Saa za Afrika Mashariki

Saa 4 Asubuhi

Daraja la Taarifa:

Tahadhari

Kuanzia:

Tarehe

14 Januari, 2014

Mpaka:

Tarehe

16 Januari, 2014

Aina ya Tukio Linalotarajiwa

1. Hali ya Upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa pamoja na mawimbi makubwa zaidi ya mita 2.0

2. Vipindi vya mvua kubwa (zaidi ya mm 50 ndani ya saa 24)

Kiwango cha uhakika:

Wastani (60%)

Maeneo yanayotarajiwa kuathirika

1. Upepo mkali: Pwani ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba

2. Mvua kubwa: Mikoa ya Rukwa, Mbeya , Njombe, Ruvuma, Mtwara pamoja na kusini mwa mkoa wa Morogoro

Maelezo:

Hali hii inatokana na kuimarika kwa mfumo wa mgandamizo mdogo wa hewa kusini magharibi mwa Bahari ya Hindi, maeneo ya mkondo wa Msumbiji. Mfumo huu unatarajiwa kuvuta upepo kutoka Pwani ya Somalia na misitu ya Congo.

Angalizo:

Watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo hatarishi wanashauriwa kuchukua tahadhari.

Maelezo ya Ziada

Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo pale itakapobidi.

Imetolewa na

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Related Posts:

0 comments: