>>PSG YAMNYATIA!!
>> SKANDALI LA UHAMISHO NEYMAR: MWANACHAMA HAFUTI KESI HADI…..!!
Huku ikiripotiwa kuwa Paris St-Germain
ilikuwa ikimnyemelea Messi, mwenye Miaka 26, Rais wa muda wa Barca,
Bartomeu, amedai: “Klabu itakaa chini na kujadiliana Mkataba mpya.
Tutafanya kila tuwezalo abaki awe Mchezaji anaelipwa vizuri sana.”
Messi na Goli:
-Msimu huu, Messi ametoa Msaada wa Magoli mara 36 na kufunga Bao 18.
Msimu uliopita, Messi alifunga Bao 60
katika Mechi 50 lakini Msimu huu amekuwa akisuasua kwa kufunga Bao 18, 8
zikiwa kwenye La Liga, na pi kuumia na kuwa nje kwa Miezi miwili.
SKANDALI LA UHAMISHO NEYMAR: MWANACHAMA HAFUTI KESI HADI…..!!
Wakati huo huo, Mwanachama wa Barcelona,
Jordi Cases, ambae ndie aliefumua Skandali la Uhamisho wa Neymar
uliofanfa Rais wa Barcelona, Sandro Rosell, ajiuzulu na Kesi kutinga
Mahakamani kwa uchunguzi juu ya Ubadhirifu wa Fedha kuhusu Uhamisho huo,
amesema hatafuta Kesi hadi apewe kimaandishi uhakika kwamba Barca
haitalipa kisasi kwa kumdai Fidia.
Kufuatia kujiuzulu kwa Sandro kulikuwa na dhana kuwa Kesi hiyo itafutwa ingawa Wakala wa Cases alidokeza kuwa hilo linawezekana.
Cases mwenyewe amethibitisha kuwa Rais
wa muda wa Barca, Josep Maria Bartomeu, amemhakikishia Klabu
haitamchukulia hatua yeyote, lakini Mwanachama huyo anataka Msimamo huo
uwe wa Kimaandishi.
Hata hivyo, hadi sasa haijulikani ikiwa
Cases ataamua kufuta Kesi kama Mahakama itakubali kuacha uchunguzi wake
wa Ubadhirifu wa Fedha ambao ukithibitika ni Kosa la Jinai.
0 comments:
Post a Comment