>>OLD TRAFFORD: MAN UNITED v CARDIFF, MATA, ROONEY & RVP NDANI!
>>VINARA ARSENAL UGENINI KWA ‘WATAKATIFU!’
LIGI KUU ENGLAND
BAADA KUPISHA FA CUP WIKIENDI, Ligi Kuu England inarejea dimbani Jumanne na Jumatano kwa Timu zote 20 kushuka Uwanjani.
ZIFUATAZO NI RIPOTI ZA VIKOSI/TATHMINI/RATIBA YA MECHI HIZO: 
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumanne Januari 28
2245 Man United v Cardiff
2245 Norwich v Newcastle
2245 Southampton v Arsenal
2245 Swansea v Fulham
2300 Crystal Palace v Hull
2300 Liverpool v Everton
MAN UNITED v CARDIFF
Ujio wa Mata ni habari njema kwa Man
United ambao Wiki iliyopita walibwagwa nje ya Capital One Cup kwa
Mikwaju ya Penati na Sunderland na Jumapili iliyopita walifungwa 3-1 na
Chelsea huko Stamford Bridge kwenye Mechi ya Ligi.
Mwezi Novemba walipokutana huko Mjini
Cardiff kwa mara ya kwanza tangu 1975, Man United na Cardiff City
zilitoka Sare 2-2 na hivi sasa Cardiff wapo chini ya Meneja mpya Ole
Gunnar Solskjaer ambae alikuwa Mchezaji Nguli hapo Old Trafford.
Katika Mechi yao ya mwisho ya Ligi,
Cardiff walichapwa 4-2 na Man City huko Etihad na kujikuta wako mkiani
kwenye Msimamo wa Ligi na kuendeleza mlolongo wao wa kutofanya vyema
Mechi za Ugenini kwani wameshinda Mechi moja tu.
Man United inatarajiwa kuwa nao
Mastraika wao Wayne Rooney na Robin van Persie ambao wamekuwa nje
kitambo baada kupona maumivu yao lakini itawakosa Nahodha wao, Nemanja
Vidic, ambae hii itakuwa Mechi ya Pili ya Kifungo chake cha Mechi 3
kufuatia Kadi Nyekundu aliyopewa kwenye Mechi na Chelsea, pamoja na
Majeruhi Rio Ferdinand (Goti), Nani (Musuli ya Paja) na Michael Carrick
(Enka).
Huenda Cardiff wakawa nae Mchezaji mpya
Kenwyne Jones kutoka Stoke City ambae amebadilishana na Peter Odemwingie
anaekwenda Stoke.
Pia, mpya mwingine kutoka Molde ya Norway, Jo Inge Berget, anaweza kuichezea Cardiff Mechi yake ya kwanza.
SOUTHAMPTON ARSENAL
Tangu wachapwe 6-3 na Man City Mwezi
Desemba, Arsenal wameshinda Mechi 7 mfululizo na hawajafungwa na
Southampton tangu Novemba 2002.
Staa wao Alex Oxlade-Chamberlain
amerejea dimbani tena baada kukosekana kwa majeruhi tokea Agosti baada
Juzi kucheza walipoitwanga Coventry Bao 4-0 kwenye FA CUP na pia Lukas
Podolski, ambae pia alikuwa nje kwa muda baada kuumia, amerejea kwa
kishindo na kwenye Mechi hiyo na Coventry alifunga Bao 2.
Arsenal bado itawakosa Majeruhi wa muda mrefu Abou Diaby na Theo Walcott, wote wakiwa na matatizo ya Goti.
Southampton, ambao wameshinda Mechi zao 3
zilizopita za Nyumbani, iatakuwa nao tena Majeruhi wao Rickie Lambert,
Artur Boruc na Mkenya Victor Wanyama lakini itawakosa Pablo Daniel
Osvaldo, aliefungiwa na Klabu baada kupigana Mazoezini, na Majeruhi
Dejan Lovren na Gaston Ramirez.
SWANSEA v FULHAM
Swansea City wanaichungulia Mechi hii na Fulham kama nafasi ya kushinda baada kutoshinda katika Mechi 8 za Ligi.
Mwendo huo mbovu umeitupa Timu hiyo
iliyo chini ya Meneja Michael Laudrup chini na wako Pointi 3 tu toka
Timu 3 za mkiani wakati Mwezi Desemba walikuwa Pointi 8 juu yao.
Lakini nao Fulham, chini ya Meneja Rene
Meulensteen ambae ni Kocha wa zamani wa Man United chini ya Sir Alex
Ferguson, nao wako taabani hasa kwa Mechi za Ugenini ambazo mara ya
mwisho kushinda ni Oktoba walipoichapa 4-1 Crystal Palace.
Tangu wakati huo, Fulham wamecheza Mechi 7 za Ugenini na kushinda moja tu na kufungwa Jumla ya Mabao 22 goals.
Lakini pia Swansea hawajashinda kwao
Liberty Stadium katika Mechi 3 zilizopita ingawa hizo zilikuwa Mechi
ngumu kwao dhidi ya Everton, Manchester City na Tottenham Hotspur.
Kwenye Mechi yao ya mwisho kati yao
Mwezi Novemba, Swansea waliishinda Fulham Bao 2-1 huku Bao la ushindi
likifungwa na Jonjo Shelvey katika Dakika 10 za mwisho lakini safari hii
Jonjo yuko nje akijiuguza enka.
CRYSTAL PALACE v HULL CITY
Hull City wanasafiri kwenda kucheza na Crystal Palace huku wakitaka kukwepa kipigo cha 4 mfululizo kwenye Ligi.
Steve Bruce, Meneja wa Hull iliyo Nafasi
ya 11, anatarajia kushinda ili kujinusuru kuburuzwa kwenye Timu za
mkiani lakini wana rekodi mbaya Uwanjani Selhurst Park ambako
hawajashinda katika Mechi 10 zilizopita kuanzia 1986.
Hull itamkosa Kiungo wao Tom Huddlestone
ambae alipewa Kadi Nyekundu katika Mechi yao iliyopita na pia itawakosa
Majeruhi James Chester, Joe Dudgeon na Sone Aluko.
Crystal Palace, chini ya Meneja Tony Pulis itawakosa Majeruhi Jack Hunt na Glenn Murray.
LIVERPOOL v EVERTON
Safari hii wanakutana huku Pointi 1 ikiwatenganesha kwenye Msimamo wa Ligi, Liverpool wakiwa Nafasi ya 4 na Everton Nafasi ya 6.
Katika Dabi yao ya mwisho, Mwezi Novemba
huko Goodison Park, Daniel Sturridge alifunga Bao mwishoni na kuipa
Liverpool Sare ya Bao 3-3.
Klabu hizi zina Mameneja wapya, Brendan
Rodgers kwa Liverpool na Everton ni Roberto Martinez, na wote hawajawahi
kuonja ushindi wa Dabi ya Merseyside.
Huku Liverpool wakiigeuza Anfield kuwa
ngome yao, kwa kufungwa Mechi moja tu Mwezi Septemba Southampton
waliposhinda 1-0, Everton wanakabiliwa na kibarua kigumu.
Kwa upande wa Majeruhi, Liverpool itawakosa Lucas Leiva (Goti), Jose Enrique (Goti) na Daniel Agger (Musuli za Mguu).
Everton watamkosa Mchezaji wao wa Costa
Rica, Bryan Oviedo, ambae alivunjika Mguu mara mbili Juzi kwenye Mechi
ya FA CUP na pia Majeruhi wengine Ross Barkley (Amevunjika Kidole cha
Mguu), Darron Gibson na Arouna Kone (Wote Goti.)
Lakini Everton huenda wakamtumia Mchezaji wao mpya Lacina Traore.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumatano Januari 29
2245 Aston Villa v West Brom
2245 Chelsea v West Ham
2245 Sunderland v Stoke
2245 Tottenham v Man City
0 comments:
Post a Comment