Monday, 27 January 2014

MOURINHO: NASKITIKA KUONDOKA KWA MATA ,LAKINI OSCAR NI BORA ZAIDI KWANGU

 
140107104916_juan_mata_mourinho_512x288_afp
Kocha wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amesema kuwa ulikuwa ni ‘uamuzi mgumu’ kwake kumwachilia mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya taifa ya Hispania Juan Mata kujiunga na wapinzani wao katika ligi kuu ya England Manchester United.
Mata aliye na umri wa miaka, 25, ameweka rekodi ya uhamisho katika klabu ya Man United kwa baada ya kuuzwa na Chelsea kwa kitita cha pauni milioni 37.1.
Akizungumza na BBC Mourinho amesema:
” Haya ni maamuzi ambaye mkufunzi anapaswa kufanya, lakini kwangu ilikuwa vigumu. Ningependa kuendelea kumuona katika kikosi changu bila shaka,”
“Lakini kuwa katika hali hii kwa mchezaji ni vigumu. Anastahili kuachiwa milango wazi katika Chelsea. Napenda kuwaona watu wakiwa na raha. Nasikitika sikuweza kumfurahisha katika kikosi hiki – nasikitika sana kwa hilo, lakini najenga kikosi changu nikizingatia mchezaji Oscar ambaye anacheza katika nafasi ya 10,” anasema mzee Mourinho.

0 comments: