Wednesday, 8 January 2014

MANISPAA YA IRINGA YALIA NA UJENZI HOLELA JUU YA MILIMA


Mstahiki  meya  wa Manispaa ya  Iringa  Aman Mwamwindi  akizungumza na wanahabari  leo kuhusu  mambo mbali mbali yanayoendelea
<
Ofisa habari wa manispaa ya  Iringa  Sima  Bingileki  akifuatilia kikao  hicho

HALMASHAURI  ya  Manispaaa ya  Iringa  imepiga marufuku ujenzi  holela  unaoendelea  katika milima ndani ya mji wa Iringa .

 Kauli  hiyo  imetolewa leo na mstahiki meya  wa Halmashauri  ya  Manispaa ya  Iringa Amani  Mwamwindi wakati  akizungumza na wanahabari  ofisini  kwake. 

Alisema   kuwa  udhaifu  wa  usimamizi  wa sheria  katika maeneo mbali mbali ndio  umepelekea  ujenzi  holela  kuendelea.

Hata  hivyo  alisema nyumba  ambazo  zinajengwa  kiholela  katika mji  wa Iringa zitaendelea  kuvunjwa  iwapo itabainika  kuwa  zimejengwa kiholela.

Kuhusu  uwekezaji  alisema  kuwa  vipo  viwanja kama  vitatu ambavyo  vinahitaji uwekezaji na  hivyo  kuwataka  wananchi  kujitokeza  kuwekeza katika maeneo hayo.

0 comments: