Saturday, 25 January 2014

KESI YA ANELKA KUZUNGUMZI WA FEBRUARI, ESSIEN AENDA RASIMI AC MILAN NA ROONEY KUBAKI HADI 2018

>>WENGER AKANUSHA KUMSAINI JULIAN DRAXLER WA SCHALKE!
ESSIENSOMA ZAIDI:
KESI YA 'QUENELLE' YA ANELKA KUSIKILIZWA FEBRUARI MWISHONI
Kesi inayomkabili Straika wa West Bromwich, Nicolas Anelka, kwa kutoaANELKA-SALUTESaluti ya 'quenelle' ambayo inatuhumiwa kama ni ya Kibaguzi itaanza kusikiliwa mwishoni mwa Februari kwa mujibu wa FA.
Anelka amepinga tuhuma hizo na akipatikana na hatia huenda akafungiwa Mechi 5 au zaidi.
Anelka, Miaka 34, alitoa Saluti hiyo ambayo Mkono mmoja unanyooshwa chini na mwingine kupita Kifuani na kuugusa mwingine, wakati alipofunga Bao kwenye Mechi na West Ham hapo Desemba 28 iliyokwenda Sare Bao 3-3.
Anelka alikabidhiwa Kabrasha la Kurasa 34 likielezea Tuhuma dhidi yake.
ESSIEN AENDA AC MILAN
Chelsea imethibitisha  kuwa imekubaliana na AC Milan kuhusu Uhamisho wa Michael Essien ambao hauna Dau lolote.
Essien, Miaka 31, ni Mchezaji wa Kimataifa wa Ghana, na Msimu uliopita alikuwa na Real Madrid kwa Mkopo na kuhamia kwake AC Milan kutamfanya awe ndie Mchezaji wa kwanza kusainiwa na Meneja mpya Clarence Seedorf.
Essien alianza kucheza Soka huko Ulaya kwenye Klabu ya Ufaransa Bastia akiwa na Miaka 17.
Mwaka 2003, Essien alijiunga na Lyon na kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi 1 Mwaka 2005 kabla Mwaka huo kuhamia Chelsea kwa Dau la Rekodi ya Klabu kwa wakati huo la Pauni Milioni 24.4 na kuichezea zaidi ya Mechi 250.
WENGER AKANUSHA KUMSAINI JULIAN DRAXLER WA SCHALKE!
Arsene Wenger amezitupilia mbali ripoti kuwa Winga wa Schalke Julian Draxler amesaini Arsenal kwa Dau la Pauni Milioni 37.
Wenger amesema anao Mawinga wengi na hatamsaini Draxler.
Akiongea baada ya Jana kuifunga Coventry 4-0 kwe FA CUP, Wenger alisema: “Hiyo ni dhana tu. Hamna kinachotokea, hapana, kweli, hapana. Hatuhitaji kusaini Mchezaji wa Wingi. Tunao Mawinga 17!”
WAYNE ROONEY AKARIBIA KUSAINI MKATABA MPYA OLD TRAFFORD!
ROONEY-NAMBA_10-MKONO_KICHWANIWayne Rooney anatarajiwa kusaini Mkataba mpya na Man United wa Miaka Mitano na utakaomlipa £300,000 kwa Wiki.
Ukisainiwa, Mkataba huu utamweka Old Trafford hadi 2018 na kuzipiga kibega Klabu za Chelsea, Real Madrid na Arsenal ambazo zimeripotiwa sana kumwinda.
Habari hii, ambayo imelipuliwa na Gazeti moja kubwa huko England likidai ni habari za uhakika toka ndani ya uongozi wa Manchester, zinakuja mara tu baada ya Man United kuthibitisha kumsaini Juan Mata toka Chelsea.
Rooney, ambae mara mbili ilidaiwa anataka kuiham Man United na Chelsea kutoa Ofa mbili mwanzoni mwa Msimu ili kumnunua,inasemekana aliwaamrisha Mawakala wake kuanza kuzungumza na Uongozi wa Man United mwanzoni mwa Mwezi huu ili kukubaliana Mkataba mpya utakaobadili huu wa sasa unaomalizika baada Miezi 18 na ambao unamlipa £250,000 kwa Wiki.

Related Posts:

0 comments: