Thursday, 13 February 2014

UKWELI KUHUSU MWENYEKITI IRINGA PRESS CLUB AKAMATWA NA KUACHIWA


KOKO_11111_5b656.jpg
Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Iringa
Frenck Leonard akiongea na waandishi baada ya kuachiwa na Polisi alipo kamatwa ndani ya mahakama wakimtuhumu kuvunjasheria wakati akisikiliza kesi ya Mshitakiwa wa mauaji ya Daud Mwangosi aliekuwa mwandishi wa Chanel ten na Mwenyekiti wa (IPC).

KOKO_222222_0ccf6.jpg
Waandishi wa habari Wakiwa viwanja vya mahakama ya wilaya iringa wakisubili kupata maelezo kwa msajili wa mahakama juu ya kitendo cha Polisi kumkamata Mwennyekiti wa IPC wakimshuku kuvunja sheria ndani ya mahakama kosa ambalo halikujulikana nakupeleke kumuachia huru.
KOKO__3333_6a612.jpg
Askari kanzu wakimpa ulinzi mtakatifu mshitakiwa wa kosa la mauaji ya aliekuwa muandishi wa chanel ten Daudi Mwangosi wakati ana toka mahakamani leo kwa kumpandisha katika gari maalumu ili asipigwe picha na waandishi baada ya kesi yake kuandikishwa rasimi katika mahakama kuu na itajadililiwa katika kikao kitakacho pangwa tayali kwa kusikilizwa.
 
WAKATI mahakama kuu kanda ya Iringa jana ikianza  kusikiliza kesi ya mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa Chanel Ten na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) marehemu Daudi Mwangosi ,polisi mjini Iringa waanza  kuwanyanyasa  wanahabari wanaofika kufuatilia  kesi hiyo baada ya kumkamata mwenyekiti wao Frank Leonard akiwa ndani ya mahakama wakati kesi hiyo ikiendelea.

Mwenyekiti  huyo alikamatwa  leo majira ya saa 5 asubuhi  wakati jaji  Mary Shangali  akiendelea kumsikiliza wakili wa  serikali Adoph Maganga  ambae  alikuwa akiwasilisha  baadhi ya vielelezo  muhimu  vya kesi  hiyo mahakamani  hapo.

Hata   hivyo katika  hali  iliyowashangaza  wananchi na  wanahabari   waliofika mahakamani  hapo  kusikiliza  kesi hiyo ni baada ya askari  mmoja kusimama ghafla  katika kiti  chache na kwenda kwa wakili wa  serikali na kurudi eneo ambalo wanahabari  walikuwa  wamekaa na  kumsimamisha Leonard  na kwenda kumpeleka kituo  cha  polisi kwa madai kuwa amepiga  picha mahakamani hapo  wakati   jaji akiendelea na kesi jambo ambalo si la kweli.

Akizungumia uamuzi huo  wa askari  hao  kumkamata  Leonard  alisema  kuwa aatambua taratibu zote za  kimahakama na  kuwa asingeweza kupiga  picha  wakati jaji akiendelea na kesi na kuwa  kilichotokea baada ya  kuingia mahakamani hapo kamera  yake  ilikuwa ndani ya mfuko  huku  yeye  akiendelea  kuchukua maelezo kwa  kuyaandika .

Hata  hivyo  alisema wakati  huo  simu  yake aliyokuwa ameiweka mfukoni wakati  akiitoa mfukoni na kutaka  kuiweka  vizuri askari  huyo aligeuka na kuona ameishika simu hiyo na hivyo  kuhisi kama amepiga  picha na kumkamata   na kutaka  kumbambikia kesi ya  kupiga  picha mahakamani  ila baada ya uchunguzi wa awali na maelezo ilibainika si kweli na ndipo alipoachiwa  huru na kutakiwa kuripoti baada ya muda kituoni hapo.

Kabla ya  kukamatwa  kwa  mwenyekiti huyo wa IPC  wanahabari  zaidi ya 10  waliokuwepo mahakamani hapa mapema  majira ya saa 2 asubuhi  walizuiwa  na askari polisi waliomfikisha mahakamani mtuhumiwa wa mauwaji hayo kuwa hawapaswi kuingia mahakamani kusikiliza kesi hiyo kabla ya kufikisha malalamiko hao kwa msajili wa mahakama ambae  alipinga  hatua ya jeshi la polisi kufukuza wanahabari mahakamani  hapo.

Hatua  ya  polisi hao  kumkamata  mwanahabari huyo  iliwalazimu  wanahabari  kumtafuta  kamanda wa  polisi mkoa wa Iringa kwa  njia ya simu ili kuhoji uhalali wa jeshi la polisi kuzuia wanahabari katika mahakama  hiyo na kwakesi hiyo ya askari anayetuhumiwa kufanya mauwaji ya Mwangosi.

Akizungumza kwa  njia ya  simu akiwa safarini kamanda Mungi  alisema polisi hawana mamlaka ya  kuwazuia  wananchi ama  wanahabari  wanaofika mahakamani kwani mwenye mamlaka ya kufukuza ama kuagiza kwa  mtu yeyote anayevunja sheria ndani ya mahakama kukamatwa  ni hakimu ama jaji anayesikiliza kesi na si polisi .

Hata hivyo  wanahabari  hao wameeleza  kusikitishwa na askari  polisi hao  kuendelea  kukandamiza uhuru wa  vyombo  vya habari katika  kesi hiyo ya Mwangosi huku kesi nyingine zikiwemo za  wana siasa  kufikishwa mahakamani kwa  tuhuma za  vurugu  polisi hao  wamekuwa wakionyesha urafiki wa hali ya  juu na wanahabari na hata  kuwapigia  simu ili kufika mahakamani  ila inapofika kesi ya mwenzao huyo  wamekuwa  wakiwageuka  wanahabari na kuwaona adui .

 Mtuhumiwa  huyo ambae   alifikishwa mapema zaidi  kuliko simu nyingine na gari  la polisi akiwa mbele aliondolewa mahakamani hapo kwa  kufishwa  kupita kiasi  na kuingizwa katika gari dogo  binafsi lenye namba T 165 BMP lililokuwa  likiendeshwa na  askari mwanamke (WP) huku vioo vya gari hilo vikiwa haviangazi kwa   ndani  huku  watuhumiwa wawili  wa mauwaji ambao  walikuwa na askari  huyo mahakamani hapo wakipakiwa katika karandinga la polisi.

Msajili wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Dunstan Nduguru aliwashangaa Polisi kwa kuingia shughuli za mahakama.

"Hata kama mwandishi huyo angekuwa anapiga picha, haikuwa kazi yao kumkamata mpaka wapewe agizo na Jaji Mfawidhi aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo," alisema.

Pamoja na askari hao kuwazuia wanahabari kuchukua picha mara baada ya mtuhumiwa huyo kufikishwa mahakamani, Nduguru alisema utaratibu wa mahakama unawaruhusu wanahabari kuchukua picha kabla shughuli kabla shughuli za mahakama hazijaanza na baada ya shughuli hizo kwisha.

"Kuwazuia wanahabari kufanya kazi zao kwa utaratibu huo sio sahihi; siku nyingine mkiona kuna dalili ya kupata bugudha kama hiyo naomba mnijulishe ili niondoe mzozo huo," alisema.

Mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Iringa, Mary Shangali, Wakili wa upande wa mashtka, Adolph Maganga alisema Adolph Maganda alisema kwa kukusudia mtuhumiwa Pacificius Cleophace Simoni anatuhumiwa kumuua Mwangosi kinyume na kifungu cha sheria ya kanuni ya adhabu namba 196 sura ya 16 kilichofanyiwa marejeo mwaka 2002.

Alisema katika tukio hilo lililotokea Septemba 2, 2012 katika kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa, mshtakiwa alifyatua bunduki yake na kusababisha kifo cha marehemu, papo hapo.

Alisema siku ya tukio marehemu alikuwa Nyororo kwa ajili ya kuripoti na kutoa taarifa kwa umma juu ya mkutano uliokuwa ufanywe na katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Alisema mshtakiwa akiwa mmoja wa wafanyakazi wa Polisi, waliwasihi Chadema wasifanye mkutano huo kabla wafuasi wake hawajaanza kurusha mawe kwa Polisi na baadhi yao kupata majeraha.

Kutokana na mzozo huo, wakili huyo wa serikali alisema polisi walipiga mabomu ya machozi ili kuwatawanya wafuasi hao kabla mshtakiwa huyo hajamfyatulia bomu marehemu.

Wakili huyo aliwasilisha ramani ya eneo la tukio, ripoti ya mtaalamu wa milipuko na ripoti ya daktari aliyechunguza mwili wa marehemu Mwangosi na gazeti la Mwananchi la Septemba 3, 2012 lililochapisha  picha ya tukio hilo katika ukurasa wa mbele kama vielelezo vinavyohusiana na kesi hiyo.

Wakili wa upande wa utetezi Lwezaula Kaijage alitaja mambo wanayokubaliana katika kesi hiyo kuwa ni jina na anuani ya mshtakiwa na kwamba marehemu Mwangosi alikufa kifo ambacho si cha kawaida.



Mtuhumiwa huyo wa mauwaji askari  wa FFU  Pacificus Cleophase Simon
aliyekuwa na miaka 23 wakati akitenda  kosa  hilo alisomewa  shitaka  hilo la kuua kwa kukusudia na wakili wa  serikali Maganga mbele ya jaji Shangali huku upande wa  utetezi  wakipinga baadhi ya vielelezo  kutumika mahakamani hapo kama ushahidi katika kesi  hiyo.

Wakili wa  serikali alisema kuwa moja kati ya  vielelezo  ni  pamoja na taarifa ya kifo  cha marehemu Mwangosi  vinavyoonyesha Mwangosi  aliuwawa ,pia mshitakiwa alihojiwa kwa onyo na Nidhamu na katika maelezo yake alikubali kosa ,tatu  mtuhumiwa huyo siku ya  tukio tarehe 2 septemba 2012 alikubali  kuwepo eneo la Nyololo ambako mauwaji hayo  yalifanyika  na kusikia mkuu wa  polisi Mafinga Aser Mwampamba akipiga  kelele kuwa anapigwa  kabla ya yeye  kufika na akiwa na silaha na  kufyatua risasi na kumuua Mwangosi .

Alisema wakili  huyo kuwa mtuhumiwa alikiri silaha  iliyoonyeshwa katika gazeti la Mwananchi la Septemba 3 mwaka 2012 kuwa ndio ilitumika  kufanya mauwaji hayo

Hata hivyo wakili wa upande wa utetezi Lwezaula Kaijage ulikubali  jina la mtuhumiwa na anwania  yake  pia  kukubali  kuwa  Mwangosi kweli alikufa kwa  kifo kisicho cha kawaida na hakuna  ubishi kama  alikufa  Nyololo pia  unakubali kuwa mtuhumiwa alikamatwa ila vingine vyote si  sahihi na kutaka  aliyehariri picha  katika gazeti la Mwananchi  kabla ya gazeti  hilo kutumika kama kielelezo kuitwa na kuhojiwa  pia hakuna uvbishi kama  mshtakiwa Simoni alikamatwa na amefikishwa mahakamani akihusishwa na mauaji hayo.

Kesi hiyo ina mashahidi 9 ambao nane kati  yao ni askari  na mhariri wa picha gazeti la Mwananchi  kesi  hiyo inataraji kuendelea  kusikilizwa katika kikao  kijacho kama hicho na mtuhumiwa huyo amekana shtaka  hilo.
Chanzo, Mnyalublogspot.com Francis godwinblog

Related Posts:

0 comments: