Aidan Pugili |
WAKALA
wa magazeti mjini Iringa, Aidan Pugili (34) amejitokeza kuwania ubunge
katika jimbo la Kalenga mkoani Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema).
Uchaguzi
mdogo wa kujaza kiti hicho kilichoachwa wazi na Dk William Mgimwa
aliyefariki Januari 1, mwaka huu, utafanyika Machi 16, mwaka huu.
Akitumia
umaarufu wake wa kuuza magazeti mjini hapa, Pugili aliyesindikizwa na
baadhi ya wauza magazeti wenzake alichukua fomu za Chadema kwa staili ya
aina yake huku akisindikizwa na magari madogo manne ya kukodi.
Akizungumza
na wanahabari mara baada ya kuchukua fomu hizo anazotarajia kuzirudisha
Jumanne, alisema amejipima na ameona anatosha kuiwakilisha Chadema
katika uchaguzi huo.
Kwa
mujibu wa taarifa rasmi kutoka katika chama hicho kura za maoni kwa
wagombea watakaojitokeza zitapigwa Jumatano ya Februari 12.
Pugili
ambaye pia ni mjasiriamali aliyewekeza biashara ndogondogo mjini Iringa
na Mbeya alisema tangu Chifu Mkwawa afariki dunia kwa kujiua mwenyewe
wananchi wa Kalenga iliyokuwa ngome kuu ya chifu huyo hawajawahi kupata
mwakilishi mwenye nguvu.
“Nina uwezo wa kuwa mwakilishi wao. Ni mzoefu katika siasa za upinzani na nimekuwepo ndani ya Chadema kwa muda mrefu,” alisema.
Alisema
ajenda yake ya kwanza endapo atapewa ridhaa ya chama chake na wananchi
wa jimbo la Kalenga itakuwa ni kupambana na ufisadi ndani ya halmashauri
ya wilaya ya Iringa.
Ajenda
yake ya pili alisema itakuwa ni kuleta mapinduzi katika kilimo kwa
kuwashawishi wagiriki wenye mashamba makubwa ya tumbaku katika jimbo
hilo kugawa ardhi wasiyoitumia kwa wananchi.
“Lakini ili kilimo kiwe na tija Chadema tunataka kuondokana na biashara ya kuwatumia mawakala kusambaza pembejeo,” alisema.
Alisema
watapigania uanzishwaji wa Mamlaka ya Kilimo Tanzania itakayosimamiwa
na serikali ili kuratibu kwa uhakika ukopaji na usambazaji wa pembejeo.
“Nataka
wananchi wa jimbo la Kalenga ambao asilimia 80 ni wakulima wanufaike na
kilimo ili waweze kupeleka watoto wao shule,” alisema.
Alisema afya na utalii zitakuwa ajenda zake zingine muhimu katika kinyang’anyiro hicho.
“Afya ni majisafi, matibabu na lishebor, nitapiga kuhakikisha wananchi wa Kalenga wanapata huduma hizo muhimu,” alisema.
Alisema
serikali ya CCM imeyatelekeza makumbusho ya Mkwawa yaliyopo Kalenga na
kufanya jimbo hilo na watu wake wakose mapato mengi kutoka kwa watalii.
“Nitahamasisha
utalii wa makumbusho hayo. Nataka dunia isisahau historia ya chifu
Mkwawa na katika hilo nitakuwa naenzi ushujaa wake,” alisema.
0 comments:
Post a Comment