Tuesday, 14 January 2014

JKT RUVU YAJIVUNIA MAFANIKIO YAKE MAKUBWA NA KUMTOA RAIS DR KIKWETE

8E9U3247
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga risasi hewani kuashiria kuzundua mafunzo  ya JKT kwa vijana katika kambi ya RUVU JKT yatakayo itwa Operesheni Miaka Hamsini (picha na maktaba)

Maadhimisho  ya  miaka  50  ya  jeshi  la  kujenga  taifa  JKT  Ruvu  yameadhimishawa   leo  mlandizi  nje  kidogo   ya    jiji  la Dar  es  salaam  huku   kikosi  hicho  kikijivunia  mafanikio  makubwa  ndani  ya  miaka  hiyo  ikiwa  ni   pamoja  na  kikosi  hicho  ndicho  kikosi  pekee  ambacho  kimetoa  amili  jeshi  mkuu  ambaye  ni  Rais  wa  jamuhuri    ya  muungano  wa  Tanzania  mheshimiwa  Jakaya  Mrisho  Kikwete  pamoja   na  Mama  Salma  kkwete.

Akizungumza  katika  maadhimisho  hayo  mkuu  wa  kikosi  kamanda  luten  kanal    Charles  Mbuge  alisema  kuwa  hadi  sasa  wanamengi  ya  kujivunia  katika  kikosi  hicho  ambayo  ni  pamoja  na  kuanzisha  miradi  mbalimbali  ya  ufugaji  wa  ng’ombe  na  kuku  wa  kisasa.

Naye  mkuu  wa  JKT  meja  jenerali  Raphaeli  Muhuga  ambaye  ndiye  alikua  mgeni  rasmi  katika  maadhimisho  hayo  lisema  kuwa  kikosi  cha  JKT  Ruvu  kimeweza  kuzalisha  mali  kwa  ubunifu  mkubwa  pamoja  na  kubuni  miradi  mingi  na  hakuna  mradi  ambao  haujabuniwa  katika  kikosi  hicho  na  kuongeza  kuwa  kikosi  cha  Ruvu  kimekuwa  ni  kioo  kwa  taifa  kutokana  na  kufanya  shughuli  nyingi  ikiwa  pamoja  na  shughuli  za  kitamaduni. 

Aidha  Meja  jenerali  Muhuga  katika  maadhimisho  hayo  amefanya  uzinduzi  wa  bohari  la  kulia  chakula,saloon  pamoja  na  chumba  cha  kopyuta  na  kuahidi  kutoa  kopyuta  5.

Pamoja  na  hayo   naye  muanzilishi  wa  JKT  Ruvu    Brigedia  Jeneral  mstaafu  Dismas  Msilu  alisema  kuwa  uwajibikaji  wa  vijana  wa  sasa  unaridhasha  kutokana  na  vijana  wengi  wa  sasa  ni  wasomi    kwahiyo  hata  namna  ya  kufundisha  ni  tofauti  na  ile   ya  awali  ambapo  wengi  walikuwa  ni  vijana  waliomaliza  darasa  la  saba  na  la  nane  na  kusema  kuwa  kwa  wakati  huo  ilimbidi  aende  nao  kwa  utaratibu  katika  mafunzo.
 
Hata  hivyo  mstaafu  Brigedia  jeneral  Dismas  Msilu  alizungumzia  swala  la  kurudisha  kwa  mafunzo  ya  JKT  kwa  vijana  na  kusema  kuwa  hali  hiyo  ilivyorudishwa  inasaidia  sana  kwa  vijana  kuwawek a  mahalai  pamoja  na  kuwafundisha  siasa  na  kupata  elimu  ya  namna  ya  kujitegemea 
 CHANZO Na Kenneth  John wa  matukiodaima.com,Dar es Salaam

Related Posts:

0 comments: