Wednesday 30 April 2014

NI HATARI! MOURINHO AWAPA ZA USO WAJUAJI WA MPIRA KULIKO YEYE

396477_heroa 
ZIKIWA zimebaki saa chache kushuhudia timu itakayoungana na Real Madrid katika mchezo wa fainali ya UEFA mei 24 mjini Lisbon nchini Ureno kati ya Chelsea au Atletico, Jose Mourinho ametetea mbinu yake ya kupaki basi inayolalamikiwa na makocha wengi. 
Mourinho amesema kuwa kuna falsafa nyingi za soka na anashangaa wanaolalamika juu ya mbinu zake kwasababu asingefanya hivyo angekuwa anafungwa mara nyingi.
 
Kocha huyo raia wa Ureno alilalamikiwa `kupaki basi` na Atletico Madrid kwenye uwanja wa Vicente Calderon na kulazimisha suluhu ya bila kufungana.
 
Jumapili iliyopita, alitumia mbinu kama hiyo na kuwafunga Liverpool mabao 2-0 uwanja wa Anfield na kufufua matumaini kidogo ya kutwaa ubingwa, lakini kocha wa majogoo wa jiji Brendan Rodgers alimlalamikia Mourinho kwa kupaki basi na kusema anacheza mpira wa kizamani.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: