Thursday 24 April 2014

IRINGA KUADHIMISHA SIKU YA MALARIA KESHO IJUMAA


Ikiwa imebakia siku moja kabla ya kuadhimisha siku ya Malaria Duniani, wakazi wa Iringa wametakiwa kuwa makini na ugonjwa huu hatari unaoua mamia ya watu kila mwaka.

 

Akizungumza na mtandao  wa  wandishi  wa habari  ofisini kwake Mratibu wa kuthibiti malaria Manispaa ya Iringa Dokta Nicolous Ntabaye alisema kuwa maadhimisho hayo ya kuthibiti malaria dunia huwa yanafanyika kila tarehe 25 Aprili na kusema thumuni la kufanya maadhimisho hayo ni pamoja na kuthibiti uongezekaji wa ugonjwa huo hatari wa malaria.

 

“sisi kama Manispaa tumejipanga vizuri kwa kuwaasa wananchi wetu kuwa waangalifu na ugonjwa huu wa malaria na mikakati tukiyojiwekea kwa wananchi wa Iringa ni pamoja na kuwaasa wahakikishe mazingira yanayowazunguka yawe safi na salama, mama wajawazito wahakikishe wanatumia vidonge vya SP ili kumkinga mtoto aliyeko tumboni asipatwe na malaria pia kuendelea kutumia vyandarua vilivyowekwa dawa na endapo mtu akijua ana dalili za maralia ahakikishe anawahi kwenda hospitali akapatiwe matibabu mapema,” alisema Dokta.

 

Hata hivyo ametoa wito kwa wamama wajawazito kuhakikisha wanapewa vidonge vya SP dozi mara tatu kwa miezi yake tisa mpaka atakapojifungua ili kumfanya mtoto azaliwe katika afya njema na asipatwe na ugonjwa wa malaria kwa kufanya hivyo uongezekaji wa malaria utapungua Nchini.

 

Maadhimisho hayo ya ugonjwa wa Malaria yanatarajia kufanyika kesho huku kauli mbiu ikiwa “wekeza katika muda wa baadaye, tokomeza Malaria”.

 

HABARI  NA DIANA BISANGAO  , IRINGA

0 comments: