MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Sunday 27 July 2014

UJIO WA REAL MADRID TANZANIA SASA YAWA GUMZO NCHINI


FIGO


Gumzo la ujio wa wakongwe wa Real Madrid sasa umeanza kuwa gumzo kuliko hata ilivyotarajiwa awali.
Mwanzo ilionekana kama wengi hawaamini kama kweli wakongwe hao wa Madrid wanaweza kuja nchini.
Baadhi wametuma baruapepe kwenye mtandao huu wakihoji kama ni kweli.
Wengine walitaka kujua kama kweli wachezaji kama Luis Figo au Raul Gonzalez wanaweza kukanyaga ardhi ya Tanzania.
“Maandalizi yanaendelea vizuri kama tulivyosema awali na watu wanapaswa kuamini kuwa kweli Madrid wakongwe wanakuja.
“Hii ni nafasi kubwa kwa Watanzania kukutana na nyota hao na kuwaona wanacheza, hivyo wajiandae kupata burudani hiyo,” alisema Ssebo ambaye ni mratibu wa ziara hiyo.
Wakali hao watakipiga na nyota wa Tanzania ambao watajumuishwa pamoja katika mechi itakayopigwa Agosti 23 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salam.

ETO'O AIFUNGIA MABAO MAWILI BARCELONA DHIDI YA PORTO

  KATIKA MCHEZO WA KUMUAGA DECO

VIKOSI viwili vilivyoshinda mataji ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa awamu tofauti jana viliungana kuichezea Barcelona katika mechi dhidi ya FC Porto, kumuaga kiungo wa zamani wa kimataifa wa Ureno, Deco.
Mchezo huo uliowahusisha wachezaji nyota kama Lionel Messi, Eidur Gudjohnsen, Benni McCarthy na Paulo Ferreira, ulimalizika kwa sare ya 4-4, huku Samuel Eto'o akifunga mabao mawili na Deco aliyechezea nusu moja kila timu, akiifungia bao moja kila timu, likiwemo la mwisho la Porto lililoamua matokeo.
Mabao ya Porto yalifungwa na Derlei dakika ya tatu, McCarthy dakika ya 15, Jankauskas dakika ya 62 na Deco dakika ya 89, wakati ya Barca yalifungwa na Eto'o dakika za 54 na 68, Deco 57 na Messi 81.
Kikosi cha Porto kilikuwa: Baia, Ferreira, Costa, Emanuel, Valente, Costinha, Maniche, Mendes, Deco/Jankauskas dk46, Derlei na McCarthy.
Barcelona: Jorquera, Oleguer, Belletti, Gerard, Sylvinho, Davids, Van Bommel, Van Bronckhorst, Giuly/Deco dk46, Ezquerro/Eto'0 dk46 na Gudjohnsen/Messi dk46.
Messi na Deco wakimpongeza Eto'o baada ya kufunga
Magwiji: Samuel Eto'o na Deco wakisalimiana Uwanja wa Estadio de Dragao mjini Porto kabla ya mchezo
A familiar sight: Messi streaks past two defenders who end up on the floor trying and failing to take the ball off the Barcelona maestro on his first game after the World Cup
Messi akiwatoka mabeki wa Poro
Still got it: Former Blackburn and Porto striker Benni McCarthy vies for the ball with former Barcelona defenders Sylvinho and Oleguer
Benni McCarthy akipambana katikati ya Sylvinho na Oleguer

MAN UNITED YASHINDA CHINI YA VAN GAAL ...ROONEY HATARI!!!!!!!!

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa England, Wayne Rooney amemdhihirishia ubora wake kocha mpya wa Manchester United, Mholanzi Louis van Gaal usiku huu baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-2 dhidi ya AS Roma mjini Denver, Marekani. 
Katika mchezo wa kujianda na msimu, Rooney alifunga katika dakika za 36 na 44 kwa penalti, wakati bao lingine la United lilifungwa na Juan Mata dakika ya 39.
Mabao ya Roma yalifungwa Miralem Pjanic dakika ya 75 na mkongwe Francesco Totti kwa penalti dakika ya 88.

Anatisha: Rooney akishangilia na wenzake, Antonio Valencia na Ander Herrera baada ya kufunga bao la kwanza
Opener: Rooney opened the scoring for United with a sublime strike from 25 yards in Denver
La kwanza: Rooney alifunga bao la kwanza kutoka umbali wa mita 25 mjini Denver
On form: Juan Mata scored with a superb lob as the first-half came to a close
Yuko vizuri: Juan Mata alifunga bonge la bao kipindi cha kwanza

Mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Allen Chapman mbele ya mashabiki 54,117, Rooney aliibuka mchezaji bora baada ya filimbi ya mwisho.
Kikosi cha Manchester United kilikuwa; Johnstone/Amos dk45, Blackett, Jones/M Keane dk45, Evans/Smalling dk45, Valencia/Young dk45, Herrera/Nani dk45, Cleverley/Hernandez dk69, Mata/Kagawa dk45, James/Shaw dk45, Rooney/W Keane dk45 na Welbeck/Lingard dk45.
AS Roma; Skorupski, Calabresi/Somma dk45, Benatia, Romangnoli/Castan dk45, Emanuelson/Cole dk45, Ucan, Keita/Pjanic dk68, Iturbe/Ljajic dk45, Paredes/Nainggolan dk45, Florenzi/Totti dk6 na Destro
Spot: Rooney scored his second and United's third from the penalty spot as his side ran riot before the break
Tuta: Rooney akifunga kwa penalti
Mine: Rooney stretches in an attempt to get the ball from Mattia Destro
Rooney akigombea mpira na Mattia Destro

LEWANDOWSKI APIGA BAO LA MWAKA KWA BAYERN MUNICH

MCHEZAJI mpya wa Bayern Munich, Robert Lewandowski jana ameendelea kung'ara katika timu yake mpya baada ya kufunga bao zuri katika safe ya 2-2 na Borussia Monchengladbach mchezo wa kujiandaa na msimu.
Mshambuliaji huyo wa Poland aliyetua kama mchezaji huru kutoka wapinzani wao wa Bundesliga, Borussia Dortmund -tayari amefunga mabao mawili tangu awasili.
Bao la pili ni la jana alipomtungua kipa mbele ya mabeki wake wanne ndani ya boksi.
Bao tamu: Robert Lewandowski akipitisha mpira juu ya mabeki na kipa wao kufunga bao zuri
Happy days: Lewandowski gets the congratulations from Franck Ribery on his Bayern return
Siku za furaha: Lewandowski akipongezwa na mwenzake Franck Ribery aliyerejea Bayern baada ya kupona

Na baada ya Bayern kutoa safe ya 2-2 mchezo ulihamia kwenye mikwaju ya penalti, ambako walishinda, na ilikuwa ni furaha mno kwa Franck Ribery aliyerejea uwanjani baada ya kupona maumivu yaliyomfanya akose fainali za Kombe la Dunia.

RAIS KIKWETE ,JUMUIYA YA MADOLA NA MICHEZO YOTE WAMEKUDANGANYA MCHANA KWEUPE!



Rais wangu, Jemedari wangu na Amiri Jeshi mkuu wa Nchi yangu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete Vyama vya Michezo na Wizara ya Michezo Imekudanganya na kukufanya wewe kama Babu yao.

Rais Tangu uingie Madarakani  Mwka 2005 umekutana na Viongozi wa  Vyama Mbalimbali vya michezo kwa Bahati Mbaya hakuna kiongozi hata mmoja aliyekueleza ukweli wengi wao waliomba kitu ambacho sio sahihi pengine walikuwa wanakuogopa lakini naweza sema hawajui kutumia nafasi Adhimu ya Kukutana na wewe uso uso! 

Watu waliokudanya Zaidi hivi karibuni ni wanamichezo waliokwenda kushiriki Jumuiya ya Madola pale Glascow Uskochi hawa walikuwa wanalia kwa Muda Mrefu sana maandalizi ,Maandaliz Mzee wangu Ukasema isiwe Tabu ukawapeleka Kambi Nje wakaa kwa Muda walioona unafaa, Binafsi yangu niliona kuwa hakuna cha timu pale! ni ubabaishaji mtupu hayo yaliwahi kufanywa hata na Rafiki yako Maximo kuipeleka Stars Brazil .

Timu hii ya Jumuiya ya Madola ambayo inawachezaji wa Riadha,Ngumi,Judo ,Kuogelea,  kwangu mimi hakuna Tofauti na kikosi cha mastaa wa Real Madrid wanaokuja Kutariii na sio kucheza soka Zidane,Figo,Salgado Hawaji kucheza mpira wanakuja kutarii .
Hivi Rais wangu wanakuja na dawa za kukufanya uingine mkenge au?  maana wanakudharirisha tu hawa 
Ningekuwa mimi Ndio napata Bahati ya Kukutana nawewe uso kwa uso ningeomba yafutayao kwako katika michezo.

Kwanza kabisa ningekuomba ujenge shule tano  kuu za michezo tofauti ukiziweka katika Kanda tofauti shule ya Riadha Arusha ,soka Dar es salaam na Zanzibar ,Masumbwi Musoma,kuogelea mikoa kanda ya Ziwa   pamoja na Pwani ,kwanini nasema hivi Sisi shida yetu ni Maandalizi ya awali sio kuchukua watu ambao wamekwisha komaa ndo kuwapeleka Uskochi  wamekwenda kutarii Mh Rais kwa utaratibu tulionayo sasa sidhani kama tutafanikiwa kama ulivyowahi kusema wewe mwenyewe wakati ukipokea ujio wa Kombe la Dunia "Mpaka Mwisho Dunia hatutofanikiwa ni kwa mambo kama haya hawakuelezi ukweli !

Mimi nakueleza Rais wangu Inawezekana aliyetuloga katangulia mbele ya haki sababu haiwezekani tunachemka kila siku halafu tunakaa na kubandika kwenye magali yetu Picha za Usain Bolt,Beckham,Causic Clay Mohammed Ally .

Mbona hakuna Picha za Nyambui,au Ikangaa kwa sababu hakuna shule za michezo na hakuna anayewajua  wachezaji tuliopeleka wanatakiwa kuwa makocha na sio wachezaji Mh rais nahuzinika kuwa utakapotoka madarakani utoka kama kaka yako Mkapa Bila kumtunza mwanamichezo yoyote aliyeleta Medali katika michezo ya kimataifa sizungumzii waliofanya vizuri kwenye klabu au timu za nchi Nyingine wakati mwingine huwa najiuliza Hivi ni Laana au Tumelogwa tu Mkuu mbona wanakufedhehesha Kila siku wanasema hoo hari ya Hewa hivi hiyo hewa wanayosema mbona kenya ,Uganda,Ethiopia Nigeria Ghana haziwaathiri au wenzetu wanavuta hewa Tofauti na tunayovuta sisi .

Rais Kikwete hawa Vijana wanakuhujumu Mimi nakuhakikishia kama hatutajenga shule za michezo zenye ubora wa Kimataifa na kuweka Viongozi sahihi hatutofanikiwa mpaka Yesu ninae mwanimini au Isah Bin Mariam unavyomwita wewe atakaporudi Tena kuchukua watu wake na hata kama hakasamehe Dhambi tulizofanya akaamua kuchukua watu kwa Medali walizoshinda kwenye michuano Mbalimbali bado tutashindwa kwenda Mbiguni . Kikwete umehujumiwa na Tasnia ya wanamichezo wanao Taka mafanikio Bila kufa .
Kazi unayo Mkuu wangu wa Nchi.

NAIBU WAZIRI AMOS MAKALLA ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA MAREKANI

 


 Naibu Wazirti wa Maji, Amos makalla akiwa na balozi wa Tanzania nchini marekani balozi Liberata Mulamula katika ubalozi wa Tanzania Marekani.

DIAMOND ALAMBA TUZO MBILI AFRIMMA 2014

Zinaitwa African Muzik Magazine Awards ambapo za mwaka huu 2014 zimetolewa huko Eisemann center Texas Marekani na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali akiwemo Diamond wa Tanzania ambae pia alikua mmoja wa wanaowania tuzo.
Good news kwa mujibu wa meneja Babu Tale ni kwamba Diamond ameshinda tuzo mbili moja ya Msanii bora wa Afrika Mashariki na nyingine ni wimbo bora wa kushirikiana ambao ni ‘number one rmx’ alioufanya na Davido wa Nigeria.
Kolabo bora ni tuzo iliyokua inawaniwa na single ya T Pain na 2 Face – rainbow, Khona ya Uhuru na Mafikizolo wa South Africa, Surulere remix ya Dr Sid wa Nigeria, Mkenya Amani ft. Waganda Radio na Weasel ‘kiboko changu’ J Martins ft. Dj Arafat ‘touching body’ na Rebees na Wizkid ‘slow down’
Tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika Mashariki aliyoishinda Diamond ilikua inawaniwa pia na Ben Pol kutoka Tanzania, Bebe Cool wa Uganda, Wyre wa Kenya, Navio wa Uganda na Jackie Gosee wa Ethiopia.
Lady Jaydee ameshinda tuzo ya Msanii bora wa kike Afrika Mashariki aliyokua anashindania na Rema wa Uganda, Aster Aweke wa Ethiopia, Avril wa Kenya, Victoria Kimani wa Kenya na Irene Ntale wa Uganda.
Producer bora wa mwaka tuzo yake imechukuliwa na Mtanzania Sheddy Clever aliekua anashindana na Don Jazzy wa Nigeria, Shizz wa Nigeria, Killbeatz wa Ghana, Oskido wa South Africa, Nash Wonder wa Uganda na Ogopa wa Kenya.
Tuzo ya Mtayarishaji bora wa video imekwenda kwa Ogopa Dj’s ambao ndio waliifanya ile video ya kwanza ya ‘My number 1′ ya Diamond Platnumz.
Screen Shot 2014-07-27 at 8.17.33 AM

Tuzo zenyewe zimetolewa kwenye hili jengo
Stori zaidi na pichaz vitafata baadae hivyo endelea kukaa karibu na Baakubwamagazine.com ili ujue kilichotokea kwenye tukio hili ambalo limewahusisha wakali wengine kama Davido, 2Face, Fally Ipupa, Iyanya, Flavour, Wyre, Miriam Chemmoss na wengine ambao ni sehemu ya watu kutoka nchi 17 za Afrika.

ANGALIA BASI LA HOOD LlLIVYO PATA AJALI MBAYA LIKITOKEA MBEYA


Muda mchache baada ajali kutokea 
 Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo


 Basi la Hood limepata ajali asubuhi hii likitoka Mbeya haijafahamika mara moja lilikuwa linaelekea wapi na haijafahamika kama kuna watu waliojeruhiwa, endelea kufutilia hapa kupata taarifa kamili hii ni taarifa ya awali.

Picha Kwahisani ya Mbeya yetu Blog

Saturday 26 July 2014

ASERNE WENGER AFICHUA SIRI YA KUOKOA KIWANGO CHA AARON RAMSEY


Wenger reveals pep talk that revived Ramsey’s career

BOSI wa Asernal, Mfaransa, Aserne Wenger amefichua siri kuwa alikaa kwa kirefu na Aaron Ramsey kwa lengo la kuzungumza naye ili kunusuru kiwango cha nyota huyo wa Wales.

Majeruhi ya mfululizo iliathiri sana kiwango cha nyota huyo mwenye miaka 23, lakini alionekana kuwa msaada katika klabu ya Asernal wakati wa harakati zake za kumaliza ukame wa miaka 9 bila kikombe msimu uliopita.

Baada ya kukaa chini na kocha wake, Ramsey aliibuka tena na kuwa moja ya wachezaji nyota wa ligi kuu msimu uliopita, akifunga mabao 16 na kuisadia Asernal kutwaa kombe la FA.

“Nilikaa chini na Aaron na nilimwambia, ‘Sidhani kama watu hawakupendi, lakini hawapendi mchezo wako kwa wakati huu’, Mfaransa huyo alieleza wakati wa ziara yao ya maandalizi ya kabla ya msimu nchini marekani.

“Alitakiwa kurejea katika mchezo wake….halafu ulimuona mchezaji tofauti, kwasababu ana akili, na baada ya kutoka katika mazungumzo, nilijua kijana ataweza kurudi  upya”.


Ramsey alianza katika ushindi wa Asernal wa mabao 2-0 dhidi ya Boreham Wood, ukiwa ni mchezo wao wa kwanza wa kirafiki wakati huu wa maandalizi ya kabla ya msimu, na anatarajiwa kucheza dhidi ya New York Red Bulls siku leo jioni.

MARCIO MAXIMO AHITAJI KUONA UWEZO WA KHAMIS KIIZA NA EMMANUEL OKWI



Maximo ahitaji kuona uwezo Kiiza na Okwi.
Baada ya Maximo kumsajili Jaja Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo wamekuwa wakiumiza kichwa kutaka kujua mchezaji gani kati ya Kiiza na Okwi atakatwa kwenye usajili

 
KOCHA wa Yanga Marcio Maximo amesema pamoja na kumpa mkataba wa miaka miwili Mshambuliaji Geilson Santana Santos ‘Jaja’lakini bado anahitaji kuona uwezo wa washambuliaji wawili raia wa Uganda Hamisi Kiiza na Emmanueli Okwi.
Maximo ameiambia Goal kwamba anataka kuwa na timu imara itakayohitaji wa wachezaji wote na siyo mchezaji mmoja mmoja kama zilivyo baadhi ya timu nyingine ambazo ikitokea mchezaji huyo anaumwa zinashindwa kufanya vizuri.
“Nalazimika kuwaona mazoezini Okwi na Kiiza ndiyo nitakuwa na jibu la kusema lakini kwa sasa bado ni mapema mno kusema nitampunguza nani kwa sababu hata katika rekodi za klabu naona wachezaji hawa wamekuwa na mchango mkubwa ndani ya timu ukitoa usumbufu ambao inasemekana wanao,”alisema Maximo.


Baada ya Maximo kumsajili Jaja Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo wamekuwa wakiumiza kichwa kutaka kujua mchezaji gani kati ya Kiiza na Okwi atakatwa kwenye usajili wa msimu ujao huku kila mtu akiwa na mapendekezo yake.
Chanzo:Goal.com

KOCHA WA ZAMANI STARS ASEMA KIKOSI CHA NOOIJ KITAING'OA MSUMBIJI


Imechapishwa Julai 26, 2014, saa 6:53 mchana

Aliyewahi kuwa Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh, amesema uwezo ulioonyeshwa na timu hiyo katika mechi yake dhidi ya Msumbiji ni mkubwa na anaamini itashinda katika mchezo wa marudiano.
Stars ilikutana na Mambas ya Msumbiji wiki iliyopita katika mchezo wa kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika inayotarajiwa kufanyika mwakani nchini Morocco ambapo katika mchezo wa awali, ilifanikiwa kutoka sare ya mabao 2-2.
Mambas ni moja kati ya timu ambazo zimekuwa zikiisumbua Stars kwa muda mrefu pindi zinapokutana nayo.
Marsh amesema kuwa mwenendo wa timu hiyo kwa sasa ni mzuri kufuatia maandalizi waliyoyafanywa na kuwataka Watanzania wasiwe na haraka ya kupata mafanikio, kwani hali hiyo hutokea hata katika maisha ya kawaida.
“Uwezo wa Stars kwa sasa upo juu ya Mambas kwa jinsi nilivyowaona walivyocheza katika mechi ya kwanza licha ya kutoka sare, hivyo nina imani kubwa kuwa itashinda na kuitoa katika mchezo wa marudiano.
“Tumeweza kuona katika mchezo wa awali tulifanikiwa kuitoa Zimbabwe licha ya kuwa na matokeo mabaya ya awali katika uwanja wa nyumbani.
“TFF imejitahidi kwa kiasi kukubwa kuiandaa timu hiyo kwa kukaa kambi kwa muda mrefu na kuipeleka nje ya nchi kwa ajili ya kujiandaa pamoja na kucheza mechi za kirafiki, ambapo imebadilika kwa kiasi kikubwa, hivyo ni vyema wadau wakawa na subira kuhusiana na suala hilo ili timu iweze kufanya vizuri hapo baadaye,” alisema Marsh.

Chanzo: Salleh Ally

HII NDIYO SABABU YAJOSE MOURINHO KUGOMA KUMSAJILI LUKE SHAW?, SOMA HAPA.......


Just a kid: Mourinho says he didn't want to sign Shaw because of his extraordinary wage demands
Mtoto: Mourinho amesema hakutaka kumsajili Shaw kwasababu mshahara wake ni mkubwa sana.

 

JOSE Mourinho amesema hakuthubutu kutaka kumsajili Luke Shaw kwasababu mshahara aliohitaji kinda huyo `ungeua umoja' wa timu kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.
Shaw mwenye miaka 19, alisaini Manchester United kwa dau la paundi milioni 30 na inasemekana atakuwa analipwa mshahara wa paundi laki moja na elfu 20.
Mourinho alisema kiwango hicho ni kikubwa sana kwa klabu yake.
‘Kama unamlipa mshahara mkubwa kijana mwenye miaka 19 Luke Shaw, tulikuwa tunahitaji nini?, tungekufa' alisema kocha wa Chelsea. "Tungeua umoja na utulivu wetu katika matumizi ya hela. Tungeua umoja kwenye vyumba vya kubadilishia nguo".
"Kwasababu unapomlipa zaidi mtoto wa miaka 19-mchezaji mzuri, wa ajabu-siku inayofuata, mimi na (Mkurugenzi wa Chelsea) bwana Mrs Granovskaia na (mkurugenzi wa ufundi) Michael Emenalo tutagongewa milango na wachezaji wakisema inawezekanaje tumeichezea klabu mechi 200 na kushinda hili na lile, lakini bwana mdogo anatuzidi mshahara?
New mould: Diego Costa, Cesc Fabregas and Filipe Luis joined Chelsea this summer, along with Didier Drogba
Kifaa kipya: Diego Costa, Cesc Fabregas na Filipe Luis wamejiunga na Chelsea majira haya ya kiangazi, sambamba na Didier Drogba.

"Inawezekanaje kijana wa miaka 19 anakuja hapa na kupata hela ambazo hata mimi sipati? ningeua usawa wa timu na nisingeruhusu hilo kutokea".

'Filipe Luis aliichezea Brazil, ameshinda makombe ya Ulaya, alicheza nusu fainali ya UEFA, huyu mchezaji ni bei rahisi kuliko huyu mtoto wa England?
"Sikosoi klabu nyingine kwa kumlipa vile. Lakini kwa klabu yangu, tunaweza kusema ingekuwa mbaya kwetu".
Comparing: Mourinho noted how Filipe Luis cost much less than the 'English young lad' Shaw
 Mourinho alisema inawezekanje Filipe Luis anakuwa na bei rahisi kuliko mtoto wa England, Shaw.

MKURUGENZI AC MILAN ASEMA KWA ASILIMIA 99.9% MARIO BALOTELLI HANG'OI MGUU!



Happy in red and black: Mario Balotelli looks as if he won't be moving from AC Milan this summer
Ana furaha katika rangi nyekundu na nyeusi: Mario Balotelli anaonekana kama vile ataondoka katika klabu ya  AC Milan majira haya ya kiangazi.

 

DHAMIRA ya Arsenal kutaka kumsajili Mario Balotelli inaonekana kufa , baada ya Mkurugenzi wa AC Milan,  Adriano Galliani kudai mshambuliaji huyo mtukutu atabakia klabuni hapo.
Mshambuliaji huyo wa kati wa zamani wa Manchester City amekuwa akihusishwa kujiunga na Aserne Wenger na hata Rais wa Ac Milan,  Silvio Berlusconi alikaririwa mapema majira ya kiangazi akisema: 'Nilikuwa namuuza Balotelli kwa timu za England kwa mamilioni ya fedha".
Hata hivyo,  Galliani amejitokeza na kusema hakuna uwezekano wa nyota huyo kutua England kwasababu mshambuliaji huyo mwenye miaka 23 yupo katika mipango ya klabu msimu ujao.
Winner: Balotelli celebrates scoring against England for Italy during the World Cup group stages
Mshindi: Balotelli akishangilia baada ya kufunga bao la ushindi katika mchezo wa kombe la dunia hatua ya makundi dhidi ya England.

'Balotelli kamwe hajawahi kuomba kuuzwa,' Alisema Galliani. 'Kuna asilimia 99.9% ana nafasi ya kubakia hapa, lakini huwezi kujua nini kitatokea".
Japokuwa washika bundiki hawajapoteza nafasi kwasababu Mkurugenzi wa Milan aliwahi kusema hivyo hivyo kuhusiana na Mbrazil Kaka, akisema: 'Ni kweli tutambakisha hapa. Nina asilimia 99.9%, atabakia hapa'.
Lakini Kaka aliondoka na kujiunga na Orlando City kwa mkopo kupitia klabu ya Sao Paulo.
Lakini Wenger alikaririwa akisema anafurahia wachezaji alionao safu ya ushambuliaji na kuonekana kama vile amepiga chini dili la kumsajili Balotelli majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Him again: Former Man City star Balotelli (left) has been linked with a move to Arsenal
Yeye tena: Nyota wa zamani wa Man City, Mario Balotelli (kushoto) amekuwa akihusishwa kujiunga na Asernal.