MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Wednesday 30 October 2013

SIMBA, KAGERA SUGAR KUKUTANA LEO ALHAMISI


>> PAMBANO LA SIMBA, AZAM LAINGIZA MIL 64/-
PATA ZAIDI:
Release No. 186

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UWANJA_WA_TAIFA_DAROktoba 29, 2013
PAMBANO LA SIMBA, AZAM LAINGIZA MIL 64/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Azam lililochezwa jana (Oktoba 28 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 64,261,000.
Washabiki waliohudhuria mechi hiyo namba 76 iliyomalizika kwa Azam kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 walikuwa 10,728 ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 9,802,525.42, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,793,490 wakati kila klabu ilipata sh. 14,946,170.45.
Wamiliki wa uwanja walipata sh. 7,599,747.49, gharama za mchezo sh. 4,599,848.61, Bodi ya Ligi sh. 4,599,848.61, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,279,924.31, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,773,274.46.

SIMBA,KAGERA SUGAR KUKUTAANA  LEO ALHAMISI

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaanza raundi ya 12  Leo (Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
Viingilio katika mechi hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kupitia TBC 1 vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A.

Nayo Yanga itashuka uwanjani Novemba Mosi mwaka huu katika mechi nyingine ya ligi hiyo dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.
Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

WANAFUNZI WA UDOM SKULI YA TIBA WAJAFUNGUA CHUO NA HAJUI NILI WATAFUNGUA ?

Nukuu ya kilichoandikwa:
Wanafunzi wa UDom College of Health Sciences, School of Medicine ambao wako clinical years (mwaka wa nne na mwaka wa tano) hawajafungua chuo bado na hawajui ni lini watafungua.

Hata hivyo wanafunzi wanalalamika kua hata upatikanaji wa waalimu imekua ni shida hivyo kufanya mafunzo yao kwa
vitendo kua magumu sana hasa katika miaka  hii miwili ya masomo. Hii inawatia hofu sana wanafunzi ambao wako mwaka wa mwisho ambao wanatazamia kumaliza taaluma yao na kujiunga na internship hasa ukizingatia kwamba internship ni zoezi la kitaifa (halina excuse na ratiba mbovu za chuo).

My take; JK, UDom ikitoa madaktari wabovu ni janga kitaifa, ni hasara kwa Serikari, vilevile ni aibu kwa vyuo vya Serikari, utawala pale central kuna uzembe/matatizo, chukua hatua wanafunzi hawa warudi shuleni kumalizia taaluma zao na suala la waalimu vilevile lipatiwe ufumbuzi!

Nawasilisha!!

---
by maghambo619
via JF: News Alert: Jk unajua kinachoendelea udom skuli ya tiba?

MTOTO ALIYEBAKWA NA BABA YAKE AOMBA ASAIDIWE APATE HAKI YAKE

Mtoto aliyefanyiwa ukatili kwa kubakwa na kulawitiwa na baba yake mzazi huko kijijini Kiria katika kata ya Mamba Kusini wilaya ya Moshi Vijijini ameomba msaada wa wanaharakati, wanasheria na taasisi huska ili apatiwe haki yake.

Mtoto huyo ambaye kwa sasa analelewa na msamaria mwema, amesema kamwe hatakaa asahau mateso aliyoyapata na 
angependa kuona baba yake akipewa hukumu inayostahili kwa maovu alioyoyatenda kiasi cha kusababisha mdogo wake kutoroka na hadi sasa haifahamiki alikotokomea.

Baba mzazi wa mabinti hao wawili aliripotiwa kuwabaka na kuwalawiti binti zake hao wenye umri wa miaka 10 na 13 na kuwajeruhi vibaya.

Wakinamama wa kijiji hicho walipopata taarifa hizo walishikwa na hasira, wakamkamata mtuhumiwa na kumpeleka kwenye Kituo cha Polisi Himo na wakatishia kumtoa uhai endapo polisi watamwachia huru, kwa madai imekuwa ni kawaida yao kila akifikishwa kituoni hapo kuhusiana na unyama anaowafanyia watoto hao huachiwa.

Imedaiwa mzazi huyo alianza kuwatenda wanawe unyama huo baada ya kuachana na mkewe kutokana na ugomvi baina yao na kwa kuwa aliachiwa watoto, ndipo alipoanza kuwatumia wote kwa zamu na kuwatisha kuwa endapo wangesema kokote kuhusu wanavyofanyiwa, angewaua.

Taarifa iliyotolewa na daktari wa Hospitali Teule ya Kilema baada ya kumpima mtoto huyo, ilionyesha kuwa aliharibiwa sehemu zote mbili za kutolea haja na kuota vijinyama ambavyo kwa sasa amepatiwa dawa ya kutumia kwa muda wa siku 14 na endapo havitaisha, atalazimika kufanyiwa upasuaji.

 
Source: /www.wavuti.com.bofya hapa kusikiliza sauti ya habari hiyo

ANGALIA UHALIBIFU ULIFANYWA NA MASHABIKI SOKA WA MBEYA CITY


Picha zilizopachikwa hapo juu   zinaonesha uharibifu ulioripotiwa kufanywa na washabiki wa timu ya soka ya Mbeya City punde tu baada ya kumalizika kwa mchezo baina ya timu hiyo na ile ya Prisons (ya Mbeya pia) wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara, tarehe 29 Oktoba 2013.

Hii si mara ya kwanza kwa washabiki hao kushutumiwa kuhusu uharibifu wa mali na watu wa timu pinzani. Timu hiyo ilipocheza na timu ya Yanga, kulitokea uharibifu vile vile. Ni suala ambalo lisipodhibitiwa litaendelea kudidimiza soka letu.

 Bofya hapa kutizama picha zaidi kwenye blogu ya Malafyale-leo.

S

HII NDIYO RIPORT :YA MAHAKAMA YA RUFAA ILIVYO SIKILIZA MAOMBI YA "BABU SEYA" NA "PAPI KOCHA"

Picture
Nguza Vicking 'Babu Seya' akiwa na mwanawe Johnson Nguza 'Papii Kocha' wakiwa na nyuso za furaha wakati wakitoka katika Mahakama ya Rufaa baada ya majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania kusikiliza maombi yao ya kuitaka mahakama hiyo kupitia hukumu iliyoitoa mwaka 2010. (Picha: Francis Dande)
Wakili Mabere Marando, amedai Mahakama ya Rufani, iliteleza kisheria katika uamuzi wake ambao uliwatia hatiani  na kuwahukumu kifungo cha maisha mwanamuziki Nguza Vikings au 'Babu Seya' na mwanawe Johnson Nguza 'Papii Kocha'.

Marando alidai jana mbele ya jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililotoa hukumu hiyo, likiongozwa na Jaji Natharia Kimaro, kwamba mahakama iliteleza kwa kutozingatia miongozo ya kisheria ya nanma ya kuchukua ushahidi wa 
mtoto, kutoitwa kwa mashahidi muhimu. Mbali na Jaji Nathalia, Majaji wengine ni Mbarouk Mbarouk na Salum Massati.

Wakili huyo, alidai hayo wakati wa kusikilizwa kwa maombi ya mapitio ya hukumu hiyo, iliyotolewa Februari, 2010, Jopo hilo liliwatia hatiani Babu Seya na mwanawe Papii na kuwapa adhabu ya kifungo cha maisha. Jopo hilo liliwaachia huru watoto wengine wa Babu Seya, Nguza Mbangu na Francis Nguza.

Marando alidai mahakama hiyo ilijiridhisha kulikuwa na makosa katika kupokea ushahidi wa watoto na kwa sababu matakwa ya sheria hayakufuatwa hivyo ushahidi huo ulipaswa kufutwa na waleta maombi kuachiwa.

"Mlikubaliana na sisi kwamba Mahakama ya Kisutu ilikosea haikuzingatia uchukuaji wa ushahidi lakini mlisema ilimradi kuwe na ushahidi wa kuunga mkono. Sisi tulisema hapana,"alidai.

Pia, alidai mahakama hiyo, ilikosea katika hukumu yake kwa  kusema  kuna shahidi wa 13 aliyedai kwenye nyumba ya Babu Seya kuna mlango wa siri ambao mtu anaweza kuingia na asionekane, ushahidi ambayo haupo na wala shahidi huyo hakusema hivyo.

“Mashahidi walisema wao waliona katika nyumba ya Babu Seya kuna milango miwili wa mbele na nyuma na yote inainghia sebuleni, mtu huwezi kuingia katika chumba chochote bila kupitia sebuleni... Sasa katika ukurasa wa 38 wa hukumu yenu, mmetamka kwamba shahidi wa 13 aliiambia mahakama kuna mlango fulani wa kuingia katika nyumba bila ya mtu mwingine kukuona. Ushahidi huo haupo katika ushahidi wa shahidi wa 13 hawakusema. Haya ndiyo mambo yanayojidhihirisha kuna kuteleza," alidai Marando.

Aidha, alidai katika ushahidi wa mashahidi wanaohusika na ushahidi uliowatia hatiani Babu Seya na Papii Kocha, walidai walikuwa wakiingia katika nyumba hiyo wakitokea dukani kwa Mangi ambaye alikuwa akijua kinachotokea.

Marando alidai kwa mujibu wa sheria, upande wa Jamhuri ulipaswa kumleta Mangi ambaye ni shahidi muhimu ili aje kuthibitisha, lakini katika hukumu yao walisema upande huo una hiari wa kumuita shahidi wanayemtaka, kauli ambayo ni kinyume cha sheria.

Alidai kuna kijana anaitwa Size ambaye anadaiwa alikuwa anawakusanya watoto wa kike na kuwapeleka kwa Babu Seya na kufanya kinachodaiwa kutendeka, lakini hakuitwa na wala mahakama hiyo katika hukumu haye haimkumzungumzia.

Hoja nyingine, Marando anadai mahakama hiyo, iliteleza kwa kutotoa maoni yake juu ya utetezi wao, kuhusu uwepo wa watu katika nyumba ya Babu Seya, ambao walidai ingekuwa si rahisi watoto kuingia bila ya wao kuwaona kwa kuwa kuna milango miwili ambayo inaingia sebuleni.

"Naomba mpitie tena hukumu yenu na kurekebisha mambo ninayoona yana makosa ya kiuterezi na mkikubaliana nasi mfute washitakiwa kutiwa hatiani na mfute adhabu zao," aliomba Marando.

Upande wa Jamhuri ulikuwa ukiwakilishwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Jackson Bulashi, akishirikiana na Mawakili wa Serikali Waandamizi, Mwangaza Mwipopo, Emmaculata Banzi, Joseph Pande na Wakili wa Serikali Apimaki Mabrouk.

Wakili Bulashi aliiomba mahakama hiyo, kutupilia mbali maombi hayo kwa sababu yalishatolewa uamuzi katika rufani waliyokata waleta maombi. Alidai kwa upande wao wanaona hakuna makosa yaliyofanywa katika kufikia uamuzi huo na kwamba kilichowasilishwa ni sababu za rufani ambazo tayari zilishatolewa uamuzi.

Jopo la Majaji lilisema kuwa limesikia hoja za pande zote na kwamba wataarifiwa tarehe ya kutolewa uamuzi. Awali, jopo hilo lilitupilia mbali maombi ya mapitio yaliyokuwa yamewasilishwa na Babu Seya na Papii Kocha mwenyewe kwa msaada kutoka gerezani, kwa kuwa hawakutumia vifungu sahihi kuyawasilisha.

Na FURAHA OMARY, gazeti la Uhuru — 
Picture
Nguza Vicking na mwanaye Johnson Nguza katika chumba cha Mahakama ya Rufaa Tanzania jijini Dar es Salaam leo, kabla ya kuanza kusikilizwa kwa rufaa ya kesi yao. (Picha: Francis Dande)

 

MWANAMUKIZI wa muziki wa dansi nchini Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanae Johnson Nguza 'Papi Kocha Mtoto wa Mfalme', wameiomba Mahakama ya Rufaa nchini iifanyie upya hukumu yake iliyoitoa Februali mwaka 2010 ambayo iliwahukumu kifungo cha maisha kwasababu hukumu hiyo ina utetelezi wa wazi wa kisheria.

Ombi hilo Na.5/2010 liliwasilishwa kwa niaba yao na wakili wao Mabere Marando jana mbele ya jopo lilelile lilotoa hukumu ya awali ya Februali 2010  ambalo linaongozwa na Jaji Nataria Kimaro, Salum Massati na Mbarouk .S.Mbarouk.

Wakili Marando alidai kwa mujibu wa kanuni ya 66 ya Mahakama ya Rufaa ya mwaka 2009  inatoa mamlaka kwa mahakama ya rufaa kufanya mapitio ya hukumu inazozitoa  hivyo wateja wake wamewasilisha ombi hilo la mapitio kwasababu wanaamini  mahakama yake ilikosea wazi wazi kisheria katika hukumu yake ya Februali 2010 na kwa mujibu wa kanuni hiyo inatoa mamlaka kwa mahakama hiyo kufanya mapitio ya hukumu yake.

Wakili Marando alieleza kuwa ombi lake amelileta chini ya kifungu cha 3 aya A ya Kanuni ya Mahakama ya Rufaa ya mwaka 2009 ,   ikisomwa pamoja na Ibara 13 (3) (6)(a) ya Katiba ya nchi, litaja  moja ya utelezi wa wazi wazi wa kisheria uliofanywa na mahakama hiyo, ni kwamba katika hukumu hiyo  kuna baadhi ya aya inasomeka kuwa majaji hao walikubaliana na hoja yake iliyodai kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakati inasikiliza kesi hiyo, ilikosoea kufuata utaratibu wa kurekodi ushahidi wa watoto waliokuja kutoa ushahidi katika kesi hiyo na kwamba mahakama ya rufaa ikasema licha ya taratibu za kurekodi ushahidi wa watoto kukiukwa, mahakama yake iliona kuna ushahidi unaounga mkono na kwamba mahakama ya rufaa ilitumia ushahidi wa kuunga mkono ndiyo walioutumia kuwatia hatiani waomba rufaa kwa adhabu ya kifungo cha maisha.

“Waheshimiwa majaji kwasababu jopo lenu katika hukumu yake lilikiri wazi wazi  kuwa mahakama ya kisutu ilikosoea kurekodi ushahidi wa watoto wa dogo ambao walidai walitendewa vibaya na waomba rufaa(Nguza na Papii), na sheria za nchi zipo wazi kabisa zina sema endapo mahakama itabaini kuwa mahakama ya chini ilikiuka taratibu za kurekodi ushahidi wa watoto wa dogo, basi ushahidi ule wa watoto wa dogo uliotumika katika mahakama ya chini kuwatia hatiani washitakiwa, ushahidi huo wa watoto unafutwa na waomba rufaa au washitakiwa wanaachiriwa na pia maamuzi ya kesi mbalimbali yaliyokwisha kutolewa na mahakama hii;

“Nafahamu ni kazi ngumu sana  kuwashawishi nyie majaji kubadili uamuzi wenu mlioutoa katika hukumu ya Februali 2010 ambapo mliwatia hatiani wateja wangu, ila kwa uterezi huo wa kisheria niliouanisha unaonyesha katika hukumu yenu mlikubaliana na hoja yangu kuwa Mahakama ya Kisutu ilikosea kurekodi ushahidi watoto wadogo ,naamini mtatumia busara zenu na kufuata sheria inayosema wazi wazi kuwa endapo utaratibu wa kurekodi ushahidi wa mtoto utakiukwa basi ushahidi huo utafutwa na wateja wangu wataachiliwa huru, basi leo naiomba mahakama hii iwaachirie huru wateja wangu’ alidai Marando.

Kwa upande wao mawakili wa upande wa mjibu maombi (DPP),Angaza Mwipopo,Jackson Mlati, Imaculata Banzi na Joseph Pande waliomba mahakama hiyo itupilie mbali ombi hilo kwasababu sababu zote alizozitoa jana ni sababu ambazo alizitoa wakati wa usikilizwaji wa rufaa na ziliamliwa katika hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo Februali mwaka 2010.

Jackson alidai kama Marando anaona hukumu ya mwaka 2010 ilikuwa na dosari , basi angeomba mahakama hiyo impangie jopo la majaji watano wa kusikiliza ombi na siyo ombi lake kuja kusikilizwa na jopo la maji watatu wale wale waliotoa hukumu ile ambayo Marando anadai ina dosari.

“Hoja za Marando ni za kirufaa, na hoja zake zote anazotaka kuonyesha hukumu ya mahakama hii ina dosari zilishaamriwa na mahakama hii wakati ikisiliza rufaa ya wateja wake mwaka 2010 na tunamtaka Marando aelewe kuwa hakuna maamuzi yasiyonamwisho hivyo sisi tunaomba ombi la Marando linalotaka mahakama hii ifanyiwe mapitio hukumu yake halina msingi”alidai wakili  Jackson.

Aidha Jaji Kimaro alisema amesikiliza hoja za pande zote mbili akaamuru waomba rufaa warejeshwe gerezani na kwamba mahakama itatoa tarehe ya kutoa uamuzi wake kuhusu maombi hayo kwa pande zote mbili.

Aliyekuwa Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Addy Lyamuya, aliyekuwa jaji wa Mahakama Kuu Thomas Mihayo na jopo hilo la majaji wa tatu linaloundwa na Jaji Kimaro ,Massati na Mbarouk liliwatia hatiani kwa makosa ya kuwabaka watoto wadogo na likawahukumu kifungo cha maisha gerezani na hadi sasa wameishakaa gerezani kwa miaka kumi.

Mahakama ya Rufaa, Februali mwaka 2010 ,ilirekebisha hukumu ya Mahakama Kuu na Mahakama ya Kisutu ambapo iliwaachiria huru waomba rufaa wawili katika kesi hiyo  ambao ni watoto wa Nguza Vicking, Nguza Mbangu na Francis Nguza waliachiwa huru, huku Viking na Papi Kocha wakiendelea kutumikia kifungo chao hadi sasa.

Hata hivyo jana mahakama hiyo ilifurika wanamuziki, mashabiki, ndugu wa washitakiwa na wengine walilazimika kukaa sakafuni ambao walikuja kusikiliza kesi hiyo. 
Na HPPINESS KATABAZI, Tanzania Daima
 
 Taarifa mbili zimepachikwa hapo chini kwa uchambuzi wako, kutoka magazeti ya UHURU na TANZANIA DAIMA

 

RAIA WA CONGO DRC WAKIMBILIA NCHINI UGANDA

 


Wakimbizi wa DRC wengi wana kimbilia usalama wao nchini Uganda
Melfu ya wakimbizi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo, wameingia nchini Uganda, huku majeshi ya serikali ya DRC yakipambana vikali na waasi wa M23.
Makabiliano makali kati ya pande hizo mbili yamepamba moto huku kukiripotiwa kutokea mashambulizi ya maombora karibu na mji wa Bunagana ulio kati ya mpaka wa DRC na Uganda.
Msemaji wa shirika la kuwahudumia wakimbizi la UNHCR, alisema kuwa wakimbizi elfu mbili wamevuka na kuingia Uganda hii leo na kuifikisha idadi ya wakimbizi hao hadi elfu tano.
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa mapema wiki hii alisema kuwa kundi la waasi la M23 lsio tisho tena la kijeshi kufuatia ushindi kadhaa wa jeshi dhidi ya waasi hao ambapo waliweza kuthibiti miji iliyokuwa imetekwa na waasi hao.

Aliongeza kuwa waasi hao wametoeroka maeneo ya Bunagana na kwamba sasa wako katika kipnade kidogo cha ardhi karibu na mpaka wa Rwanda.

Wanajeshi wa DRC wakisaidiwa na jeshi la Umoja wa Mataifa( MONUSCO) walifanikiwa kudhibiti kambi ya kijeshi ya Rumangabo siku ya Jumatatu

Chanzo :bbc swahili

 

TANZANIA YASEMA INAWEZA KUJITOA KATIKA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI



Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete

Serikali ya Tanzania imesema inatafakari ushiriki wake ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na inaweza kujitoa ndani ya Jumuiya hiyo iwapo itaendelea kutengwa katika baadhi ya vikao.
Aidha imesema Tanzania haitambui vikao vinavyofanywa na nchi tatu zilizopo ndani ya Jumuiya hiyo ambazo zimekuwa zikizitenga Tanzania na Burundi.
Katika mikutano iliyofanyika hivi karibuni Tanzania na Burundi hazikualikwa kwenye vikao hivyo.
Kwa mujibu wa Waziri Sitta mikutano ya wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambayo ilianza kwa kuitenga Tanzania ilifanyika Entebbe nchini Uganda mwezi Juni mwaka huu na kufuatiwa na mkutano wa pili uliofanyika Agosti mwaka huu huko Mombasa nchini Kenya ambapo nchi hizo tatu bila kuishirikisha Tanzania walizungumzia uanzishaji wa himaya moja ya forodha.
Mambo mengine waliyozungumza wakuu hao ilikuwa uanzishaji wa visa moja ya utalii kwa nchi zao na matumizi ya vitambulisho vya uraia ambavyo vitatumika kama hati za kusafiria miongoni mwa nchi hizo.

Aidha Waziri Sitta amesema ndani ya mikutano hiyo pia walizungumzia kuanzisha mchakato wa kuanzisha shirikisho la nchi hizo.

Tayari Tanzania imeanza mazungumzo na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kuangalia ni kwa namna gani zitaanzisha ushirikiano nje ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama zinavyofanya nchi za Rwanda, Uganda na Kenya.

CHANZO:    bbc swahili.com

POLE SANA JUMA KASEJA KWA MAJANGA.


Aliyekuwa Kipa Namba moja na Nahodha wa Kikosi cha Taifa Stars Juma Kaseja amepata majanga mengine baada ya Kuachwa na Taifa Stars baada ya Kocha
Kim Poulsen kutangaza Kikosi cha Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars)huku Juma Kaseja akiwa hayupo katika Orodha ya Taifa Stars . 

Ikumbukwe kuwa Kaseja baada ya kumaliza mkataba wake na Simba Msimu wa Ligi uliopita hakupata tena nafasi baada ya wekundu wa Msimbazi kumtema,lakini naadaye ilianza mipango ya kumtafutia Timu Nje ya Nchi lakini nayo haikuweza kuzaa matunda kutokana na zengwe za hapa na pale.

WASANII WA BONGO MOVIE WAPONDWA KUJIPODOA MISIBANI

Msanii katika Kiwanda cha Filamu Nchini Tanzania Baturi amefunguka na kutoa ya moyoni kwa Wasanii na Raia wengine ambao kazi yao ni kujiremba na
kujipodoa Pindi waendapo katika Misaba,kwani amefananisha hali hiyo ni sawa na Kwenda kuuza Sura wakati wenzako wapo katika Kipindi Kigumu.

HII NDIO ADHABU WALIOPEWA WANAJESHI WALIO IBA VITU WESTGATE WAKATI WANAPAMBANA NA MAGAIDI.

Wanajeshi wawili nchini Kenya wamefutwa kazi na kufungwa jela kwa kitendo cha kupora mali wakati wa shambulizi la kigaidi kwenye Jengo la Westgate mwezi jana.  Hayo yamesemwa na mkuu wa jeshi la Kenya, Julius Karangi.


Karangi amesema kuwa mwanajeshi wa tatu aliyeshukiwa kwa uporaji anachunguzwa.

Awali Karangi alikanusha kuwa wanajeshi walifanya uporaji kwenye jengo hilo licha ya picha za CCT kuonyesha wanajeshi wakibeba mifuko ya plastiki kutoka kwenye moja ya maduka makubwa yaliyokuwa ndani ya Jengo la Westgate.

Hivi karibuni wanamgambo wa Somalia, al-Shabaab walikiri kufanya shambulizi hilo na kuwateka  nyara Wakenya kadhaa waliokuwa ndani ya jengo hilo kwa siku nne.

Watu 67 walifariki na mamia ya wengine kujeruhiwa.

Wakati huohuo, mkuu wa kitengo cha uchunguzi wa uhalifu katika idara ya polisi,Ndegwa Muhoro alisema kuwa mmoja wa magaidi waliokuwa ndani ya jengo hilo walipiga simu nchini Norway wakati walipovamia jengo hilo.

Mmoja wa washukiwa wa shambulizi hilo ametajwa kuwa Hassan Abdi Dhuhulow mzaliwa wa Somalia ambaye ana uraia wa Norway.

Jeshi limesema kuwa magaidi wote wanne waliofanya shambulizi hilo waliuawa.

MWANAFUNZI ALIYE BAKWA NA KUPATA MIMBA AOMBA KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE


Vitendo vya ubakaji vimeendelea kuumiza akili za wapigania haki na ustawi wa wanawake nchini Tanzania kwa muda mrefu sasa. Miongoni mwa kesi hizi zimehusisha wasichana wadogo wenye malengo makubwa katika maisha yao, lakini kutokana na mfumo uliopo, jamii hushindwa kutoa msaada kwa wahanga wa matukio hayo ili wafanikishe malengo yao.

Emma Roberts ni binti mwanafunzi aliyekumbwa na mkasa wa kufukuzwa shule kutokana na ujauzito alioupata baada ya
 

 CHANZO WAVUTI BLOG

MTUHUMIWA SUGU AKAMATWA NA SIRAHA ZA KIVITA 45 ZA KIENYEJI 17 NA RISASI 892

 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Salum Msangi amesema operesheni maalumu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu ya kukabiliana na vitendo vya ujambazi, ujangili wa uwindaji haramu pamoja na wahamiaji haramu imefanikisha kukamatwa kwa silaha 45, zikiwemo za kivita na 17 za kienyeji, risasi 892 na magazine 24 pamoja na watuhumiwa sugu wa ujambazi.

Kamanda Msangi amesema miongoni mwa silaha zilikamatwa ni G3 moja ikiwa na risasi zake 35 iliyokuwa ikitumiwa na mwanamke mmoja aliyetambulishwa kwa majina,Hollo Mabuga (28) mkazi wa wilayani Bariadi.

“Tumeweza pia kumkamata mtuhumiwa hatari wa matukio ya uhalifu ambaye hivi karibuni aliachiwa kutoka Gerezani lakini tukapata taarifa za raia wema kuwa amekuwa akijihusisha na ujangiri na ujambazi ambaye ni Masanja Sumuni, tukaweka mtego na kufanikiwa kumkamata akiwa na SMG moja na risasi 96....” Bofya haa kumalizia habari hii kwenye GSengo blog

 

Tuesday 29 October 2013

WAKI DADA WAPIGANA BARABANI WAKI GOMBANIA BWANA


Angalia picha hii wakidada  wazichapa kavkavu barabarani kwa kisa cha mwanaume chezea mapenzee wewe hatari
Wadada wawili Warembo wa Mitaa ya kawe waliamua kuzichapa kavu kavu bila maglovsi mbele za watu kwa
eti mmoja akimtuhumu mwenzie kuwa anatoka na Boyfriend wake...Inasemekana hawa madada ni marafiki sana lakini leo yamewashinda baada ya kuchangia bwana mmoja

MGANGA AKUTWA NA KIGANJA CHA BINADAMU AKIMUUZIA MTEJA WAKE

KWA MILIONI 100 JIJINI MWANZA MAJANGA YA  MWAKA

Mtu mmoja jijini Mwanza anadaiwa kukamatwa na kiganja cha mtu akiwa anajiandaa kumuuzia mteja kwa sh million 100.


Washukiwa walikamatwa  jana  karibia na uwanja wa ndege wa Mwanza  wakifanya  biashara  hiyo  haramu.... 

 Baada  ya  upekuzi  wa  kina, mteja  alikuwa  ana  milioni  100  na mganga alikutwa  na   kiganja cha  binadamu  ambacho kilikuwa  kibichi kikitoa damu.

Kiganja  hicho  kilikuwa  kimevishwa  tunguri  na nywele za binadamu.


source:Udakuspecially.

REAL MADRID YAMTAKA SEPP BLATTER AOMBE RADHI KAULI YAKE JUU YA RONALDO


>>YAMSHAMBULIA KWA KUMVUNJIA HESHIMA RONALDO!!
sepp_blatterKOCHA wa Real Madrid Carlo Ancelotti ameyaelezea matamshi ya Rais wa FIFA Sepp Blatter kuwa ni ya kuonyesha kutomheshimu Mchezaji wao Cristiano Ronaldo na pia alitoboa kuwa Klabu yao imemtaka Blatter afute kauli yake.
Real wamechukizwa na Blatter ambae, wakati akijibu swali alipotakiwa kuwafananisha Lionel Messi wa Barcelona na Ronaldo huko Chuo Kikuu cha Oxford Nchini England Wiki iliyopita, alitoa majibu wanayotuhumu ni ya dharau na kumvunjia hadhi Ronaldo.

Blatter alisema Wachezaji wote hao ni wenye vipaji lakini akamuelezea Messi kuwa ni Kijana mzuri na kumsema Ronaldo kuwa ‘anatumia gharama nyingi kwa Watengeneza Nywele.’

Leo, akihojiwa kabla ya Mechi ya Real na Sevilla itakayochezwa Jumatano, Kocha Carlo Ancelotti alisema: “Nafahamu kuwa Rais wetu, Florentino Pérez, amepeleka Barua FIFA akitaka matamshi hayo yafutwe na kwangu ni matamshi ambayo yamemvunjia heshima Mchezaji makini sana kwenye fani yake ya Soka la Kulipwa!”
Aliongeza: “Nakubaliana na Rais wetu. Sijaongea na Cristiano. Yeye amefanya mazoezi vizuri, kama ilivyo Siku zote. Kila Siku anaonyesha yeye ni Mchezaji bora, makini na anaejali kazi yake, mwenye heshima kwa kila Mtu na ataendelea hivyo.”

Alipoulizwa kuhusu Messi na Ronaldo huko Oxford, Blatter alijibu: “Wote ni Wachezaji wazuri lakini wako tofauti kabisa na Soka ni kuhusu staili tofauti na Messi ni Kijana mzuri ambae kila Mama na Baba angependa kuwa nae nyumbani. Ni Mtu mzuri, ni mwenye kasi sana, hajikwezi, anacheza vizuri, anadundika, Mtu mwema, Kijana mzuri. Na hayo yanamfanya apendwe na ni wazi atafunga Mabao mengi kwa vile ni Kijana mzuri na anacheza vizuri na anafunga.”

Kisha Blatter akaonekana akimzungumzia Ronaldo pale aliposema: “Yule mwingine, ni kitu tofauti. Huyu mwingine yuko kama Kamanda kwenye Kiwanja cha kuchezea…..Hiyo ni upande mwingine wa Soka na ni vizuri kuwa na Makamanda Uwanjani. Kwa sababu huna aina moja ya mwelekeo hilo huleta uhai kwenye Soka na huyu anazo gharama kubwa kwa Mtengeneza Nywele kupita mwenzake lakini hilo halijalishi.”

Blatter akamalizia: “Kwa hiyo siwezi kusema nani bora. Listi ya Ballon d'Or itachapishwa Jumanne na Umma utaamua nani bora. Nawapenda wote, lakini nampendelea Messi!”

YANGA, MBEYA CITY ZA SHINDA MECHI ZA LEO ZAZISHUSHA SIMBA CHINI NAFASI YA 4!

  Tuesday, 29 October 2013 19:00

MATOKEO:
Jumanne Oktoba 29
Tanzania Prisons 0 Mbeya City 2
Yanga 3 Mgambo Shooting 0
Rhino Rangers 1 JKT Ruvu 0

VPL_2013-14_LOGO-NEWUSHINDI kwa Mabingwa Watetezi Yanga na Mbeya City katika Mechi zao za leo umeishusha Simba hadi Nafasi ya 4 huku Mbeya City wakikamata Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 23 sawa na Vinara Azam FC na Yanga wakishika Nafasi ya Tatu wakiwa na Pointi 22 na Simba kuwa Nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 20.
Timu zote hizo zimecheza Mechi 11 kila mmoja.
Huko Mjini Mbeya, ambako Timu za Mji huo zilipambana, Mbeya City iliichapa Tanzania Prisons Bao 2-0.

Jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa, Mabingwa Yanga waliibamiza Mgambo Shooting Bao 3-0.

Hadi Mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 31 la Mbuyu Twite.
Kipindi cha Pili, katika Dakika ya 50, Hamis Kiiza alifunga Bao la pili kwa Penati kufuatia Kipa wa Mgambo kumchezea faulo Didier Kavumbagu.
Bao la Tatu lilifungwa Dakika ya 67 na Didier Kavumbagu.
 
RATIBA:

Alhamisi Oktoba 31
Simba vs Kagera Sugar

Ijumaa Novemba 1
JKT Ruvu vs Yanga

Jumamosi Novemba 2
Mgambo Shooting vs Coastal Union
Tanzania Prisons vs Oljoro JKT
Azam vs Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar vs Rhino Rangers

Jumapili Novemba 3
Mbeya City vs Ashanti United

Jumatano Novemba 6
JKT Ruvu vs Coastal Union
Ashanti United vs Simba
Kagera Sugar vs Mgambo Shooting
Rhino Rangers vs Tanzania Prisons
Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar

Alhamisi Novemba 7
Azam vs Mbeya City
Yanga v JKT Oljoro

MSIMAMO:
NA TIMU P W D L GD GF PTS
1 Azam FC 11 5 5 0 10 17 23
2 Mbeya City 11 6 5 0 8 15 23
3 Yanga SC 11 6 4 1 13 24 22
4 Simba SC 11 5 5 1 11 21 20
5 Mtibwa Sugar 11 4 4 3 1 16 16
6 Ruvu Shooting 11 4 4 3 3 13 16
7 Kagera Sugar 11 4 4 3 3 12 15
8 JKT Ruvu 11 4 0 7 -1 9 12
9 Coastal Union 11 3 6 2 4 10 15
10 Rhino Rangers 11 2 4 5 -6 9 10
11 Ashanti UTD 11 2 4 5 -9 10 10
12 Prisons FC 11 1 5 5 -9 6 8
13 JKT Oljoro 11 1 4 6 -8 8 7
14 Mgambo Shooting 11 1 2 8 -18 3 5


MATOKEO:
Jumatatu Oktoba 28
Simba 1 Azam FC 2
Coastal Union 3 Mtibwa Sugar 0
Oljoro JKT 0 Ashanti United 0
Ruvu Shooting 1 Kagera Sugar 1

L ANGALIA JINSI LADY GAGA ALIVYO TUMBUIZA AKIWA UCHI WA MNYAMA MBELE ZA WATU.


Lady Gaga anasifika kwa vituko vya mara kwa mara vinavyomfanya awe controversial sana, and this time around ameamua kufanya onesho akiwa uchi wa mnyama!..ndio nimesema uchi wa mnyama katika show ya G-A-Y huko London, Uingereza Ijumaa iliyopita.


Gaga (27) alipanda jukwaani akiwa amevalia vazi linalomfunika hadi miguu lakini wakati akiendelea kuperform ghafla akaanza kusaula taratibu kutokea juu hatimaye kulishusha vazi lote na kubaki mtupu.



RAY C ,AMTWANGA DADA NORA WA BONGO MOVIE

 

Na Musa Mateja
KATIKA hali ya kushangaza, siku chache baada ya kuripotiwa kupona na kuacha matumizi ya madawa ya kulevya, mwanamuziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ anadaiwa kugeuka mwanamasumbwi na kumpa kipigo mwigizaji Nuru Nassoro ‘Nora’, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa.