MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Tuesday 3 May 2016

IGP Mangu: Sina Taarifa Juu ya Agizo la Rais Kumpandisha Cheo Askari

 
Amesema hajapewa taarifa za Rais Magufuli kuagiza koplo Deogratius Mbango kupandishwa cheo baada ya kumdhibiti mke wa mmoja wa mawaziri wa serikali yake kwa kosa la kukiuka sheria za usalama barabarani.

" Bado hajapandishwa cheo kwa sababu sijapewa taarifa hizo na nitakapopewa taarifa atalazimika kwenda kwenye mafunzo kwanza, sisi jeshi la polisi tuna taratibu zetu" alisema IGP Mangu .

Chanzo: Nipashe

Urusi Sasa kujikita Tanzania, yapanga Kujenga Mtambo wa Nyuklia Tanzania

  
Makampuni makubwa ya Viwanda na uzalishaji ya Kirusi ya "Russian Helicopters", "United Aircraft Corporation (UAC)" na "United Wagon Company (UWC)" yako tayari kuwekeza kwenye miradi ya viwanda nchini Tanzania.

Waziri wa viwanda wa Urusi amesema Urusi iko tayari kujenga nuclear reactor nchini Tanzania kwa ajili ya tafiti na kwa ajili ya mambo ya afya.

Huu ni mpango wa Urusi kufufua uhusiano wake na nchi za Afrika kwa upya tangu miaka ya 90 kwa kupitia mshirika wake wa zamani, Tanzania.

Uchumi wa Tanzania Waongoza Afrika Mashariki Ukifuatiwa na Kenya



Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.

Katika ripoti yake iliyotolewa jana Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka  2016.

Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
 
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.

IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.

Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15.
 
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola. Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.

Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.

Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
 
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
  1.     Ivory Coast 8.5%
  2.     Tanzania 6.9%
  3.     Senegal 6.6%
  4.     Kenya 6%
  5.     Zambia 3.4%
  6.     Nigeria 2.3%
  7.     Afrika Kusini 0.6%

Mawaziri Waja juu Jeshi kuhusishwa na Siasa

 

MAWAZIRI wa Serikali ya Awamu ya Tano wamewajia juu wabunge wa upinzani na wananchi wanaovishutumu kila mara vyombo vya ulinzi nchini na kuwataka kuacha kuvihusisha vyombo hivyo na masuala ya kisiasa.

Mawaziri hao ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yussuf Masauni na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba.

Wamewataka wananchi na hususani wabunge wa vyama vya upinzani, kutambua kuwa vyombo hivyo vya ulinzi ambavyo ni pamoja na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Polisi wajibu wake mkubwa ni kulinda mipaka ya nchi na usalama wa raia na mali zao.

Akizungumza wakati wa mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara inayoshughulikia Muungano na Mazingira, Dk Mwinyi alisema haijawahi kutokea na wala haitotokea jeshi kutumika kisiasa.

Alisema Jeshi la Tanzania limekuwa likitekeleza majukumu yake kwa kufuata sheria iliyojiwekea pamoja na za kimataifa na wala hata siku moja haliwezi kutumika kwa ajili ya kutumiza malengo ya kundi fulani.

“Jeshi letu lina sifa ya kimataifa ya ulinzi wa amani, dunia kote tunasifika kwa weledi, kulinda amani na mipaka yetu. Haijawahi kutokea wala haitotokea jeshi kujiingiza kwenye shughuli za kisiasa,” alisisitiza Dk Mwinyi.

Alisema tangu mjadala wa makadirio ya bajeti hiyo uanze, baadhi ya wabunge hususani wabunge wa upinzani wamekuwa wakilitupia shutuma nzito jeshi na vyombo vya dola kwa ujumla kuwa limetumika vibaya kwenye uchaguzi wa Zanzibar na chaguzi nyingine.

Aliwataka wabunge hao pamoja na wananchi wanaovilaumu mara kwa mara vyombo hivyo vya dola kumuogopa Mungu kwa kutoa madai ya uongo dhidi ya vyombo vyao vya ulinzi na usalama.

Alisema madai kuwa jeshi hilo limetumika na kuandikisha wananchi kwenye kambi zao za jeshi visiwani Zanzibar si ya kweli na kama kuna mwenye ushahidi auwasilishe ili ukweli ujulikane.

Dk Mwinyi alisema amesikitishwa na madai ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu masuala ya Muungano, Ally Abdallah Saleh kwamba Zanzibar imetekwa na jeshi la Tanganyika kana kwamba nchi iko katika vita.

“Naomba nikujibu kwanza ili ufahamu kuwa hakuna jeshi la Tanganyika, jeshi ni moja na ni la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania. Naomba nimuelimishe kazi kubwa za jeshi ni ulinzi wa mipaka, ulinzi wa amani na kutoa msaada kwa mamlaka za kiraia au vyombo vingine vya ulinzi na usalama inapohitajika kufanya hivyo,” alisema.

Alisema inapotokea matukio makubwa kama shughuli ya uchaguzi, duniani kote si Tanzania pekee, majeshi yote yanakuwa tayari kukabiliana na hali yoyote na ndio maana askari wake wanakuwa kwenye sare za kombati.

Kuhusu madai ya kambi hiyo ya upinzani kuwa Jeshi limekuwa likitumika kulazimisha Muungano, Dk Mwinyi alisema JWTZ ni kielelezo cha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alisema tangu Tanganyika na Zanzibar ziungane mwaka 1964, jeshi ni moja na kamwe halijawahi kulazimisha utawala, ila lipo hadi Zanzibar kwa sababu ya kulinda mipaka ya Tanzania, na Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.

“Tangu mwaka 1964 jeshi lina vikosi vyake Zanzibar na siku zote vikosi hivi huwa na silaha, sasa tuna haja gani ya kupeleka wanajeshi na silaha wakati miaka yote vyote viko huko? "Alihoji Dk Mwinyi. 

Naye Naibu Waziri Masauni alisema hoja kwamba jeshi lilitumia mabavu Zanzibar na askari walikuwa ni wengi si ya kweli.

Alisema kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, kila kituo cha uchaguzi kinahitajika angalau askari wawili wakati Zanzibar kulikuwa na vituo vya uchaguzi zaidi ya 3,000 na askari waliopo visiwani humo ni 5,000.

Alisema kwa hali ilivyokuwa askari wa Zanzibar walikuwa hawatoshi kwani wangesambazwa wote wasingetosha kuweka ulinzi na kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa utulivu na usalama.

Kuhusu madai kwamba Katiba imekiukwa, aliutaka upande wa upinzani kujiuliza kati ya madai yao ya kumtaka Rais John Magufuli aingilie mamlaka ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) au Polisi kulinda raia na mali zao, kipi ni uvunjifu wa Katiba.

Alifafanua kuwa majukumu ya Jeshi la Polisi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ni kulinda usalama wa raia na mali zao hivyo bila kujali cheo au utajiri wa mtu yeyote endapo atavunja sheria atachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju alisema uchaguzi wa Zanzibar ulikamilika kwa usalama na kwamba pamoja na malalamiko ya vichochoroni kuhusu uchaguzi huo, hakuna hata mmoja aliyefungua kesi kupinga matokeo mahakamani.

Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi ni ruhusa mtu asiporidhika na matokeo ya uchaguzi, kufungua kesi ya kuyapinga, lakini tangu uchaguzi huo umalizike hakuna mtu kutoka jimbo lolote visiwani humo aliyefungua kesi.

Naye January alisema kuhusu uchaguzi wa Zanzibar, Mahakama Kuu ya Zanzibar ndio pekee yenye uwezo wa kusikiliza na kuamua masuala yote yanayohusu uchaguzi wa Zanzibar.

Polisi wawili watuhumiwa kuomba rushwa milioni 7.2/

POLISI mkoani Rukwa inawashikilia askari wake wawili wa Kituo Kikuu cha Polisi wilayani Nkasi, wakituhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya zaidi ya Sh milioni 7.2 wamsaidie mtuhumiwa.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Rukwa, Leonce Rwegasira alitaja askari hao kuwa ni Konstebo Filbert Ruhemeja na Konstebo Bahati Sengerema, ambao walikuwa wakifanya kazi katika Kituo cha Polisi mjini Namanyere wilayani Nkasi.

Alisema polisi inawafanyia uchunguzi wa kina askari wake wawili, wanaotuhumiwa kwa kashfa ya kuomba rushwa ya Sh milioni 7.2 na iwapo watabainika halitasita kuwatimua na kuwafikisha mahakamani.

Rwegasira alisema hayo jana ofisini kwake wakati anazungumza na mwandishi wetu alipotaka kujua ni hatua gani zilizochukuliwa dhidi ya polisi hao kutokana na kuwepo kwa tuhuma hizo za kuomba na kupokea rushwa.

Alisema askari hao wawili wa polisi, wanatuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya fedha kutoka kwa mtu mmoja  ili wamsaidie katika shitaka linalomkabili.

Monday 2 May 2016

Mamlaka ya Bandari-TPA Yataja Sababu Iliyosababisha Mizigo Bandarini Dar es Salaam Kupungua

Siku moja baada ya serikali  kuziagiza mamlaka ya Bandari-TPA, na Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, kufanya uchambuzi wa kina ili kubaini sababu za kupungua kwa shehena ya kontena zinazoingia nchini kupitia Bandari ya Dar es salaam kwenda nchi jirani, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Injinia Alois Matei, leo amejitokeza mbele ya waandishi wa habari  ili kutaja chanzo cha mizigo kupungua bandarini.

Agizo la kuzitaka mamlaka ya Bandari-TPA, na Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, kufanya uchambuzi  huo lilitolewa juzi Bungeni   April 30 na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dr. Philip Mpango .

Dr  Mpango alisema katika kipindi cha mwezi Oktoba mwaka jana na Machi mwaka huu kontena zilizopelekwa nchini Congo zilishuka kutoka 5,529 hadi 4,092, wakati yale yaliyokuwa yakipelekwa nchini Malawi yalishuka kutoka kontena 337 hadi 265, huku yale ya Zambia yakishuka kutoka 6,859 hadi kufikia 4,448, hivyo akaziagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania-TPA na Mamlaka ya Mapato-TRA, zichambue mwenendo huo ili kubaini chanzo cha kupungua.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Injinia Alois Matei amesema sababu kubwa  ya kupungua kwa makontena hayo imesababishwa  na kuyumba kwa  uchumi wa dunia  hasa China na kwingineko ambako mizigo inayopitia bandari ya Dar es Saam hutoka.

“Biashara za bandari dunia nzima zimeshuka.Kipindi hiki kuna mtikisiko kidogo kutokana na uchumi wa dunia kuyumba hasa China na kwingineko.

"Juzi tuliongea na wenzetu wa Singapore ambao walikuja hapa nchini, nchi yao ni moja ya nchi inayofanya biashara ya bandari kwa kiasi kikubwa. Wao pia walisema wamekumbana na tatizo hilo la kushuka kwa mizigo katika kipindi cha hii miezi mitatu." Amesema Matei

Katika hatua nyingine, Injinia  Matei  amesema serikali imepanga kutumia dola milioni 690 kuimarisha miundombinu ya Bandari ya Dar es Salaam ili kuongeza uwezo wa kupokea mizigo hadi kufikia tani milioni 38 ifikapo 2030 kutoka tani milioni 16 za mwaka 2014/15.

Akifafanua kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Matei amesema mradi huo unatekelezwa kwa kushirikiana na Benki ya Dunia,Trade Mark East Africa na DFID  na unatarajia kuanza   kabla ya mwisho wa mwaka 2016.

“Serikali,Benki ya Dunia,Trade Mark East Africa na DFID zimetiliana saini makubaliano ya ushirikiano wa utekelezaji wa mradi wa maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam” alisisitiza Matei.

Akizungumazia maeneo yatakayohusika katika maboresho hayo Injinia Matei amesema kuwa yatahusisha uboreshaji na uongezaji wa kina kufikia mita 14 katika gati namba 1 hadi 7 ili kuwezesha meli kubwa zaidi kutia nanga.

Maeneo mengine ni ujenzi wa gati mpya ya kushushia magari katika eneo la Gerezani Creek, uchimbaji ili kuongeza kina cha lango la kuingilia meli hadi kufikia mita 14 pamoja na sehemu ya kugeuzia meli.

Eneo jingine  ni uhamishaji wa gati la mafuta la Koj pamoja na bomba la mafuta katika eneo la ujenzi, uboreshaji wa mtandao wa reli ndani ya bandari na ujenzi wa sehemu ya kupakilia na kushushia mizigo.
Mhandisi Mkuu  wa TPA Bi Mary Mhayaya akitoa ufafanuzi kuhusu mradi wa Flow meter mpya ya Kigamboni ambao umeshakamilika na hivyo kuwezesha mafuta yote yanayoingia  nchini kupitia Bandari ya Dar es Salaam kupimwa na kujulikana kiasi halisi kilichoingizwa hapa nchini ili kuiwezesha Serikali kupata mapato stahiki ikiwemo kodi
 

Masoud Kipanya Aitaja Sababu iliyomrudisha Clouds FM


Masoud Kipanya amerejea tena Clouds FM baada ya miaka minane kuondoka. Mchoraji huyo maarufu wa katuni ya Kipanya, anasikika kwenye kipindi cha Power Breakfast.
“Sijui kama unajua kuwa mimi Clouds nilifukuzagwa kazi! Msingi wa kutoka Clouds ni kwamba sikutoka kwasababu nilikuwa labda niko hivi hapana, tulikuwa tunafanya kazi zetu kama kawaida baadaye kuna mambo yaliyotokea tukaonekana [Yeye na Fina Mango] ni watovu wa nidhamu tukafukuzwa,” alisema Masoud kwenye kipindi cha Danga Chee cha Channel Ten.
“Kwahiyo I was fired, nilifukuzwa kazi. Sasa miaka minane baadaye watu hao hao wakikuapproach kufanya nao kazi kwa terms ambazo mnakaa chini sasa kama watu wazima, watu ambao wanaona kabisa kwamba miaka minane umekaa bila wao na ya kwako yanakuendea. Kwanza hapo kuna heshima kubwa sana, katika hali ya kawaida nilitakiwa niwe nimeshadondoka, sipo, sifai, siwezekani tena. Lakini kama watu wamekuona kwamba unahitajika kwenye ile sehemu ni kipimo kingine cha kuonesha kwamba ‘okay kumbe kitendo cha kubaki kwenye media kama mchoraji katuni thamani iko pale,” aliongeza.

“Lakini namba mbili ni kwamba ninapofuatwa nirudi Clouds, tumekaa mezani tumezungumzia masuala ya mkwanja wa kutosha, wakati huo huo project zangu zote hakuna hata moja inayovunjika, kuna tatizo gani mimi kutengeneza extra money katika masaa matatu au masaa manne?”

Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein Aapishwa Rasmi Kuwa Mjumbe wa Baraza la Mawaziri

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein leo asubuhi tarehe 02 Mei, 2016 ameapishwa kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri ili aweze kushiriki na kutekeleza majukumu yake ndani ya Baraza hilo.

Rais Shein ameapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mohamed Chande Othman katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma, tukio ambalo limeshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Viongozi wengine walioshuhudia tukio hilo ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo mchana ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Baraza la Mawaziri, uliopo Ofisi ya Rais TAMISEMI Mjini Dodoma.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
02 Mei, 2016

Mahakama ya Kisutu Yatoa Hati ya Kukamatwa kwa Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar imetoa hati ya kukamatwa kwa Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob (Pichani)kutokana na kutofika mahakamani.

Meya huyo anakabiliwa na shitaka la kumshambulia  mwandishi wa Habari wa gazeti la Uhuru, Christopher Lissa na kumsababishia maumivu makali.

Kesi hiyo jana ililetwa mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Riwa kwa ajili ya usikilizwaji ambapo upande wa mashitaka ulikuwa na shahidi mmoja.

Wakili wa serikali Onolina Mushi alidai kwamba,kesi hiyo ililetwa kusikilizwa lakini mshitakiwa pamoja na wakili wake hawajafika mahakamani.

Kutokana na hali hiyo,aliiomba mahakama itoe hati ya kukamatwa kwa mshitakiwa huyo pamoja na kupanga tarehe nyingine ya kuendelea kusikiliza shauri hilo.

Hakimu alikubali maombi hayo ikiwemo ya kutolewa hati ya kukamatwa kwa Meya huyo.Kesi hiyo iliahirishwa hadi Mei 23 mwaka huu kwa ajili ya usikilizwaji.

Katika kesi hiyo,Boniface anadaiwa kutenda kosa hilo  Septemba 11, mwaka jana, maeneo ya Kinondoni, Dar es Salaam, kipindi hicho akiwa na cheo cha Udiwani kata ya Ubungo.
Ilidaiwa kwamba,mshitakiwa huyo alimpiga Lissa kwa mateke na ngumi sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha makali.

Shitaka la pili ilidaiwa kwamba ,mshitakiwa huyo katika tarehe hiyo kwa makusudi na kinyume cha sheria aliharibu kamera aina ya Nicon yenye thamani ya sh. milioni nane mali ya Kampuni ya Uhuru Publication Limited

Bora Ukimwi Kuliko Kutumia Dawa za Kulevya-Ferooz

Msanii wa kizazi kipya Ferooz amefunguka na kusema ni bora mtu apate virus vya Ukimwi kuliko kutumia madawa ya kulevya kwani anadai mtu akitumia dawa za kulevya mwisho wake ni kuaibika na kushindwa kufanya mambo ya msingi katika jamii.


Akizungumza kwenye kipindi cha eNewz Ferooz alidai kuwa yeye anaona ni bora mtu apate Ukimwi kwani itawezekana mtu huyo kuishi kwa matumaini, huku akiendelea kufanya mambo yake ya msingi katika jamii na kudai tofauti na mtumiaji wa dawa za kulevya kwani hataweza kufanya jambo lolote la maendeleo.

“Madawa ya kulevya ni zaidi ya kupata HIV, ni mara kumi upate Ukimwi kuliko ukiwa unatumia madawa ya kulevya, sababu Ukimwi unaweza kuishi kwa matumaini na ukatumia madawa za ARVs ukaishi miaka mingi ukadumu,lakini madawa ya kulevya utaadhirika na hautafanya kitu chochote katika maisha yaani utakuwa ‘nothing’ (bure) katika maisha, kwa hiyo ni tatizo baya zaidi hivyo madawa ya kulevya si ya kuyasogelea kabisa,” alisema Ferooz.

Mbali na hilo Ferooz alieleza kuwa wasanii wengi wanajikuta wanaingi kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kutokana na msongo wa mawazo kwa kazi zao kutochezwa kwenye vyombo vya habari na kazi hizo kutopokelewa vyema na mashabiki jambo ambalo linawapelekea kuwaza sana hivyo wengine wanaona njia ya kupunguza mawazo hayo ni kunywa viroba kama si kwenda kutumia dawa za kulevya

Prof. Tibaijuka: Rais Magufuli Aache Kutumbua Majipu..Wengine Tunatolewa Kafara na Mtandao Hauguswi



Akiongea na Count Down ya Clouds Fm Prof Tibaijuka amesema yeye ni muhanga wa ufisadi. Amesema kuna mtandao wa mafisadi unaotoa watu kafara na wenyewe hauguswi.

"Naafiki kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi, labda itasaidia kukamatwa na kushitakiwa mafisadi wenyewe. Maana wengine tunatolewa kafara na mtandao hauguswi, labda zitaachwa kukamuliwa nyama na kuziita majipu". Alisema Prof Tibaijuka.

My take:
Mtandao huu ni upi? Unalindwa na nani? Hivi Prof ni msafi au anajitetea?

Zitto: Millioni 50 za Magufuli Kila Kijiji ni Hadaa Kwa Wananchi.

 
MBUNGE wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe, amesema Serikali ya Awamu ya Tano imewahadaa wananchi kuhusu kuwapa Sh. milioni 50 kila kijiji/mtaa huku akiamini ahadi hiyo haitekelezeki.

Zitto alisema ahadi hiyo "kimahesabu, haitekelezeki."

"Kwanza kwenye bajeti ya Waziri Mkuu, fungu lililotajwa la Sh. bilioni 59 halipo. Na hata kama lipo Tamisemi wanakodai wao (Ofisi ya Waziri Mkuu), halitoshi kuvikopesha vijiji vyote Tanzania," Zitto alisema na kuongeza:

"Sh. bilioni 59 katika mwaka wa fedha 2016/17 maana yake vijini 1,000 tu vitapatiwa fedha. Kama serikali inatekeleza ahadi hiyo kwa vijini 1,000 kila mwaka, maana yake ni kwamba katika miaka mitano ya Rais Magufuli Ikulu, ahadi hiyo itatekelezwa katika vijiji 5,000 tu.

"Huku ni kuwahadaa wananchi. Tanzania ina zaidi ya vijiji 15,000. Kwa fungu linalotengwa, vijini zaidi ya 10,000 havitapata fedha hii."

MASHARTI MAGUMU

Wakati Zitto akitoa tahadhari hiyo, imebaini kuwepo kwa vigezo vya kupata fungu la Sh. milioni 50 za kila kijiji/mtaa ni vigumu.

Akihitimiha mjadala wa makadirio ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika mwaka wa fedha 2016/17 wiki iliyopita Majaliwa, alivitaja vigezo saba vitakavyotumika kugawa fedha za mradi huo, huku vyote vikionekana vitakuwa na ugumu kunufaisha wananchi wengi hasa katika maeneo ya vijijini.

Majaliwa alisema mradi huo unalenga kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa njia ya kukopesha vikundi vya wajasiriamali kupitia ushirika wa kuweka na kukopa katika vijiji.

Alivitaja vigezo vya kukopeshwa fedha hizo kuwa ni kikundi cha kifedha kiwe kimesajiliwa na Halmashauri na Tume ya Ushirika, kikundi kiwe na Katiba, uongozi uliochaguliwa kidemokrasia na kupata mafunzo ya mikopo pamoja na kikundi hicho kuwa chini ya Asasi ya Kiraia inayotambulika na yenye uzoefu wa shughuli za mikopo.

Majaliwa alikitaja kigezo cha nne kuwa ni kikundi husika kionyeshe uzoefu wa kukopeshana kwa muda wa mwaka mmoja tangu kuanzishwa na historia ya urejeshaji mikopo ya asilimia 95 na cha tano ni kuwa dhamana ya serikali itakuwa kwenye kiasi cha msingi cha mkopo na si kwenye kiasi riba.

"Kigezo cha sita ni kikundi kuweka amana ya akiba ya fedha kwenye benki katika akaunti maalumu (Fixed Deposit) asilimia 10 ya mkopo," alisema.

Majaliwa alisema kigezo cha saba ni kuzingatiwa kwa Sheria ya Vyama vya Ushirika ya mwaka 2013 kuhusu mkopo kwa SACCOS.

Alisema serikali imeandaa mpango wa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu suala hilo hususan masuala ya ujasiriamali na biashara


Chanzo: Siasahuru.com 

Meya wa Kinondoni Agawa Bure Maeneo ya Biashara Leo na Kufuta Umiliki wa Vibanda na Vizimba 100

 
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam Mstahiki Boniface Jacob amezua taharuki kwa wamachinga wa ubungo na kukimbia biashara zao wakiambatana naye mithili ya Maandamano mara baada ya kutangaza kufuta umiliki wa vizimba na mabanda takriban 100 yaliyokuwa yakimilikiwa na watendaji na Madiwani wa Manispaa ya Kinondoni katika soko la Mawasiliano Maarufu kama Simu 2000 akiagiza wapewe bure.

Mstahiki Jacob aliyefuatana na watendaji wa Manispaa hiyo alitembea kwa miguu akiongea na wamachinga mmoja mmoja na makundi kuanzia Ubungo Plaza hadi ubungo maji akiwaelimisha umuhimu wa oparesheni ya kuwaonda barabarani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya ujenzi wa njia za juu na kuanza kwa usafiri wa mabasi ya kasi Dart ambao hali ilibadilika pale alipotaja Manispaa kuwa na masoko 26 yaliyohodhiwa na viongozi kwa kuingia Mikataba ya kupangisha wakati wamejiagawia bure.

Aidha Mstahiki Meya Boniface Jacob amesema katika kuhakikisha wafanya biashara wadogo wanatengewa maneo yao watafanya uhakiki katika masoko yote kubaini viongozi na watendaji waliojimilikisha na kuwanyang’anya ili masoko yatumiwe na walengwa ikiwa ni hatua ya kuboresha mazingira ya jiji huku mtendaji wa kata ya ubungo Bw. Gilbati Mushi akieleza hatua hiyo kudhirisha utawala bora.

Baada ya Kutoka Marekani Mtoto Getrude Clement Akaribishwa Bungeni Leo


Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali 

Hivi karibuni Getrude  alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchiuliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni  amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.

Getrude amesema kuwa amefarijika kwa kuwawakilisha vijana wa Tanzania na dunia kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo mataifa 175 yalikutana kusaini makubaliano ya Paris.

Katika kuwahimiza vijana kujenga tabia ya kutunza mazingira, Getrude amewaasa vijana hasa wanafunzi kusimamia suala la utunzaji wa mazingira wakiwa shuleni kwa kwa kujiunga na klabu mbalimbali ambapo yeye amejiunga na klabu ya “Mali Hai” iliyopo shuleni anaposoma.

Kwa upande wa Watanzania kwa ujumla kwenye utunzaji wa mazingira, Getrude amesema kuwa ni vema wajifunze kutoka mataifa mengine yanavyosimamia utunzaji wa mazingira hasa matumizi ya mifuko ya plastiki.

Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.
 

Nyumba 400 Zabomolewa Eneo la Iloganzila Jimbo la Kibamba Jijini Dar es Salaam

 

Wakazi waliojenga eneo la Iloganzila Jimbo la Kibamba Dar es salaam leo wamebomolewa nyumba zao ambazo ni zaidi ya nyumba 400, zoezi hilo limekuja baada ya amri iliyotolewa na Mahakama Kuu juzi.

Taarifa zinasema eneo hilo lenye ukubwa wa heka 33, mali ya Henry Kashangaki lilikuwa na mgogoro tangu 1997 baada ya kundi la watu 11 kuvamia na kuanza kujenga nyumba na kuwauzia wananchi wengine.

Baada ya eneo hilo kuvamiwa mmiliki wake aliamua kwenda mahakamani na kuwashtaki Shaha Matibwa na wenzake kumi, kesi hiyo iliendeshwa kwa muda wa miaka mitano na mwaka 2010 hukumu ilitolewa na Kashangaki na Matibwa walionekana wana haki ya kumiliki hivyo walitakiwa kugawana.

Hata hivyo, Kashangaki hakuridhika na hukumu hiyo na kukata rufaa na kwenda Mahakama Kuu, January 2016 kesi hiyo ilitolewa hukumu na Kashangaki alishinda, hivyo juzi Mahakama hiyo ilitoa amri nyumba zivunjwe ili kumpisha mwenye eneo lake.