MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Thursday 9 April 2015

Angalia mwanaume aliyejibailisha kuwa mwanamke swala lililipingwa vikali na rais OBAMA

Obama apinga ubadilishaji wa maumbile

Mwanamume aliyejibadilisha maumbile na kuwa mwanamke 

 Rais Barrack Obama amesema swala la kisaikolojia miongoni mwa vijana ili kubadilisha maumbile yao linafaa kukoma mara moja.
Wengi wa wanaotaka kufanyia mabadiliko ya maumbile yao ni watu wa mapenzi ya jinsia moja hasa vijana.
Mshauri mkuu katika Ikulu ya Marekani Valerie Jarrett amesema kuwa utawala wa Bwana Obama umekubali kwa kauli moja kuwa ushahidi wa kisayansi kuhusiana na maamuzi ya kujibadilisha maumbile, ni swala ambalo haliwezi kukubalika kitaaluma na kimatibabu.
Taarifa hiyo ya Obama inajiri baada ya kifo cha kijana mmoja ambaye alikuwa amebadili jinsia yake na ambaye alijitia kitanzi mwezi wa Disemba baada ya kulazimishwa kuhudhuria mabadiliko hayo ya kimaumbile.

Wednesday 1 April 2015

MWANDOSYA AOMBWA KUGOMBEA URAISI NA VIONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYUO VIKUU MBEYA.


 Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyuo vikuu Mkoa wa Mbeya(CCM),Raymond Mweli akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakikanusha kuhusu wenzao kutumia jina la shirikisho hilo kumshawishi Mwandosya kugombea urais
 Katibu Shirikisho la Vyuo vikuu Mkoa wa Mbeya(CCM),Karimu Nyanga akisoma tamko kuhusu wenzao kutumia jina la shirikisho hilo kumshawishi Mwandosya kugombea urais.
 Baadhi ya viongozi wa Shirikisho wakiwa kwenye mkutano na waandishi wa habari.
 Baadhi ya Waandishi wa habari wakichukua maelezo kutoka kwa viongozi wa shirikisho.

SHIRIKISHO la Wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mkoani Mbeya limeonekana kuwa na mkanganyiko juu ya tamko lililotolewa na baadhi ya wanashirikisho hilo la kumtaka mbunge wa Rungwe Mashariki Prof.Mark Mwandosya kugombea urais.
Mkanganyiko huo umekuja baada ya matamko mawili kutolewa kwa siku tofauti na wanashirikisho hilo,moja likimtaka Prof Mwandosya kuchukua fomu na jingine likilaani tamko la awali kuwa lilikuwa batili.
Tamko lililotolewa  na katibu wa jumuiya hiyo Karimu Nyanga kwa wanahabari lilibainisha kuwa tamko la tarehe Machi 21 la kumtaka Prof Mwandosya kuwania urais halikutolewa na uongozi wa jumuiya kama watoa tamko hilo walivyobainisha.
Nyanga alisema waliotoa tamko hilo walikuwa watu wachache wasio na nia njema juu ya shirikisho,Chama na taifa kwa ujumla,
“Kimsingi tumesikitishwa sana na kuhuzunishwa sana juu ya matamko hayo ambayo yapo kinyume na misingi ya kimaadili ya chama cha mapinduzi licha ya ukweli kwamba watu hawa si viongozi wala hawakuwahi kuwa viongozi wa shirikisho la vyuo vikuu mkoa wa Mbeya.Tunashangazwa na matamko yasiyo na tija kwa shirikisho na kwa chama yaliyotolewa na watu ambao si viongozi wa shirikisho letu” alisema Nyanga.
Alisema msimamo wa shirikisho hilo ni kutofungamana na upande wowote wa urais kwa sasa wakiamini kwamba wakati muafaka ukifika vikao halali vya chama vitawaletea mgombea wa urais anayetosha kupeperusha bendera ya chama chao katika uchaguzi mkuu ujao.
Mnamo Machi 21 mwaka huu watu waliojiita viongozi wa shirikisho hilo mbelea ya wanahabari walitoa tamko la kumtaka Prof Mwandosya kuchukua fomu ya kuwania urais wakisema ana sifa za kuwania nafasi hiyo.
Akisoma tamko hilo Oscar Mwaihabi aliyejitambulisha kama katibu wa shirikisho alisema kwa pamoja wanashirikisho wamekubaliana kumshawishi Prof Mwandosya baada ya kuridhishwa na sifa alizo nazo.
Na Mbeya yetu 

TGNP YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI


 Mtafiti wa maswala ya kijamii kutoka Mtandaowa jinsia Tanzania(TGNP), Dinah Nkya,akitoa mada katika semina ya waandishi wa habari kutoka Kanda ya Nyanda za juu kusini.
 Afisa uhusiano wa TGNP, Melkizedeck Karol akiendesha mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari.
 Waraghibishi kutoka kituo cha maarifa na taarifa cha Tuamke, Nsalaga wakiwa kwenye chumba cha semina baada ya kutoa mambo mbali mbali waliyoyafumbua kutoka vijijini.
Waandishi wa habari wakishiriki semina hiyo.

 IMEELEZWA kuwa iwapo wanawake  wataendelea  kuwa  nyuma katika  kuwania nafasi mbali mbali za uongozi ikiwemo Urais bado changamoto  zilizopo katika jamii  zitaendelea  kuwatesa  wanawake nchini.
 
Kauli hiyo imetolewa  na ofisa mawasiliamo wa mtandeao wa Jinsia Tanzania(TGNP) Melikizedeck  Karol wakati  akitoa  mada ya  ushiriki  wa   wanawake  kwenye  uchaguzi  mkuu mwaka 2015 wakati  wa mafunzo ya siku  mbili ya  wanahabari  mikoa ya  nyanda  za  juu  kusini. Yaliyofanyika jijini Mbeya.
 
Alisema  kuwa  usawa  katika nafasi  za uongozi  wa  kutaka  kuwa na asilimia 50 kwa 50 kati ya  wanawake na  wanaume ni lazima  utimie  katika uchaguzi  huu  kwa  wanawake kuanza  kujitokeza kuwania nafasi  mbali mbali zikiwemo  za  juu kama Urais ,ubunge  na udiwani .
 
Hata hivyo Ofisa huyo alisema kwamba mwaka 2005  kuwa akidi nzima ya  bunge la jamhuri ya  muungano  wa Tanzania  ni wabunge 357 kwa  mujibu  wa katiba  hata  hivyo  viti maalum pekee ni 102 sawa na asilimia 28.6 vilivyogawanywa miongoni mwa vyama vya siasa kwa  kuzingatia  matokeo  ya uchaguzi kati ya  viti 239 vya majimbo (vikiwemo kutoka Zanzibar) ni wanawake 21 tu sawa na asilimia 8.8 ndio  walipewa viti  vya  kuchaguliwa bungeni.
 
 
Alisema ili kuwepo na usawa hakuna budi kwa wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi ikiwemo urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
 
"Hivi  wataka  kusema hakuna  mwanamke katika  nchi hii ambae  anaweza kuongeza nchini kama Rais na kama wapo  kwanini  hawajitokezi  kugombea nafasi za  juu kama Urais .....lazima  wanawake  wachangamkie nafasi  hiyo "
 
Alisema kwa mwaka 2005  kuwa akidi nzima ya  bunge la jamhuri ya  muungano  wa Tanzania  ni wabunge 357 kwa  mujibu  wa katiba  hata  hivyo  viti maalum pekee ni 102 sawa na asilimia 28.6 vilivyogawanywa miongoni mwa vyama vya siasa kwa  kuzingatia  matokeo  ya uchaguzi kati ya  viti 239 vya majimbo (vikiwemo kutoka Zanzibar) ni wanawake 21 tu sawa na asilimia 8.8 ndio  walipewa viti  vya  kuchaguliwa bungeni.
 
Huku  idadi  ya  madiwani  wa  kuchaguliwa  asilimia 4 na  wenyeviti wa  vijiji ni  asilimia 2 wakati  wenyeviti wa vitongoji ni asilimia 3 .
 
 Hivyo  alisema  ni  wajibu  kwa  vyombo  vya  habari na  wanawabari  nchini kuendelea kuhamasisha  makundi  ya  vijana na  wanawake  kujitokeza  kwa  wingi katika nafasi  za  udiwani ,ubunge na Urais katika  uchaguzi  mkuu mwaka huu.
 
Na Mbeya yetu Blog

 

WACHEZAJI SIMBA KUZAWADIWA GARI, MAMILIONI TASLIMU

20150401_105301-1

Kampuni ya EAG Group Limited, imeingia mkataba wa miaka mitano na klabu Simba kwa ajili ya kuitafutia mipango thabiti ya kuiendesha timu hiyo kuhakikisha inapiga hatua katika maendeleo yake.


EAG Group iliingia mkataba na timu hiyo leo asubuhi kwenye hoteli ya Southern Sun iliyopo Posta jijini Dar es Salaam.

  Rais wa Simba, Evans Aveva alisema kuwa kwa kumpitia udhamini wa kampuni hiyo wameandaa tuzo mbalimbali kwa wachezaji wao kuhakikisha wanajituma uwanjani.


Aveva alizitaja tuzo hizo ni ya mchezaji bora wa mwaka atakayepewa gari jipya, mchezaji kijana mwenye kipaji atkayepewa milioni 5 na mchezaji mwenye nidhamu atakayeramba milioni moja.

Pia, wachezaji hao wote kila mmoja atapewa zawadi ya simu aina ya Huawei yenye thamani ya shilingi milioni moja ambao nao wameingia kwenye udhamini huo.

20150401_110238-1“Lengo tunataka kuona timu yetu inapiga hatua katika soka ukanda wa Afrika Mashariki na Afrika Mashariki na Kati na ndiyo tumetoa zawadi hizo kwa ajili ya kuwapa morali wachezaji wetu kupitia Kampuni ya EAG Group Limited na Huawei,” alisema Aveva.


Pia Mkurugenzi wa kampuni ya EAG Group, Imani Kajula alisema kuwa, huo ndiyo wa udhamini kwao, wamepanga kuleta mabadiliko ya soka kwa kuhakikisha wanawekeza zaidi kwa vijana kwa kuanza na Simba.

Andrey Countinho aanza mazoezi Yanga.

Mbrazil wa Yanga, Andrey Countinho ameanza mazoezi mepesi na timu yake katika kile kinachoonekana kuimarika kwa hali yake ya goti.
Countinho aliumia wiki kadhaa zilizopita na alishindwa kusafiri katika safari ya Yanga ya kuelekea Gaborone, Botswana wakati Yanga ilipokuwa inacheza mechi ya marudiano na BDF XI ya nchini humo.
Kufanya mazoezi kwa kiungo huyo kunaleta matumaini kwa Yanga kumtumia katika mechi zake za ligi kuu na zile za Kombe la Shirikisho barani Africa, kwa mujibu wa kocha msaidizi, Charles Boniface Mkwasa.
Countinho anasifika kwa uchezaji wake, hasa kwa upigani wa mipira ya adhabu.
Timu yake inakaribiwa na kibarua cha kuitoa Platinum FC ya Zimbabwe katika michuano hiyo ya Afrika ili icheze hatua inayofuata
Habari zinasema kuwa endapo Yanga itaitoa Platinum, yenye kibarua cha kushinda baada ya kufungwa 5-1 Dar es Salaam, itacheza na moja ya klabu kongwe na yenye uzoefu, Etoile du Sahel ya Tunisia au au S.L Benfica ya Angola katika hatua inayofuata
 

Andy Cotinho katika pozi kwa raha zake

Palestina yapewa uanachama wa ICC

Mahakama ya uhalifu wa kivita ICC
Wapalestina wamepata uanachama wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita miezi mitatu baada ya ombi lao kukubaliwa.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Palestina Riad Malki anatarajiwa kutoa taarifa baada ya kuhudhuria sherehe za makaribisho kwenye mahakama hiyo mjini Hague.
Uanachama wa ICC unaiwezesha Palestina kuifungulia Israeli mashtaka ya uhalifu wa kivita lakini pia utachangia wanamgambo wa Hamas nao kufunguliwa mashtaka.
Serikali ya Palestina inasubiri kutoa malalamishi dhidi ya Israel kuhusu madai ya uhalifu wa kivita mnamo mwaka 2014 katika eneo la Gaza na hatua ya Israel kujenga makaazi katika ardhi yake.

Rais wa Shirikisho la Soka Kenya achafuka kwa rushwa


Kenya
Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), Sam Nyamweya, amechafuka kutokana na jina lake kuwamo kwenye orodha ya watu wanaojihusisha na rushwa nchini humo iliyotolewa leo na Baraza la Maadili na Kuzuia Rushwa (EACC) akihusishwa na utafunaji wa ovyo wa fedha za shirikisho hilo.
Kwa mujibu wa mitandao ya michezo ya Kenya leo, Nyamweya amekamata nafasi ya 92 kwenye orodha ya viongozi ‘wachafu’ kutokana na kujihusisha na rushwa nchini Kenya huku ikielezwa kuwa kesi yake inachunguzwa.
Alhamisi ya wiki iliyopita, yaani Machi 26, Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, aliwataka viongozi wote walioingia kwenye orodha hiyo kukaa pembeni kupisha uchunguzi na tayari viongozi mbalimbali nchini humo wakiwamo Makatibu wa Baraza la Mawaziri, wameshaachia ngazi.
Kinachosubiriwa kwa sasa nchini Kenya ni kuona Nyamweya ambaye amekuwa kiongozi wa juu ya shirikisho hilo tangu 2011, akiacha kazi.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya FKF wamekaririwa wakisema Nyamweya anapambana kuhakikisha anachuguliwa tena kuliongoza shirikisho hilo katika uchaguzi mkuu ujao utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Mtu mwenye umri mkubwa duniani afariki






 
Mtu aliyekuwa na umri mkubwa duniani kutoka nchini Japan amefariki wiki kadhaa baada ya kusherehekea miaka 117 tangu azaliwe.
Misao Okawa alifariki katika kituo cha uangalizi mjini Osaka,mji ambao alizaliwa mwaka wa 1898.
Okawa amewaacha vitukuu sita na wajukuu wanne .
Kufuatia kifo chake kuna madai kwamba kumesalia watu wanne pekee wanaodaiwa kuwa hai ambao walizaliwa karne ya kumi na tisa.
Wote ni Wanaume huku mwanamume wa mwisho akifariki mwaka 2013.

AU yapongeza uchaguzi Nigeria bila furugu yeyote


Mkuu wa Umoja wa Afrika Nkosana Dlamini Zuma
Mkuu wa umoja wa Afrika ,Nkosana Dlamini Zuma anasema kuwa uchaguzi wa Muhammadu Buhari kama rais mpya wa Nigeria unaonyesha ukuwaji wa demokrasi nchini Nigeria.
Rais anayeondoka Goodluck Jonathan ambaye alishindwa kwa kura millioni mbili alimpigia bwana Buhari siku ya jumanne ili kukubali kushindwa.
Msemaji wa bwana Jonathan amesema kuwa alikuwa na furaha licha ya kupoteza uchaguzi huo.
Bwana Buhari hatochukua mamlaka hadi mwisho wa mwezi Mei na atachukua mda wa wiki chache zijazo kujenga serikali yake.
Kiongozi huyo wa zamani wa jeshi alifanya kampeni ya mwana demokrasia anayetaka kusafisha siasa za taifa hilo.