MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYO WEZA KUVUTIA DUNIANI KOTE

Asante kwa kututembelea mbeyagreennews kwa taarifa zaidi endelelea kututembela kila siku ,saa,dakika usipitwe na matukio kem kemu

Friday 31 January 2014

TBL YAPONGEZWA KWA KUJENGA MRADI WA MAJI KITUO CHA AFYA TUNDUMA.

 Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia ya TBL, Doris Malulu, wa pili toka mwisho wakati akikagua mradi wa uchimbaji wa Kisima cha Maji  uliofadhiliwa na Kampuni ya TBL  katika kituo cha Afya cha Tunduma kilichopo Wilayani Momba Mkoa wa Mbeya.



 Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia ya TBL, Doris Malulu,
Alisema ili miradi iwe endelevu na imnufaishe mwananchi aliyekusudiwa ni vema suala la uangalizi likawa shirikishi kwa kila mtu ambapo itakuwa misaada kwa vizazi vijavyo na kwamba kampuni hiyo imelenga kituo cha Afya kwa kuwa ndiyo kimbilio la Watu wengi.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji mdogo wa Tunduma, na pia ni mkaguzi wa ndani  Helen Kagamizi, aliishukuru Kampuni ya Tbl kwa msaada wa kisima cha maji katika Kituo cha Afya kwa kile alichosema Mji wa Tunduma unatatizo kubwa la uhaba wa maji.





Mganga wa Kituo hicho Dk. Gbson Mbaza alienyoosha mkono  alisema Tbl imetoa msaada mkubwa na muhimu katika sekta ya afya kwa sababu huduma hiyo inahitaji huduma ya maji kwa wingi kutokana na mahitaji ya usafi kwa wagonjwa na mazingira kuhitaji maji mengi.






KAMPUNI ya Bia Tanzania(TBL) imezitaka Halmashauri mbali mbali nchini ambako miradi mingi ya kijamii inatekelezwa kutokana na misaada ya Wahisani kutoa uangalizi ili iwe endelevu kwa manufaa ya wananchi ambao ndiyo walengwa.

Ombi hilo limetolewa na Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia ya TBL, Doris Malulu,wakati akikagua mradi wa uchimbaji wa Kisima cha Maji  uliofadhiliwa na Kampuni hiyo katika kituo cha Afya cha Tunduma kilichopo Wilayani Momba Mkoa wa Mbeya.

Doris alisema maeneo mengi wanapeleka miradi ambayo Serikali ilitakiwa kuifanya ambapo baada ya kufanikisha miradi hiyo na walifadhili kuondoka miradi hiyo hufa kutokana na kukosekana kwa uangalizi toka Serikalini.

Alisema ili miradi iwe endelevu na imnufaishe mwananchi aliyekusudiwa ni vema suala la uangalizi likawa shirikishi kwa kila mtu ambapo itakuwa misaada kwa vizazi vijavyo na kwamba kampuni hiyo imelenga kituo cha Afya kwa kuwa ndiyo kimbilio la Watu wengi.

Aliongeza kuwa msaada wa kisima hicho unagharimu zaidi ya Shilingi Milioni 24, ambapo alisema TBL imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu iliyojiwekea ya kurudisha fadhila kwa jamii kutokana na faida wanayopata kutokana na mauzo ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji mdogo wa Tunduma, Helen Kagamizi, aliishukuru Kampuni ya Tbl kwa msaada wa kisima cha maji katika Kituo cha Afya kwa kile alichosema Mji wa Tunduma unatatizo kubwa la uhaba wa maji.

Alisema mradi huo utakapoanza kufanyakazi utakuwa mkombozi kwa watu wengi hususani wagonjwa ambao ndiyo wahitaji sana wa Maji na kwa mujibu   Mkandarasi anayechimba kisima hicho anasema kinaweza kuzalisha Mililita 5000 kwa saa.

Naye Mganga wa Kituo hicho Dk. Gibson Mbaza alisema Tbl imetoa msaada mkubwa na muhimu katika sekta ya afya kwa sababu huduma hiyo inahitaji huduma ya maji kwa wingi kutokana na mahitaji ya usafi kwa wagonjwa na mazingira kuhitaji maji mengi.

Aliongeza kuwa maji hayo watayatunza vizuri ili yaweze kuwasaidia katika shughuli za kila siku za matibabu na wagonjwa kutokana na kukabiliwa na upungufu wa maji safi na salama kwa mji mzima wa Tunduma.


Na Mbeya yetu

SAMATTA MCHEZAJI BORA WA MWAKA TP MAZEMBE



Samata-Bwana58021_6e83d.jpg

MBWANA Ally Samatta ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2013 wa klabu ya Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Mshambuliaji huyo wa Tanzania, maarufu kama Sama Goal amewashinda Solomon Asante na Robert Kidiaba alioingia fainali.
Samatta alipata kura 248, Asante Solomon kura 219, Robert Kidiaba kura 200, Nathan Sinkala kura 97 na Rainford Kalaba kura 67.
Mafanikio hayo yametokana na Samatta kuwa tegemeo la mabao la Mazembe kuanzia Ligi Kuu ya DRC, Ligi ya Mabingwa na baadaye Kombe la Shirikisho, ambako timu hiyo ilifika fainali. Mazembe inaye Mtanzania mwingine, Thomas Ulimwengu.

DAKIKA ZA MWISHO ZA DIRISHA LA USAJILI: TETESI NA USAJILI ULIOKAMILIKA - NDIO HUU HAPA





Kim Kallstrom amekamilisha upimaji wa afya wa kujiunga na mkopo na Arsenal akitokea Spartak Moscow - wakati huo huo uhamisho wa mchezaji mkongwe wa kijerumani Miloslave Klose kuja Emirates umeshindikana rasmi.


Uhamisho wa beki Eliaqum Mangala na mwenzie Fernando kutoka umekwamba na wachezaji hao wameonekana kwenye ndege wakielekea jijini Madeira kwa ajili ya mechi ya Ligi ya Ureno kesho.

Papiss Cisse amekataa kujiunga na klabu ya Uturuki Trabzonspor lakini msenegal huyo bado anaweza kuuzwa usiku huu ikipatikana ofa ambayo Newcastle wanaitaka. 
Borussia Monchengladbach bado wanamhitaji mshambuliaji wa Newcastle.



Wilfred Zaha amejiunga rasmi na Cardiff City kwa mkopo akitokea Manchester United


Chelsea wamethibitisha kumsajili Kurt Zouma kutoka St Etienne, lakini mlinzi huyo ataendelea kubakia kwenye timu hiyo ya Ufaransa mpaka mwisho mwa msimu. 
Kinda hilo lenye miaka 19 amejiunga na Chelsea kwa mkataba wa miaka mitano na nusu. 
Emmanuel Frimpong amejiunga na Barnsley akitokea Arsenal

Kocha wa Manchester United amethibitisha rasmi kwamba wapenzi wa klabu hiyo wasitegemee kusajiliwa kwa mchezaji yoyote leo hii zaidi baadhi ya wachezaji wataondoka kwa mkopo.
Adel Taarabt amekamilisha usajili wake wa kujiunga na AC Milan akitokea QPR
Lewis Holtby amekamilisha uhamisho wake kutoka Tottenham kwenda Fulham kwa mkopo

VPL: KUENDELEA LEO SIMBA v JKT OLJORO, UWANJA WA TAIFA!


>>VIINGILIO: KUANZIA 5,000/=
>>JUMAPILI: YANGA v MBEYA CITY, AZAM v KAGERA SUGAR!
>> SERENGETI BOYS YAPANGIWA AFRIKA KUSINI, KOMBE LA AFRIKA!
>> TFF MPYA YATIMIZA SIKU 100
>> BODI YA LIGI YAZIPIGA JEKI KLABU ZA FDL!
SOMA ZAIDI:
VPL_2013-2014-FPRelease No. 015
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 31, 2014
SIMBA YAIKARIBISHA OLJORO JKT DAR
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania inaingia raundi ya 16 wikiendi hii kwa mechi nne ambapo kesho (Februari 1 mwaka huu) Simba itakuwa mwenyeji wa Oljoro JKT katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Viingilio katika mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 10 kamili jioni ni sh. 5,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A. Refa atakuwa Nathan Lazaro kutoka mkoani Kilimanjaro wakati Kamishna ni Hakim Byemba wa Dodoma.
Uwanja wa Azam uliopo Mbagala siku hiyo kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Ashanti United na Mgambo Shooting kutoka Handeni mkoani Tanga kwa viingilio vya sh. 3,000 kwa sh. 10,000.
Jumapili (Februari 2 mwaka huu) ni Yanga vs Mbeya City (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, saa 10 kamili jioni), na Azam vs Kagera Sugar (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi saa 10 kamili jioni).
Ligi hiyo itaendelea Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kwa mechi kati ya Tanzania Prisons vs Coastal Union (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), na JKT Ruvu vs Ashanti United (Uwanja wa Azam Complex, Chamazi).
SERENGETI BOYS YAPANGIWA AFRIKA KUSINI
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) itacheza na Afrika Kusini katika mechi za mchujo kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa umri huo zitakazofanyika mwakani nchini Niger.
Serengeti Boys ambayo pamoja na nchi nyingine 17 zimeingia moja kwa moja katika raundi ya pili itaanzia mechi hiyo nyumbani kati ya Julai 18-20 mwaka huu wakati ile ya marudiano itafanyika nchini Afrika Kusini kati ya Agosti 1-3 mwaka huu.
Ikifanikiwa kuitoa Afrika Kusini, Serengeti Boys itacheza mechi ya raundi ya tatu na ya mwisho na mshindi wa mechi kati ya Misri/Sudan vs Congo Brazzaville.
Nchi nyingine ambazo zimeingia moja kwa moja raundi ya pili ni Afrika Kusini, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Congo Brazzaville, Ethiopia, Gabon, Ghana, Ivory Coast, Mali, Morocco, Nigeria, Rwanda, Senegal, Tunisia na Zambia.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inatarajia kutangaza benchi la ufundi litakaloiongoza Serengeti Boys hivi karibuni.
TFF MPYA YATIMIZA SIKU 100
Kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) chini ya Rais Jamal Malinzi, Februari 4 mwaka huu inatimiza siku 100 tangu iingie madarakani katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 28 mwaka jana.
Hivyo, Rais Malinzi atazungumza na waandishi wa habari Februari 7 mwaka huu kuelezea utekelezaji wa Ilani yake ya uchaguzi. Muda na mahali utakapofanyika mkutano huo mtaarifiwa baadaye.
BODI YA LIGI YAZIPIGA JEKI KLABU ZA FDL
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetoa sh. milioni 1.5 kwa kila klabu ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Uamuzi wa kuzisaidia timu hizo ulifanywa katika kikao cha TPLB kilichofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam ambapo fedha hizo zitalipwa kupitia kwenye akaunti za klabu husika. Hivyo klabu ambazo hazijawasilisha akaunti zao TPLB zinatakiwa kuwasilisha haraka.
Klabu za FDL ni African Lyon, Burkina Moro, Friends Rangers, Green Warriors, Kanembwa JKT, Kimondo, Kurugenzi Mafinga, Lipuli, Majimaji, Mkamba Rangers, Mlale JKT na Mwadui.
Nyingine ni Ndanda, Pamba, Polisi Dar es Salaam, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Morogoro, Polisi Tabora, Stand United, Tessema, Toto Africans, Trans Camp na Villa Squad.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MAHAKAMA TANZANIA YAWAACHIA HURU WAANDISHI WA HABARI

 
kisutu_c1318.jpg
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Meneja Uendelezaji Biashara wa Mwananchi Communications (MCL), Theophil Makunga, aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Akizungumza na idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika(VOA ) Absalom Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri amesema maamuzi ya mahakama hiyo yamerejesha matumaini mapya kwa tasnia ya habari kwa wanahabari na vyombo vya habari kwamba pamoja na sheria kandamizi wanayo fursa ya kushinda baadhi ya hila, baadhi ya mipango ya kudhulumu vyombo vya habari nchini Tanzania.

Akielezea maamuzi ya mahakama hiyo amesema kwamba mahakama iliamua kuwa serikali ilifungua kesi hiyo katika misingi ya hisia kwani yalioandikwa ni masuala ya kawaida hakukuwa na nia ya uovu, waandishi walitumia uhuru wao wa kujieleza na hakukuwa na matukio yeyote ya wazi kwamba baada ya ile makala kumekuwa na vitendo au matukio yaliotokana na uandishi wa makala hiyo.
Amesema maamuzi hayo yatalazimisha mabadiliko kwani ni sawa na kujifunza kwa viboko kwani kuna dhamira mbaya na chuki za wazi dhidi ya vyombo vya habari, ni fundisho kwamba lazima walio madarakani, waandishi na wananchi wa kawaida wanapaswa kujifunza kwamba hakuna aliye juu ya sheria.
Amesema wana imani kupitia mchakato wa katiba mpya kuwa wataweza kupata fursa ya kuingiza masuala mengi yanayohusu uhuru wa vyombo vya habari katiba katiba mpya ijayo nchini humo.
Akielezea zaidi kuhusu chuki dhidi yao amesema upande mmoja ni kwasababu ya waandishi wenyewe na kwa upande mwingine viongozi walioko madarakani hawapendi kukosolewa kutokana na tabia zao akitolea mfano matumizi mabaya ya madaraka ya Polisi.
Chanzo, voaswahili.com