Saturday 26 July 2014

Kanali Ngemela Lubinga awataka madiwani kusimamia miradi kwa ukaribu

???????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanali Ngemela Lubinga  akifungua kikao mkutano mkuu wa mwaka wa baraza la madiwani Halmshauri ya NSIMBO Mbele ya wajumbe wa kikao hicho pamoja na watalaam wa Halamshauri hiyo
……………………………………….
Na Kibada Kibada –Nsimbo Katavi.
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanali Ngemela Lubinga amewataka madiwani kusimamia kwa ukaribu miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yao kwa kuwa wao wana dhamana kubwa katika jamii wanayoingoza kama wawakilishi wa wananchi kwenye Vikao vya maamuzi hivyo ni wajibu wao kutimiza wajibu huo. Kanali Lubinga aliyasema hayo wakati akifungua kikao cha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Fedha uliokwisha wa 2013/2014.na kueleza kuwa uwakilishi ni dhamana kubwa katika jamii ambayo ni wananchi unaowawakilishi hivyo wanatakiwa kuwatendea haki kwa kutimiza wajibu wako waliokabidhiwa katika jamii ya uwakilishi ikiwa ni pamoja na kusimamia kwa umakini utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoko kwenye Halmashauri katika eneo husika.
Alisema matatizo yaliyoko kwenye eneo la diwani unatakiwa kuyatambua na kuyapatia maamuzi mfano wizi unatokeo kwenye eneo lako kama wizi wa Soral Kijiji cha Ugala pale upo uongozi upo kuanzia ngazi ya Kijiji,Kata na Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo katika Kata ni Diwani na wataalamu wake wapo pia na Diwani yupo katika eneo , kweli kama upo uwajibikaji na kutimiza wajibu wananchi wangeweza kutoa ushirikiano na mali kama hiyo isingeibiwa kwa kuwa wanaona ni mali ya jamii kwa manufaa ya jamii lazima watailinda kwa gharama yeyote ili ila kama hakuna uwajibikaji na ushirikiano basi wananchi hwawezi kutoa ushirikiano.. Akasema siwajibu wa viongozi kuktaa watu bali wanasimamiwa ukiwasimamia kwa ukaribu matatizo yaliyopo kwenye eneolako utayafahamu na kutafuta njia ya kuyapatia ufumbuzi kabla hayajawa makubwa .
Akizungumzia suala la ujenzi wa Maabara alieleza kuwa Halmashauri ya Nsimbo iko nyuma katika utekelezaji wa agizo la Rais na agizo la Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe lakuzitaka halmashauri zote kukamilisha ujenzi wa Maabara kwa shule za Sekondari ifika mwezi Novemba hali ya ujenzi inakwenda kwa kusuasua mno tofauti na maeneo mengine katika Mkoa.
Mkuu huyo wa wilaya ameitaka Halmashauri kuwatumia na kutumia fursa zilizopo katika Hlamshauri hiyo hasa makampuni ya uchimbaji madini nay ale ya nayojishughulisha na unuzi wa tumbuka kuhakikisha wanawashirikisha wasaidie katika ujenzi wa Maabara.
Akasisitiza kuwa Mkoa wa Katavi na Halmashauri ya Nsimbo wanaoutajiri wa kutosha watumieni hawa watu waweze kuwasidia katika kujenga maabara hizo hawa wanachuma mali kwenye halmashauri yetu haiwezekana na wao wasisaidie watalaam tumieni Talaam zenu kuwasiadia wananchi hao. Akasema hataki kusikia shule hazina madawati katika Wilaya yake na ameisha agiza mamlaka inayohusika kutoa kibali au leseni ya kuvuna kupasua mbao katika Wilaya yake mvuna huyo lazima achangie madawati 300 hiyo ni lazima kwa kuwa ni agizo lasivyo asipewe leseni hiyo ya kupasua mbao kama hataki kuchangia madawati hayo. Katika hatua nyingine amewaagiza watendaji wa Halmashauri hasa Idara ya utumishi kuondoa kero na manunguniko kwa watumishi wanaolalamikia kututendewa haki kwa kulipwa masilahi yao nap engine posho zao akasema iwapo malalamiko yatazidi watu watachukia na kuichukia serikali yao vita ya namna hiyo siyo lahisi kuishinda ni vyema watu wakasilikizwa na kupewa haki zaowanazodai kama madai yao mbalimbali katika Halmashauri.
Kwa upande wake Mweyekiti wa Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Assenga alieleza kuwa kuwa kwa kuwa wote ni viongozi watajitahidi kutekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ili kuhakikisha maendeleo katika Halmashauri yanakwenda kama inavyotakiwa kwa kuwaletea wananchi maendeleo kwa mstakabali wa Taifa. Katika kikao hicho ambacho kilikuwa ni Mkutano Mkuu wa mwisho wa Mwaka wa fedha unaoishia 2013/2014 Taarifa mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na shughuli nyingine ziliwasilishwa na kujadiliwa na kupatiwa majibu.

0 comments: