Sunday 27 April 2014

KUUMIA KWA GONZALO HIGUAIN NI MSIBA KWA KLABU YA NAPOLI,


396113_heroa 
KLABU ya Napoli imekumbwa na wasiwasi mkubwa baada ya kuumia kwa Gonzalo Higuain katika mechi yao na Inter Milan hapo jana uwanja wa San Siro iliyomalizika kwa suluhu (0-0).
Mshambuliaji huyo raia wa Argentina alilazimika kutoka katika mchezo huo wa Seria A baada ya kugongana na beki wa Inter, marco Andreolli.
Napoli wamethibitisha leo hii kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid amepata majeruhi ya kifundo cha mguu na kuwa hatarini kukosa mechi ya Coppa Italia wiki ijayo.
“Amepata majeruhi makubwa sana kwenye mguu wake” amesema taarifa ya klabu.
“Majibu hayo yametokana na uchunguzi uliofanywa na madaktari wa klabu juu ya hali ya Gonzalo Higuain baada ya kugongana na Andreolli kwenye mechi ya Inter dhidi ya Napoli”.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: