Saturday 26 April 2014

MWAMBUSI: KOCHA BORA LAZIMA AJIAMINI NA KUSHIKILIA FALSAFA YAKE

1a31 
Na Baraka Mpenja  , Dar es salaam
KOCHA wa Mbeya City fc, Juma Mwambusi  amesema kuwa kuwaamini vijana katika klabu  kunahitaji kuwapa muda ili kufikia malengo.
Mwambusi amesema kuna mambo mawili yanatakiwa kuzingatiwa katika falsafa za mpira.
Mosi; falsafa ya mpira huwezi kuwajumuisha makocha wote kwasababu kila mtu ana falsafa yake.
Pili; kila klabu inakuwa na falsafa yake, hivyo inahitaji kocha atakayeiweza .
Mwambusi aliendelea kufafanua kuwa klabu inapokuwa na falsafa yake, mfano kutumia soka la vijana, lazima inakuwa na falsafa mbadala ili kama itashindikana mpango A basi waende mpango B.
Kocha huyo alisema si jambo la ajabu kuona timu inabadili mfumo wa soka lake ndani ya msimu mmoja, lakini inategemeana na malengo ya klabu.
Akizungumzia falsafa kwa Makocha, Mwambusi alisema kuna changamoto kubwa kwa walimu wa kitanzania kwasababu huwa hawajiamini katika mifumo yao.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: