Tuesday 29 April 2014

RAIS WA BRAZIL AMUUNGA MKONO DANI ALVES

 
140428164329_dani_alves_banana_512x288_bbc_nocredit_cc87b.jpg
140428100001_dani_alves_barcelona_512x288_reuters_nocredit_7950e.jpg
swala  tata la ubaguzi wa rangi katika michezo limeibua mchango wa rais wa Brazil.
Rais Dilma Rousseff, amesifu kitendo cha mchezaji wa kimataifa wa Brazil, na Barcelona Dani Alves kutokana na tukio la ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya ligi kuu ya Uhispania, La Liga kati ya Barcelona na Villareal .
Mchezaji huyo wa Barcelona aliokota ndizi aliyokuwa ametupiwa na kuila kabla ya kuitupa na kuendelea na mchezo.
Bi Rousseff aliandika katika mtandao wake wa twitter kuwa Dani Alves alionyesha ujasiri wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi katika kandanda na kuwa ni tukio la kuigwa .
Klabu ya Villarreal inasema kuwa imempiga marufuku mwanaume ambaye alitupa ndizi hiyo uwanjani na kuwa hatohudhuria mechi zote za nyumbani za klabu hiyo maishani.
Mamia ya watu na wachezaji maarufu duniani wameonyesha upendo wao kwa mchezaji huyo kwa kuweka picha zao kwenye mitandao wa kijamii wakila ndizi.
Mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero alipachika picha akila ndizi sawa na nyota wa soka la wanawake Marta .
Wengine ni Luiz Suarez wa Liverpool,Oscar, David Luiz na Willian wote wa Chelsea .
Rais wa Fifa sepp Blatter ameongezea sauti yake katika tukio la hivi punde akisema ni vibaya kwa dhulma hizo kuendelea katika karne hii.CHANZO BBC

0 comments: