Tuesday 29 April 2014

MREFA WACHEKELEA TAIFA STARS KUIVAA MALAWI SOKOINE

Staz 
Na Baraka Mpenja   Dar es salaam
CHAMA cha soka mkoani Mbeya, MREFA, kimeendelea kujivunia mafanikio ya kuaminiwa na shirikisho la soka Tanzania TFF kwa kuziweka timu za Taifa mkoani Mbeya.
Mwenyekiti wa MREFA, Elias Mwanjala ameuambia mtandao huu kuwa kuwekwa kambi ya maboresho ya Taifa stars mjini Tukuyu ilikuwa fursa nzuri kwa wafanyabiashara na wapenzi wa soka mkoani humo kuiona timu yao.
Mwanjala aliushukuru uongozi wa TFF chini ya rais Jamal Malinzi kwa kuendelea kuwapa fursa muhimu kama hizo na hasa baada ya kuamua mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Taifa Stars na Malawi kufanyika mkoni humo.
“TFF wanajua juhudi zetu. Uwanja wa Sokoine ulikuwa mbaya sana, lakini tumeuboresha kwa nguvu zote na sasa mechi ya kirafiki ya Taifa stars inafanyika katika uwanja huu. Hii ni heshima kubwa kwa MREFA”.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: