Wednesday 30 April 2014

AL AHLY YAPANGWA KUNDI LA ‘KIFO’ KOMBE LA SHRIKISHOB


VIGOGO wa Misri, Al Ahly wamepangwa katika Kundi B la Kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2014 pamoja na Sewe Sport ya Ivory Coast, Etoile du Sahel ya Tunisia na Nkana FC ya Zambia.
Katika droo iliyopangwa leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), wababe wa Cameroon, Coton Sport wametupwa Kundi A pamoja na ASEC Mimosas ya Ivory Coast, AS Real ya Mali na AC Leopards ya Kongo Brazzaville.
Kundi la kifo; Al Ahly imepangwa kundi gumu Kombe la Shirikisho Afrika 


Mechi zinatarajiwa kuchezwa kuanzia kati ya Mei 16 na 18 na Juni 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na 22-24 na washindi wawili wa kila kundi watasonga Nusu Fainali.MAKUNDI KOMBE LA SSHIRIKISHO:
KUNDI A: AC Leopards, ASEC Mimosas, AS Real Bamako na Coton Sport
KUNDI B: Al Ahly, Etoile du Sahel, Sewe San Pedro na Nkana FC

0 comments: