Sunday 27 April 2014

MHOLANZI LOUIZ VAN GAAL AMBAKISHA RVP MAN UNITED

372084_heroa 
HALI shwari sasa!. Mshambuliaji wa Manchester United, Mholanzi, Robin Van Persie ameamua kuendelea kukaa katika klabu hiyo kufuatia kufukuzwa kwa David Moyes.
Kilichomvutia  zaidi nyota huyo ni klabu hiyo ya Old Trafford kutaka kumleta Mholanzi mwenzake, Louis Van Gaal kurithi mikoba ya ukocha mkuu.
Taarifa za kuaminika zinaeleza kuwa Van Gaal tayari ameshakubali vipengele vya mkataba saa 48 zilizopita ili kuwa kocha wa kudumu wa Man united.
Sio siri kuwa Van Persie amekuwa na mahusiano mazuri na kocha wake wa timu ya taifa na sasa anaona itakuwa jambo zuri kukaa pamoja Old Trafford baada ya kumalizika kwa fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

0 comments: