Thursday 17 April 2014

ABDALAH MIHEWA AMSHANGAA DK WILBROAD SLAA

Dr-Wilbroad-Slaa-300x214

Na Gladness Mushi, Arusha

MJUMBE wa kamati kuu ya CCM, taifa, Abdalah Mihewa, amemshangaa ,Katibu mkuu wa Chadema, Dakta Wilbroad Slaa, kwa kubeza maendeleo yaliyopatikana jimboni Karatu.


Mihewa amesema hayo jana kwenye ofisi ya CCM, wilaya ya Karatu, baada ya kupokea salaam za Chama kutoka kwa katibu wa Chama wilatya ya Karastum, Elly Minja, na kusema kuwa,kiongozi huyo hana shukurani.


Mihewa ambae pia ni katibu wa CCM, mkoa wa Dar es  Salaam, aliyekuwa ziarani wilayani Ngorongoro, kusimamia uchaguzi wa viongozi wa baraza la Umoja wa vijana mkoa wa Arusha, amesema serikali ya CCM, imefanya mengi jimboni Karatu ikiwemo kujenga bara bara ya Lami kutoka Arusha hadi Lango kuu la Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, pia serikali imetekeleza mradi mkubwa wa maji kwa wananchi wa Karatu jambo ambalo ni ukombozi mkubwa lakini Salaa bado anabeza kuwa hakuna kilichofanyika .


Amesema kuwa Serikali ya CCM, inahudumia watanzania wote bila kujali itikadi hata kama majimbo yanaongozwa na wapinzanilazima wananchi waliopo watapata huduma bila ya ubaguzi wala upendekleo.


Serikali ya CCM,inaboresha miundo mbinu nchini kote bila kujalilakini leo mtu mzima anaponda na kubeza huyo ana matatizo ya akili hata angelikuwa ni kipofu basi angelipapasa aone nini kilichofanywa na serikali ya CCM,jimboni humona sio kubeza


Akawataka viongozi na wananchi kuimarisha mshikamanona kujipanga kulikomboa jimbo hilo ili kuharakisha maendeleo ya wananchi .


Awali  Katibu wa  CCM, Wilaya ya  Karatu, Elly Minja, katika salam zake amesema wananchi wilayani Karatu wamechoshwa na miaka 17 ya Chadema tangia kuchukua jimbbo hilo wamekwama kimaendeleo.


Amesem,a wananchi jimboni humo wanadai wameschoshwa na maneno bila vitendo sasa wanajiandaa kuking’oa chama cha Chadema, ili waweze kupata maendeleo kutoka Chama cha mapinduzi ambacho serikali yake inawapatia huduma mbalimbali ikiwemo mnradi mkubwa wa maji ambao limekuwa ni tatizo kubwa na la kudumu.


Amesem,a wananchi pia wamechoshwa kufanywa ngome ya Chadema,na sasa wameahidi katika uchaguzi mkuu ujao kukiondoa chama hicho cha Chadema..

0 comments: