Sunday 2 June 2013

POLISI SUMBAWANGA WAKAMATA MTENGENEZA SILAHA




 
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia Samweli Sikazwe(40)kwa kukutwa akimiliki magobore sita kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa may 31 kwa operesheni kali ya kusaka wahalifu inayoendeshwa na polisi mkoa Rukwa .

Kaimu kamanda wa polisi Peter Ngusa alisema kuwa uchunguzi wa awali ulibaini kuwa mtuhumiwa alikuwa akijihusisha na utengenezaji wa silaha hizo alizokuwa akiwauzia watu ambao huzitumia kutenda uhalifu.

Katika  tukio lingine mwanamke Lucy kiwi (60)mkazi wa kirando katika wilaya ya nkasi mkoani Rukwa amekamatwa akiwa na pombe ya moshi lita 450 nyumbani kwake.

Mtuhumiwa alikamatwa mnamo may 28 saa 2.30 alikiwa anauza pombe hiyo haramu alimaarufu kama(gongo).

Aidha Operesheni hiyo pia imefanikiwa kumnasa Juma Andrew(25)mkazi wa jangwani kmanispaa ya sumbawanga akiwa na debe 2 za bhangi kavu akiwa katika harakati za kuiuza soko la mandela lililopo mjini hapa.

Watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara tu uchunguzi wa awali utakapo kamilika.


Na Elizabeth Ntambala
  RUKWA

0 comments: