Saturday 22 June 2013

HAFLA FUPI A KUAGWA KWA SPIKA SITTA

 
Picture
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi zake pichani kwa Spika mstaafu. Samuel Sitta katika hafla ya kumuaga Spika huyo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 21, 2013. Kushoto kwake ni mkewe Tunu na wengine kutoka kulia ni Mkewe Spika Mstaafu, Margareth Sitta, Spika mstaafu, Samuel Sitta na Spika wa Bunge, Anne Makinda. (picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mhe. Samuel John Sitta (Mb, W, CCM) alishika wadhifa wa kuliongoza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwishoni mwa mwaka 2005 hadi 2010.

Habari nyepesi nyepesi kuhusu halfa ya kumuaga jana zinapasha kuwa Wabunge wa CUF waliohudhuria hafla hiyo walisusia na kuondoka ukumbini baada ya nyimbo zilizopigwa kuwakera, hasa ule wa kuwananga wapinzani wenye kiitikio chenye maneno, "...tuwachanechane tuwatupe!"

Wabunge wa CHADEMA wao inasemekana hawakuhudhuria hata mmoja.

0 comments: