Sunday 2 June 2013

KUDONDOKA KWA UKUTA WA TANGI LA MAJI LA UAWA WATU 3 LEO PEMBA

   ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiwa katika zoezi la kuokoa miili ya Marehemu waliopoteza maisha katika ajali ya kuangukiwa na Ukuta wa tangi la Maji Machomanne Chake Chake Pemba leo
 
 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiutoa mwili wa Marehemu juu ya Mnara wa tangi la Maji Machomanne, ulioangukiwa na ukuta wa tangi hoo



 WANANCHI mbali mbali wakiuangalia mnara wa Tangi la Maji Machomanne, ulioanguka na kupoteza maisha ya wananchi watatu leo asubuhi. (picha na Abdi Suleiman


 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiushusha chini mwili wa marehemu aliyepoteza maisha baada ya kuangukiwa na ukuta wa mnara wa Tangi la Maja Machomanne Pemba



 ASKARI wa vikosi vya Ulinzi na Usalama kisiwani Pemba, wakiupeleka mwili wa marehemu katika gari ya kubebea wagonja, ulioelemewa na ukuta wa mnara wa Tangi la Maji Machomanne Pemba
 WANANCHI mbali mbali wakiwa katika hospitali ya chake chake , wakitizama miili ya ndugu zao waliopoteza maisha baada ya kuangukiwa na mnara wa tangi la maji Machomanne Pemba
 Mkuu wa mkao wa kusini Pemba, Juma Kassim Tindwa, akimfahamisha jambo waziri wa Nnchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mohammed, walipofika katika Hospitali ya Chake Chake, kuaangalia majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo.
DAKTARI bingwa kutoka Quba anayefanya kazi zake kisiwani Pemba, (jina halikufahamika) akimtibu mmoja kati ya majeruhi waliolazwa katika hospitali ya chake chake, kufuatia kuwangukiwa na ukuta wa mnara wa tangi la Maji Mchomanne Pemba. 



JUMLA ya watu watatu wamefariki ndunia papo hapo na watatu kujeruhiwa baada yakuangukiwa na ukuta mnara wa tangi la maji uliopo machomanne chake chake pemba, majira ya saa tatu za asubuhi ya leo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Suleiman Hassan Suleima, amesema kuwa, merehemu hao walifikiwa na mauti wakiwa katika kazi ya kuteremsha ukuta wa mnara wa tangi la maji ambao walikuwa wameshaukata.
Kamanda Suleimana alisema kuwa, ukuta huo ulikuwa tayari umeshafanya ufa wa kupasuka, hivyo wakati wakiwa kazini kuuteremsha ukuta huo, ulianguka na kuwaelemea marehemu hao pamoja na mejeruhi waliokuwa juu wakiuteremsha ukuta huo.
Kamanda alisema kuwa idadi ya mafundi waliokuwepo kazini hapo, walikuwa ni watu 12 ambapo watatu wamepoteza maisha papo hapo na watatu kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya chake chake na wengine sita walikimbia na jeshi la polisi liko katika utaratibu wa kuwatafuta kwa ajili ya kuelewa hali zao.

Aliwataja marehemu hao kuwa, ni Juma Rashid Juma (35)mkaazi wa chanjaani, Suleiman Mohammed Abdiadi “maarufu golo” (55) mkaazi wa kwale na Salum Muhidini Vuai “Bandudu” (35) mkaazi Madungu wote ni wakaazi wa wiliya ya chake chake mkoa wa kusini Pemba.
Aliwataja majeruhi kuwa ni Jakson John (26) mzaliwa wa Iringa mkaazi wa msingini, Ali Saleh Ali (35) mkaazi wa michakaeni na Yohana Richerd (25) mkaazi wa machomanne Chake Chake Pemba.
“baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi tulifika katika eneo la tukio na tukashirikiana kikamilifu na wenzetu wa vikosi vya ulinzi na usalama wote wa pemba katika kuokoa maisha ya wananchi wetu waliokuwepo hapo”alisema kaimu kamanda Suleiman.
Aidha aliwataka wananchi kutoa mashirikiano pale panapotokea majanga kama hayo, ili kuweza kuokoa maisha ya wananchi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, DK Hilali Juma Mohammed, wa Hospitali ya Chake Chake, amesema kuwa kati ya marehemu hao watatu, wawili waliumia kichwa, Kifua na Mikono.
Alisema kuwa merehemu Suleiman Mohammed Abdiadi “maarufu golo” aliumia sehemu za kichwa ambacho kilikatika moja kwa moja, Kifua na Mikono, hivyo baada ya kumaliza taratibu za uchunguzi waliweza kuzikabidhi maiti hizo kwa ndugu na Jamaa zao.
“Tulishirikiana kikamilifu na vikosi vya ulinzi na usalama vyote pamoja na uongozi wa Serikali ya Mkoa wa Kusini Pemba, katika kuwakabidhi miili hiyo kwa jamaa wa marehemu kwa ajili ya Mazishi”alisema Dk Hilali.
Akitoa tamko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohammed Aboud Mhammed, aliwataka wananchi waliopoteza ndugu zao katika aji ya kuangukiwa na ukuta huo, kuwa na subra katika kipindi hichi kigumu kwao.
Alisema kuwa msiba huo, sio wao pekeyao bali ni wataifa kwa ujumla, hivyo Serikali iko pamoja nao katika msiba huo na itashirikiana nao kwa mazishi na madawa kwa wale ambao wamepata majeruhi na kulazwa katika hospitali.
“Nimepokea habari ya kusikitisha kutoka kwa viongozi wenzangu, kuhusu kuanguka kwa ukuta na kupelekea kupoteza maisha ya wananchi watatu, na wengine watatu kujeruhiwa”alisema Mohammed Aboud.
Kwa upande wake mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Wawi kisiwani Pemba, Hamad Rashid Mohammed, alisema kuwa kukosekana kwa taaluma kwa wananchi juu ya vifaa vitakavyo tumika pamoja na athari zake zitakazo tokea imechangia kutokea kwa tukio hilo.
Alisema kuwa, hilo lililotokea ni funzo tosha kwa serikali na kuitaka serikali kuwa makini wakati wote na kabla ya kufanya kitu chochote waangalie athari yake ili kuweza kuepusha majanga kama hayo.
Aidha alisema kuwa, kutokea kwa tuki hilo ni funzo kwa tasisi zote za umma pale wanapotaka kufanya kitu lazima wajuwe athari yake inayoweza kutokea hapo baadae, ambamba na kuwataka wananchi kuwa watulivu katika kipindi hiki kifupi.
“Nawashukuru sana vikosi vyetu vya Ulinzi licha ya kukosa zana za kisasa, walipopewa taarifa tu wamefika na kuanza kuokoa maisha ya wananchi, hilo ni jambo la kuwapongeza, wananchi tuwe pole katika kipindi hiki kigumu cha msimba kwani ni msiba wetu sote huu.”alisema Hamad Rashid.
Naye mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kassim Tindwa, aliwashukuru wananchi wa maeneo ya Machomanne kwa juhudi zao kubwa walizozionyesha kabla ya kufika kwa vikosi vya uokozi katika tukio hilo.
Aliwataka wataalamu wanaotoa tenda kutumia taaluma zao wakati wanapotoa tenda kwa kuchukuwa wafanya kazi wenyetaaluma, kwa kuangalia wafanyakazi wao taaluma zao wakati wanapotaka kufanyiwa kazi zao.
Aliwapa pole familia zote zilizopoteza ndugu na jamaa zao katika eneo la tukio hilo, katika kipindi hicho kigumu. “ Sina budi kuwapongeza wananchi wote waliofika katika tukio hilo, na kuweza kusaidia uokozi kabla ya kufika kwa vikosi vya uokozi katika tukio hili”alisema Tindwa.
Kwa upande wake Mkuu wa kikosi cha Zimamzoto na Uokozi Pemba, ACF Iddi Khamis Juma, alisema kuwa katika tuko hilo changamoto kubwa iliyowakabili ni kukosekana kwa vifaa vya kisasa vya uokozi, hali iliyopelekea kuchukuwa muda mwingi kwa kutumia vufaa vya kienyeji.
Alisema kuwa, licha ya kutumika kwa vifaa vya kienyeji lakini waliweza kuziopoa marehemu zilizokuwa zimekwama katika mnara huo, sambamba na kuwataka wananchi pindi likitokea tukio kutoa taarifa kwa wakati muafaka kwa vyombo vya Sheria.
“Tulipopata taarifa tu tuliweza kupeana taarifa makamanda wote na kufika katika eneo la tukio na kuweza kuziopoa maiti zilizokuweko juu ya Mnara huo, ila kikwazo ni zana za uokozi kwani tumetumia dhana duni”alisema.
Naye mmoja kati ya wafanyakazi katika mnara huo, Said Mohammed , alisema kuwa katika kazi hiyo jumla wako vijana 12 ambao ndio wanofanya kazi ya ubomoaji wa mnara huo.
Said alisema kuwa, wanapofika asumuhi huchonga kuta hilo kwa kutumia drili ili kuweza kuliangusha au kuvunja kidogo kidogo, na baadae hushuka chini na kuuvuta kwa gari huo ukuta.
“Leo kabla ya hawajateremka chini, ukuta uliwaangukia na tukaamua kupanda juu kwa lengo kuwaokoa merejeruhi kwanza waliokuwepo hapo juu”alisema kiongozi huo.
Ujenzi huo wa mnara wa tangi la maji Machomanne Chake Chake Pemba, unaendeshwa na kampuni wa Serengeti Limited ya Tanzania Bara.

 Na Abdi Sueliman Na Bakari Mussa, Pemba.

0 comments: