Mvua
 zinaendelea kunyesha sehemu mbalimbali za nchi bado zinaonekana 
kusumbua kwa baadhi ya maeneo hasa yaliyo mabondeni na sehemu ambazo 
mitaro yake ya maji haisafirishi maji vizuri,hii ni mchana wa leo baada 
ya mvua hiyo kunyesha ambayo imesababisha usumbufu mkubwa baada ya 
maeneo mengi kukumbwa na tatizo la maji mengi ambayo yaliziba barabara 
,nyumba za watu pamoja na maeneo mbalimbali.
Mvua hizo ambazo mamlaka ya hali ya hewa pia wametahadhalisha kwamba 
zitakuwepo kuanzia Tarehe 5.03.2014 hadi Tarehe 7.03.2014 ,miongoni mwa 
sehemu zilizopata usumbufu mkubwa wa mvua hizi ni Hospitali ya 
Halmashauri ya Kinondoni Sinza – Palestina baada ya kujaa maji kila kona
 na kufanya wauguzi kuacha kazi na kupanda juu ya Meza na viti wakikwepa
 maji hayo huku wengine kukimbia katika eneo hilo kuhofia maji hayo.
Sababu kubwa ya kukwepa maji hayo ni kile kinachosemekana kuwa  maji 
hayo si ya mvua tuu lakini yanakuwa Machafu yaliyochanganyikana na maji 
kutoka vyooni ambapo kuna chemba moja ya maji machafu imepita hapo na 
baada ya mvua hiyo kwisha inasemekana iliwachukua zaidi ya dakika 30 
kufanya usafi kutoa matope yaliyokuwa yamejaa vyumbani.
Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo amekili kwamba kuhusu usumbufu mkubwa 
wa chemba hiyo na mvua hasa katika kipindi hicho ambapo zinanyesha kwa 
kiasi kikubwa na kuongeza kuwa kunajuhudi zinahitajika kufanyika ili 
kuweza kunusuru tatizo hilo lisiendelee.
Hizi ni baadhi ya picha hizo.
Source:Dar es salaam yetu.
 






 
 
 
 






0 comments:
Post a Comment