Jana katika Mchezo wa soka wa kinyang'anyiro cha klabu bingwa Barani Afrika, uliozikutanisha timu za Yanga (Tanzania) na Al-Alhly (Misri) Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam (Tanzania), timu ya Yanga imepata ushindi wa goli moja.
Lakini cha kustajaabisha ni ripoti kuwa kabla hata ya kuanza kwa
mtanange huo, baadhi ya mashabiki wa timu ya soka ya Simba ambayo ni
wapinzani wa jadi wa Yanga, walianza kung'oa viti na kuvirusha upande
walipokuwa wameketi washabiki wa Yanga.
Chokochoko hizo inaripotiwa kuwa zilitulia wakati mchezo ukiendelea,
ila zikarejea tena mara baada ya Yanga kupata goli, saari hii ni
mashabiki wa Simba tena waliovalia jezi za Simba walianza tena kung'oa
viti na kuwarushia mashabiki wa timu ya Yanga waliokuwa wakishangilia.
Tizama picha zaidi hapo chini...
Kikosi cha Yanga:- Deogratias Munishi, Nadir Haroub 'Canavaro', Mbuyu
Twite, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Frank Domayo, Simon Msuva, Haruna
Niyonzima, Emmanuel Okwi, Mrisho Ngassa na Hamis Kiiza.
(Aiba: Juma Kaseja, Juma Abdul, Athuman Idd 'Chuji', David Luhende, Hassan Dilunga, Didier Kavumbagu na Said Bahanuzi.)
Kikosi cha Al-Ahly: Sherif Ahmed, Saadeldin Saad (c), Mohamed El Ghareeb, Ahmed El Moneim, Sayed Wahed, Shihab Saad, Hossam Mohamed, Ramy Abdel Aziz, Moussa Yedan, Mohamed Ismail na Amr Sayed.
(Akiba: Ahmed Gamal Mo, Amed Ahmed, Wael Kamel, Elsayed Mahdy, Mahmoud Ibrahim, Ahmed Adam na Ahmed Abdelraouf.)
- Picha zaidi: Michuzi-matukio.blog
- Shukurani ya taarifa kuhusu vurugu: Mdau wa wavuti.com aliyekuwa Uwanjani leo
- Majina ya vikosi: Blogu ya SufianiMafoto.com
0 comments:
Post a Comment