Jengo la kisasa la KCU 1990 LTD (Bahaya building).
Na Deogratias Kishombo
Pamoja
na juhudi zote zinazofanywa na uongozi wa juu wa chama cha msingi Mkoa
wa Kagera kwa kushirikiana na wanachama wa zao la kahwa mkoani humo
zinapigwa vita na baadhi ya watu wachache ambao kwa namna moja ama
nyingine hawawatakii mema wakulima na familia zao ambao wanategemea zao
la kahawa kiuchumi.
Kumekuwepo
na upotishaji wa makusudi hasa katika kutaka kufitinisha wakulima
ambao wana imani na viongozi wao kuanzia ngazi ya chama cha msingi hadi
chama kikuu cha ushirika (KCU 1990 Ltd)
Aidha
KCU inategemewa na si wakulima pekee yake bali pia watu wengine
wakiwepo wataalam waajiliwa kuanzia madereva, wafanyakazi wa maofisini,
wataalam washauri, n.k
Ukiwasikiliza
wakulima wenyewe ambao wanatoka katika mtandao wa vyama vya msingi
zaidi ya 100 na pia viongozi hasa wa kiserikali mkoani Kagera
watakuambia ni kuendelea kuchelewesha maendeleo katika Mkoa huo uliyoko
kaskazini mwa Tanzania.
Wakulima
wanaenda mbali zaidi kwa kusema, fitina hizo si tu zitaathiri wakulima
pekee bali zitawagusa hata watu wengine na kwenye sekta ya kahawa mkoani
humo . Wanasema kilimo cha kahawa kina changamoto nyingi hivyo si
busara kuwashambulia viongozi wa ushirika bila kangalia masuala ya
msingi kuanzia kwa mkulima mwenyewe.
Hoja
hiyo inangwa mkono na Mbunge wa Muleba Kaskazini Charles Mwijage ambaye
anasema kinachotokea sasa ndani ya ushirika wa Kagera ni changamoto
ambazo zimejikita katika katika masuala mbalimbali kuanzia kwa mkulima
mwenyewe.
“Suala
lililopo katika ushirika wa Kagera ni changamoto ambazo zinahitaji
kutatuliwa kuanzia kwa mkulima mwenyewe siyo viongozi waliopo madaraka”
anasema na kuongeza.
“Lazima
tuangalie mifumo yetu. Tuangalie tunapataje wawakilishi, tunazalisha
kiasi gani na kwa kiwango gani. Pia tuangalie mifumo yetu ya uwakilishi
kama inakidhi matakwa na mambo kadha wa kadha, kuendelea kusema viongozi
wetu hawatufai siyo suluisho la matatizo ya ushirika” anasema.
Naye
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kutengeneza kahawa cha Tanganyika Instant
Coffee Company (Tanica) Bwana Leonidas Ishansha anasema anawashukuru
KCU kwa ubia wao na kwa kutoa mchango mkubwa kwa kiwanda hicho lakini
anasema uzalishaji usioridhisha wa kahawa unaathiri mapato na uzalisha
ji wa kiwanda hicho. KCU inamiliki zaidi ya asilimia 50 ya kiwanda cha
TANICA
“Uwezo
wetu nikuzalisha tani 500 kwa mwaka lakini kutokana na uzalishaji mdogo
tunazalisha chini ya kiwango karibu tani 300 kwa mwaka” anasema.
Bwana
Ishansha amesema hayo baada ya Kampuni yake ya TANICA kupata tuzo
katika orodha ya makampuni bora ya kati (Mid-sized companies) mwaka 2013
mashindano ambayo yanaratibiwa na Kampuni ya kimataifa ya KPMG. TANICA
imeibuka kampuni bora pekee kutoka katika mkoa wa Kagera.
“Mafanikio
yetu yanatokana na juhudi za chama cha msingi cha mkoa wa Kagera yaani
KCU 1990 ltd ambacho kimekuwa chanzo chetu kikuu cha fedha na pia
wanatupatia kahawa kwa ajili ya uzalishaji” anaongeza.
KCU
imekuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya mkoa ukianzia ngazi ya
mkulima wa kawaida wa kahawa hadi kwa pato la mkoa pamoja na kupitia
katika changamoto mbalimbali.
KCU
1990 Ltd imebuni miradi mingi katika mtandao wake wa vyama vya msingi
kutoka katika wilaya za Misenyi, Muleba na Bukoba. Mtandao huu una vyama
vya msingi 125 na wanachama zaidi ya 60,000.
Katika
juhudi hizo, kimebuni kuwasaidia wakulima wanaozalisha kahwa ya
“organic” kwa kuwapatia mashine za kukoboa kahawa na kimewapatia
wasimamizi wataalamu wa kuwasidia wakulima katika maeneo yao ya kilimo.
Aidha,
katika juhudi hizo KCU pia imebuni vyanzo mbalimbali vya mapato ili
chama kikuu hicho kiweze kujiendesha na kuwasaidia wakulima. Kwa sasa
KCU inamiliki mahoteli, viwanda, majengo na vyanzo vingine mbalimbali
vya mapato ambavyo vinatoa ajira na kupunguza umasikini katika mkoa wa
Kagera.
Baadhi ya wakulima wamenufaika na mikopo inayotolewa na vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa (SACCOS) vilivyo chini ya KCU.
Kama
anavyosema Meneja mkuu wa chama kikuuu cha ushirika mkoani humo
Vedastus Ngaiza, ushirika wa Kagera ndiyo ushirika pekee wa mfano
ukilinganisha na mikoa mingine.
Ngaiza
anamshukuru Rais Kikwete kwa juhudi zake za kuunga mkono ushirika wa
Kagera. Rais Kikwete aliusifia ushirika wa Kagera wakati akizindua jengo
la kitega uchumi cha KCU katikati ya mji wa Bukoba mtaa wa One way.
Bwana
Ngaiza anasema “Tunashukuru kuona kwamba viongozi wetu wa serikali na
wakulima wanatuunga mkono pamoja na kuwepo ghiriba za watu wachache.
Hatutakata tamaa” anasema.
Anatoa ushauri kwa wakulima kwamba waendelee kuzalisha kwa kiwango kikubwa lakini wajitahidi sana kuzalisha kahawa bora.
“Ninawashauri
wakulima wazalishe kahawa bora ili wajiongezee kipato kwa ajili ya
familia zao na kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi” anaongeza.
Naye
Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Masawe chini ya kauli
mbiu yake ya kuleta maendeleo “Kagera Amani na Maendeleo” anawashauri
wanakagera kujikita katika masuala ya maendeleo na kuacha masuala ya
malumbano yasiyo kuwa na tija katika mkoa wa Kagera.
Akiongea
na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake mjini Bukoba mwishoni mwa
mwaka jana mkuu huyo wa Mkoa anasema, “Kagera ni mkoa uliobarikiwa kuwa
na rasilimali nyingi hivyo masuala yasiyokuwa na tija yanarudisha nyuma
maendeleo” alisema.
Katika
kipindi cha utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2012/2013, Mkoa wa Kagera
ulikabiliwa na changamoto mbalimbali kubwa ikiwa Mwamko mdogo wa
wananchi wa Kagera kuchangia utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani
humo.
0 comments:
Post a Comment