Wednesday, 5 March 2014

BOSI WA ARSENAL AWAPASHA MAWAKALA WA WACHEZAJI!!

>>IVAN GAZIDIS ADAI WACHEZAJI WANALIWA FEDHA ZAO!!

ARSENAL_TEAM-INDONESIAKWA MUJIBU wa Mtendaji Mkuu wa Arsenal, Ivan Gazidis, Wachezaji wanapoteza Fedha zao nyingi kwa sababu Mawakala wao wanatoza Ada kubwa na hili linapaswa kuchukuliwa hatua na Wanasoka.
Akiongea na Wanahabari baada ya Mkutano wa ECA, European Club Association, Chama cha Klabu za Ulaya, Gazidis alitamka: “Klabu nyingi hulipa Fedha za juu kabisa wakinunua Mchezaji na popote Fedha hizi zinapokwenda Klabu zitalipa Fedha nyingi mno. Lakini, Wachezaji wanapaswa kupata Fedha zaidi hasa hizi wanazolipwa Mawakala. ”
Hata hivyo, licha ya kukiri umuhimu wa Mawakala, Gazidis ametaka ziwepo Sheria mpya kudhibiti Mgao wa Fedha kwa Mawakala.
Kwa mujibu wa Utafiti wa ECA kwa Kipindi cha Miaka miwili kuanzia 2011 hadi 2013, Mawakala walivuna Kamisheni za Jumla ya Dola Milioni 254 ikiwa ni Asilimia 14.6 ya thamani ya Uhamisho wa Wachezaji 865 miongoni mwa Klabu za Ulaya.
Akizungumzia ishu hii, Umberto Gandini, ambae ni Mkurugenzi wa AC Milan na pia Makamu Mwenyekiti wa ECA, amesema: “Tunajua lipo tatizo na upo umuhimu wa kuweka Sheria mpya kuzuia Watu wa kati.”
Licha ya kulaumu Mgao wa Mawakala, wengi ndani ya ECA wamekiri kuwa Taratibu za Uhamisho wa Wachezaji zilizopo sasa zinafanya kazi barabara kama ilivyokusudiwa ambapo maslahi ya Wachezaji na Vilabu huzingatiwa ikiwemo kuzingatiwa kwa matakwa ya ‘Hukumu ya Bosman’ ambayo humpa Haki Mchezaji Huru kwenda anapotaka bila Klabu yake kumbana au kupata Mgao.

Related Posts:

0 comments: