Wednesday 25 June 2014

TIMU YA GREEN HILL FC YACHAPWA GOLI 2-0 NA WAMBI FC KATIKA MECHI YA KIRAFIKI




Mbeya;



Timu ya chuo cha Green hill institute ( Green hill fc)ya poteza mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya wambi fc kutoka songwe. Mechi hiyo imechezwa katika viwanja vya shule ya sekondari sangu. Timu ya wambi fc ilianza kwa kasi katika kipindi cha kwanza na kufanikisha kupata goli katika dakika ya 32 likifungwa na Aliki kwa kuachia mkwaju nje ya box   au nje ya kumi na nane na kumshinda golikipa na kuandikaa bao lake la kwanza.
Katika kipindi cha pili timu zilianza kwa kasi huku kila mmoja akijaribu kuliona lango la mwenzake na katika dakika ya 57 timu ya wambi fc ilijipatia bao la pili kupitia kwa kupitia mfungaji wake               Aliki.
Timu ya green hill ilishindwa kuikabili timu ya iwambi fc kwani walielemewa na kushindwa kuliona lango la wambi fc huku ingawa waliyofanyika mabadiliko katika dakika za mwisho ilileta matumaini kwa timu ya green hill kwani Benzo sanga aliweza kuwasumbua mabeki wa wambi fc lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda kwa hadi refali anapuliza kipyenga cha mwisho Wambi fc 2 green hill 0.
Akizungumza na mtandao huu   kapteni wa timu ya green hill fc Emanuel Daudi amesema kiukweli mpira wa mecheza lakini bahati haikua yao Na katika mchezo  kuna kushinda na kushindwa ameongeza kuwa  watazidi kufanya mazoezi wala hawakati tamaa.
Na kwa upande wake Kapteni wa timu ya wambi fc k Harifa amesema timu yao iko vizuri ndio maana wameshinda mechi hiyo na wanarudi kwa furaha wakisubiri mchezo wa marudiano ambao utafanyika katika uwanja wao wa wambi fc.
Baadhi ya mashabiki  ya green hill institute wamesema mchezo ulikua mzuri kwan timu zote zilipambana kwa nia ya ushindi lakini bahati ilienda upande wa wambi fc katikamchezo huo.

 Habari na Franco mkalawa 
No;0754776895. 
HABARI 25/06/2014

0 comments: