Monday 30 June 2014

MARCIO MAXIMO AANZA KAZI KWA KUWAPA `NENO` WACHEZAJI WA YANGA SC

Wachezaji wa Yanga sasa kuanza mazoezi chini ya Maximo


KOCHA mpya wa Yanga sc, Mbrazil Marcio Maximo ameanza kazi leo kwa kufanya mazungumzo na baadhi ya wachezaji wa klabu hiyo .
Mkutano huo umefanyika makao makuu ya klabu ya Yanga, makutano ya Twiga na Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es salaam.
Maximo alipata nafasi ya kuwaeleza mipango yake ya kazi na kuwataka wachezaji waelewe umuhimu wao katika kujenga mafanikio ya Yanga.
Kocha huyo aliyewahi kufanya kazi nchini kwa kuifundisha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars, baada ya kukutana na wachezaji leo hii, sasa yuko tayari kuanza mazoezi ya kujiwinda na msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza mwezi agosti mwaka huu.

 Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0 comments: