Sunday 29 June 2014

SHEREHE ZA KUAGA WASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA MKOANI MWANZA ZAFANA

1  
Meza Kuu katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza (katikati) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja ambaye pia ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo zilizofana katika Ukumbi wa Gereza Kuu Butimba, Mwanza. 2  
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa hotuba fupi kwa Maofisa wa Jeshi la Magereza na Wageni Waalikwa (hawapo pichani) katika Sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza. 3  
Maafisa na Askari wa Magereza Mkoani Mwanza wakimsikiliza Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) wakati akitoa hotuba yake fupi katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza katika Ukumbi wa Bwalo la Gereza Kuu Butimba, Jijini Mwanza. 4  
Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoani Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Mstaafu, Raphael Mollel akitoa nasaha zake kwa niaba ya Wastaafu wote wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Magereza Mkoani Mwanza. 5  
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja ( tai nyekundu) katika picha ya pamoja na Maafisa na Askari wa Magereza Mkoani Mwanza ambao Wanastaafu kwa mujibu wa Sheria ifikapo Julai 1, 2014. Sherehe ya kuwaaga imefanyika katika Ukumbi wa Bwalo la Gereza Kuu Butimba, Mwanza. 6 
Wageni Waalikwa katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza wakitosi vinywaji na Meza Kuu kama inavyoonekana katika picha. 7 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja (tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Magereza ya Mkoa wa Mwanza katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza ambao wanastaafu Utumishi wao kwa mujibu wa Sheria ifikapo Julai 1, 2014. Sherehe hizo zimefanyika Juni 28, 2014 katika Ukumbi wa Bwalo la Gereza Kuu Butimba, Jijini Mwanza(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

0 comments: