Tuesday 24 June 2014

ITALIA NJE KOMBE LA DUNIA, SUAREZ ANG'ATA MTU TENA

, ENGLAND YAAMBULIA MOJA POINTI BRAZIL

ITALIA imeaga Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufungwa 1-0 na Uruguay, bao pekee la Diego Godin katika mchezo ambao mshambuliaji Luis Suarez alimng’ata Giorgio Chiellini. Godin alifunga bao hilo dakika ya 81 na kipa Buffon wa Italia alilazimika kuingia uwanjani dakika ya mwisho kusaidia nguvu ya kusaka bao, Azzuri ikihtaji sare tu kusonga mbele. Italia ilimpoteza mchezaji wake Marchisio aliyetolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Arevalo Rios dakika ya 60. SUAREZ ALIFANANISHWA NA VAMPIRE AMBAO NI WANYONYA DAMU, SASA AMERUDIA TENA! 








 
Costa Rica imemaliza kileleni mwa Kundi D baada ya sare ya 0-0 na England leo ikifikisha pointi saba, Uruguay pointi sita na Italia pointi tatu, wakati England imeondoka na pointi moja. Kikosi cha Italia kilikuwa; Buffon, Barzagli, Bonucci, Chiellini, Marchisio, De Sciglio, Verratti/Motta dk75, Pirlo, Darmian, Balotelli/Parolo dk46 na Immobile/Cassano dk71. Uruguay: Muslera, Caceres, Gimenez, Godin, A.Pereira/Stuani dk63, Gonzalez, Arevalo Rios, Rodriguez/Ramirez dk78, Lodeiro/M Pereira dk46, Cavani na Suarez.

0 comments: