Taarifa
iliyosambaa kwenye mitandao mbalimbali inasema kuwa kuna kundi la watu
waliokuwa na visu limewashambulia na kuua watu 28 huku zaidi ya
100 wakijeruhiwa katika kituo cha treni kilichopo mjini Kunming nchini
China.
Mashahidi
wa tukio hilo wamesema kuwa washambuliaji hao walivalia nguo nyeusi na
kuwavamia abiria waliokuwa wakingojea treni na kuwakatakata huku wengine
wakiwadunga visu wale hasa walioshindwa kukimbia kwa kasi.
Polisi
wamefanikiwa kuwauwa washambuliaji watano kati ya kumi waliofanya
shambulio hilo,Shirika la habari la Xhinua limewalaumu watu wanaopigania
kujitenga katika mkoa wa Shinjiang kwa tukio hilo,ulinzi bado
umeimarishwa eneo la tukio.
0 comments:
Post a Comment