Saturday 15 March 2014

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI PIKIPIKI MALI YA WIZI NA VIFAA VYA KOMPYUTA.VYA KAMATWA

DSC00207 
PRESS RELEASE” TAREHE 15.03.2014.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LAKAMATA PIKIPIKI MOJA MALI YA    
WIZI NA VIFAA MBALIMBALI VYA KOMPYUTA.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA TAREHE 14.03.2014 MAJIRA YA SAA 04:00 USIKU HUKO KATIKA ENEO LA VWAWA, KATA NA TARAFA YA VWAWA, WILAYA YA MBOZI LAKAMATA  PIKIPIKI MOJA YENYE NAMBA ZA USAJILI T.575 CET AINA YA  T-BETTER, CPU KUMI [10] ZA KOMPYUTA PAMOJA NA KEY BOARD MOJA MALI ZA  WIZI. KATI YA MALI HIZO CPU ZIMETAMBULIWA. MTUHUMIWA ALIKIMBIA MARA BAADA YA KUONA ASKARI, JUHUDI ZA KUMTAFUTA ZINAENDELEA.
AIDHA KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA TAREHE 14.03.2014 MAJIRA YA SAA 06:30 ALFAJIRI KATIKA ENEO LA IYELA-AIRPORT, KATA YA IYELA, TARAFA YA IYUNGA JIJI NA   MKOA WA MBEYA, MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FRANSIS JOHN (21) MKAZI WA IYELA ALIKAMATWA AKIWA NA BHANGI KETE 04 SAWA NA UZITO WA GRAM 20. MTUHUMIWA NI MTUMIAJI WA BHANGI HIYO, TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYIKA IKIWA NI PAMOJA NA KUMFIKSHA MAHAKAMANI.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WANANCHI KUTOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI ILI MTUHUMIWA WA TUKIO LA WIZI AWEZE KUKAMATWA. AIDHA ANATOA WITO KWA JAMIII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.
Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

0 comments: