Sunday, 13 July 2014

UTABIRI KOMBE LA DUNIA 2014: ARGENTINA ITAIPIGA 3-1 UJERUMANI, AMESEMA DAVID BECKHAM

article-2690038-1F945EEA00000578-753_634x455Amejitahidi: Lionel Messi ameisaidia Argentina  kufika fainali dhidi ya Ujerumani.
NAHODHA wa zamani wa England, David Beckham anatabiri kumuona Lionel Messi akifanya maajabu katika fainali ya kombe la dunia na kuiongoza Argentina kutwaa ubingwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1986.
Messi anakosolewa na wadau wa soka kwamba ameshindwa kuonesha kiwango chake cha Barcelona katika soka la kimataifa, lakini amefanya kazi kubwa kuifikisha Argentina katika fainali ya leo usiku  dhidi ya Ujerumani.
“Ni mtu wa ajabu,” Beckham alisema kwenye mahojiano na chaneli ya  Adidas football ya YouTube.
article-2690038-193A0E87000005DC-277_634x562“Anawapa watu presha kubwa kwa aina yake ya uchezaji na kitu kinachompa upekee ni kuweza kucheza kama wenzake, ni mchezaji wa timu”.
“Amepata uwezo binafsi mkubwa, lakini ushindi unamaanisha kila kitu kwake. Kama  wachezaji wenzake wanafunga mabao, anakuwa wa kwanza kushangilia nao na nadhani ile ina maana kubwa kuhusu yeye”
“Kucheza na Argentina, nina uhakika kuna presha kiasi fulani ukiangalia huko walikotoka. Kushinda ina maana kubwa kwake, familia na kila mmoja anayemzunguka duniani”.
Kusoma zaidi bofya www.bkmtata.blogspot.com

Related Posts:

0 comments: