Thursday, 6 March 2014

TAIFA STARS YAREJEA TANZANIA JION HII KUTOKA NAMIBIA BAADA YA KUTOKA SARE YA 1-1 KATIKA MECHI YA KIRAFIKI


>>BAO LA STARS LILIFUNGWA NA MCHA KHAMIS!!
>>TAIFA STARS KUREJEA LEO JIONI KUTOKA NAMIBIA!!
NAMIBIA_v_TAIFA_STARS1BAO la Dakika za Majeruhi la Mchezaji alietoka Benchi,NAMIBIA_v_TAIFA_STARS2Panduleni “Kaka” Nekundi, limeiokoa Namibia na kuipa Sare ya Bao 1-1 walipocheza na Taifa Stars, Timu ya Taifa ya Tanzania.
Nae Mchezaji alietoka Benchi, Mcha Khamis, aliifungia Taifa Stars Bao Dakika 3 kabla Mpira kumalizika kufuatia Kona lakini Nekundi alifunga kwa Kichwa baada ya Frikiki iliyopigwa na Petrus Shitembi Dakika 5 ndani ya Dakika za Majeruhi.
Mechi hii ilishuhudiwa na Watu wasiozidi 2000 kwenye Uwanja wa Sam Nujoma na Watazamaji hao hawakuwa na furaha yeyote baada ya Timu yao kushindwa kutengeneza nafasi yeyote ya kufunga.
[RIPOTI NA PICHA TOKA THE MAMIBIAN]
Release No. 038
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Machi 6, 2014
TAIFA STARS KUREJEA MCHANA KUTOKA NAMIBIA
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kurejea Leo Jioni Saa 12 Dakika 45 kutoka Windhoek, Namibia kwenye mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA.
Taifa Stars ambayo katika mechi hiyo dhidi ya Namibia (Brave Warriors) ilitoka sare ya bao 1-1 itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kwa ndege ya South Africa Airways.
Timu inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager baada ya kuwasili itakwenda hoteli ya Accomondia kwa ajili ya chakula cha mchana na baadaye kuvunja rasmi kambi yake.
Boniface Wambura Mgoyo
Media and Communications Officer
Tanzania Football Federation (TFF)

Related Posts:

0 comments: