Friday 23 May 2014

MOHAMMED DEWJI AFANYA ZIARA YA KUKAGUA SHUGHULI ZA MAENDELEO JIMBONI KWAKE

    DSC_0073
    MO akisalimiana na wazee wa kijiji cha Uhamaka kabla ya kuanza kuzungumza na wananchi.
    DSC_0094
    MO akisalimiana na mmoja wa watoto waliofika kwenye mkutano wake Uhamaka.
    DSC_0086
    Mbunge MO akilakiwa na mmoja wa bibi kizee aliyefika kwenye mkutano wake , Karibu mjukuu wangu hapa Uhamaka.
    DSC_0107
    Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akiweka saini kwenye kitabu cha ofisi ya kijiji cha Uhamaka Manispaa ya Singida wakati akiwa kwenye ziara ya kiazi ya siku moja kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo katika jimbo hilo, kulia ni diwani wa kata hiyo na Shaban Kiranga. Kushoto ni mjumbe wa NEC Manispaa ya Singida, Hassan Mazala.

    DSC_0198
    Afisa Mtendaji wa Kata ya Uhamaka akisoma taarifa ya ujenzi huo.
    DSC_0220
    Mbunge Dewji akizungumza na wananchi wa kijiji cha Uhamaka wakati wa mkutano wake wa kutembelea jimbo hilo.
    DSC_0111
    Sehemu ya umati wa Kinamama na watoto wa kijiji cha Uhamaka Manispaa ya Singida wakimsikiliza Mbunge wao.
    DSC_0119
    Kikundi cha Ngoma na Kwaya ya kijiji cha Uhamaka wakiimba wimbo wa kumkaribisha Mbunge wao Mohammmed Dewji (MO).
    DSC_0243
    Mjumbe wa NEC Manispaa ya Singida, Hasan Mazala akizungumza kwenye mkutano huo.
    DSC_0177
    Vijana nao walihudhuria mkutano wa Mbunge wao MO katika kijiji cha Uhamaka.

    : MO akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa ya sekondari ya Uhamaka.
    DSC_0274
    DSC_0287
    Sheikh wa msikiti wa kijiji cha Ititi akimkaribisha MO.
    DSC_0294
    Sehemu ya Msikiti wa kijiji cha Ititi ambapo MO aliguswa na kuwachangia mifuko 30 ya Saruji na Mabati 30 kwa ajili ya kuedeleza ujenzi wao.
    DSC_0344
    MO akishiriki kucheza ngoma ya Kinyaturu.
    DSC_0380
    Viongozi wa kijiji cha Uhamaka wakiwa ofisini kwao na Mbunge MO .
    DSC_0387
    Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ititi, Jumanne Ivanga akisoma taarifa ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Ititi kwa Mbunge MO.
    DSC_0404
    MO akihutubia wananchi wa kijiji cha Ititi, pia aliahidi kutoa mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa zahanati hiyo.
    DSC_0425
    “ Kwa hiyo mimi kama Mbunge wenu nitatoa mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huu sawa jamani.” Alisisitiza MO huku akishangiliwa na wananchi hao.
    DSC_0449
    DSC_0433
    Kinamama wa kijiji cha Uhamaka wakimshangilia Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO) wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Zahanati ya Kijiji hicho jana.
    DSC_0454
    Sehemu ya viongozi wa dini na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Ititi wakimsikiliza mbunge wao.
    DSC_0468
    Jamani mmeona utekelezaji wa ilani ya CCM..??? Ni maneno ya MNEC Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akizungumza na wakazi wa kijiji cha Ititi.
    DSC_0473
    Mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo.
    DSC_0488
    Mh. Mohammed Dewji akimsikiliza MNEC Hassan Mazala.
    DSC_0522
    Afisa Mtendaji wa kijiji cha Ititi Jumanne Ivanga akimwonyesha Mbunge Mh. Mohammed Dewji sehemu ambapo Zahanati hiyo itajengwa.
    DSC_0526
    Muonekano wa sehemu ya Zahanati ya Kijiji cha Ititi itakapojengwa.
    DSC_0537
    Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akisalimiana na viongozi wa kijiji cha Unyianga mara baada ya kuwasili kwenye hafla fupi ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara jimbo kwake.
    DSC_0557
    MO akicheza na baadhi ya wanakikundi wa uhamasishaji kwenye hafla hiyo.
    DSC_0565
    MO akisikiliza mashairi kutoka kwa kijana Masoud Mkari mara baada ya kuwasili kwenye hafla fupi ya kukagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara jimbo kwake.
    DSC_0581
    Afisa Mtendaji wa kijiji cha Unyianga, Ramadhani Mpondo akisoma taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa Sekondari ya kijiji hicho mbele ya Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini.
    DSC_0607
    Mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji (MO), akizungumza na wapiga kura wake kuhusu mchango wake katika ujenzi wa shule hiyo inayojengwa kwa nguvu za wanakijiji pamoja na mfuko wa jimbo la Singida Mjini ambapo ameahidi mifuko 100 ya Saruji pamoja na Mabati 100.
    Ujenzi wa mradi wa Sekondari ya Kijiji cha Unyianga ulibuniwa na Halmashauri ya kijiji na kuafikiwa na wananchi kwenye mkutano mkuu wa kijiji baada ya kubaini changamoto nyingi zinazohusu wanafunzi wanaoendelea na masomo sekondari ya kata ya Mwankoko ikiwa ni umbali uliopo kati ya Unyianga na Mwankoko takribani Kilometa 18 kwenda na kurudi, hali inayowalazimu wanafunzi kutembea umbali mrefu na hivyo kuchoka na kushindwa kufanya vizuri kwenye masomo.
    DSC_0586
    Baadhi ya wanakijiji wa Unyianga wakimsikiliza Mbunge wao Mh. Mohammed Dewji.
    DSC_0589
    DSC_0622
    MNEC wa Manispaa ya Singida, Hassan Mazala akiwahamisha wananchi kushiriki kuchangia shughuli za maendeleo.
    DSC_0653
    Mh. Mohammed Dewji akipata picha ya pamoja na wapiga kura wake.
    DSC_0656
    Mh. Mohammed Dewji akikagua mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kijiji wakati wa ziara ya jimboni kwake.
    20140523_181746
    Mh. Mohammed Dewji, akifurahi na watoto walipomwambia wanampenda sana wangetamani kuwa kama yeye.

    0 comments: