Saturday 24 May 2014

AL SHABABU WASHAMBULIA BUNGE LA NCHI YA SOMALIA

 
140524105611 al shabaab somalia 512x288 bbc nocredit 2bdab

Kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab limeshambulia bunge la Somalia na kusababisha vifo vya watu kadhaa mjini Mogadishu.
Milipuko na milio ya risasi imesikika huku bunge likishambuliwa, wabunge wakiwa ndani kwa mkutano.
Gari lililokuwa na mabomu lilipuka leo kabla ya saa sita mchana na kufuatiwa na milipuko mingine pamoja na milio ya risasi.
Wabunge pamoja na wafanyakazi wengine waliweza kuokolewa punde baada ya gari kulipuka.
Mashambulizi hayo bado yanaendelea huku wapiganaji hao walifyatua risasi wakiwa ndani ya msikiti mmoja karibu majengo ya bunge.
CHANZO BBC

0 comments: