Thursday 30 May 2013

WATU 92 WAFIKISWA KIZIMBANI KWA CHANZO CHA VURUGU ZA GESI MTWARA

Watu 92 wamefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Mtwara na kusomewa mashitaka mbalimbali, ikiwamo kufanya fujo, kuvunja nyumba, kuiba, kujeruhi na kuhujumu uchumi katika vurugu zilizotekea mjini Mtwara, Mei 22, mwaka huu.

Watu hao walifikishwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Mussa Esanju.
Waendesha Mashitaka wa Serikali, Justine Sanga, na Renatus Mkude, walidai kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo katika tarehe hiyo. 

Watuhumiwa kwa pamoja walikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande.

Uamuzi huo unatokana na wengi wa washtakiwa kukabiliwa na tuhuma za kuhujumu uchumi, kosa ambalo mahakama hiyo haina uwezo wa kuwaachia kwa dhamana.

Hakimu Esanju aliiahirisha kesi hiyo hadi Juni 10, mwaka huu, kwa ajili ya kutajwa.


Source:  Nipashe gazeti

0 comments: