Sunday 26 May 2013

BAYERN MUNICH MABINGWA ULAYA JANA 2013/2014

UCL-FAINALI: BAYERN MUNICH MABINGWA ULAYA!


Robben ajifuta machozi Wembley.
>>BAO LA DAKIKA YA 89 LA ROBBEN NI MUUAJI!!
BAO LA DAKIKA YA 89 la Arjen Robben limefuta gundu kwake na Bayern Munich katika Fainali za UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, baada ya Bao hilo kuipa ushindi wa Bao 2-1 Bayern dhidi ya wenzao wa Germany Borussia Dortmund katika Mechi iliyochezwa Wembley Stadium Jijini London Jumamosi Usiku.
Bayern walipoteza Fainali mbili za UCL katika Miaka mitatu iliyopita, ikiwemo kutolewa kwa Mikwaju ya Penati na Chelsea Mwaka jana tena katika Uwanja wao wenyewe Allianz Arena, lakini safari hii waliibuka Washindi wa Kombe hili kwa mara ya 5.
Ni Real Madrid, mara 9, na AC Milan, mara 7, ndio wameshinda Kombe hili mara nyingi kupita Bayern Munich.
Kwa Kocha wao, Jupp Heynckes, huu ni ushindi mtamu kwa vile anastaafu na nafasi yake kuchukuliwa na aliekuwa Kocha wa Barcelona, Pep Guardiola kwa ajili ya Msimu ujao.

MAGOLI:
Bayern Munich 2
-Mandzukic Dakika ya 60
-Robben 89
>>BAO LA DAKIKA YA 89 LA ROBBEN NI MUUAJI!!

Borussia Dortmund 1
-Mandzukic Dakika ya 68 [Penati]

Mara baada ya Filimbi ya mwisho kulia, Arjen Robben alitokwa machozi kwani alikuwepo wakati Bayern Munich inapoteza Fainali mbili kwa Inter Milan, Mwaka 2010, na Chelsea, 2012, ambapo alikosa Penati katika Mikwaju ya Penati iliyoipa Chelsea Ubingwa, na vile vile akiwa na Chelsea katika Miaka ya 2005 na 2007 walitolewa kwenye Nusu Fainali ya Mashindano haya na mara zote hizo walikuwa ni Liverpool ndio waliowabwaga.
Mechi hii ilitangaza vyema Soka la Kushambulia la Germany.
VIKOSI:
BAYERN MUNICH: Neuer; Lahm, Boateng, Dante, Alaba; Martinez, Schweinsteiger; Robben, Muller, Ribery; Mandzukic.
Akiba: Starke, Van Buyten, Shaqiri, Luiz Gustavo, Tymoshchuk, Pizarro Gomez
BORUSSIA DORTMUND: Weidenfeller; Pisczcek, Subotic, Hummels, Schmelzer; Bender, Gundogan; Blaszczykowski, Reus, Grosskreutz; Lewandowski.
Akiba: Langerak, Kirch, Santana, Kehl, Leitner, Sahin, Schieber.
REFA: Nicola Rizzoli [Italy]
 
 Bayern Munich yatwaa Ubingwa wa Ulaya.

UCL-MABINGWA WALIOPITA:
MSIMU
BINGWA
1955–56 Real Madrid
1956–57 Real Madrid
1957–58 Real Madrid
1958–59 Real Madrid
1959–60 Real Madrid
1960–61 Benfica
1961–62 Benfica
1962–63 Milan
1963–64 Internazionale
1964–65 Internazionale
1965–66 Real Madrid
1966–67 Celtic
1967–68 Manchester United
1968–69 Milan
1969–70 Feyenoord
1970–71 Ajax
1971–72 Ajax
1972–73 Ajax
1973–74 Bayern Munich
1974–75 Bayern Munich
1975–76 Bayern Munich
1976–77 Liverpool
1977–78 Liverpool
1978–79 Nottingham Forest
1979–80 Nottingham Forest
1980–81 Liverpool
1981–82 Aston Villa
1982–83 Hamburg
1983–84 Liverpool
1984–85 Juventus
1985–86 Steaua BucureÈ™ti
1986–87 Porto
1987–88 PSV Eindhoven
1988–89 Milan
1989–90 Milan
1990–91 Red Star Belgrade
1991–92 Barcelona
1992–93 Marseille
1993–94 Milan
1994–95 Ajax
1995–96 Juventus
1996–97 Borussia Dortmund
1997–98 Real Madrid
1998–99 Manchester United
1999–2000 Real Madrid
2000–01 Bayern Munich
2001–02 Real Madrid
2002–03 Milan
2003–04 Porto
2004–05 Liverpool
2005–06 Barcelona
2006–07 Milan
2007–08 Manchester United
2008–09 Barcelona
2009–10 Internazionale
2010–11 Barcelona
2011–12 Chelsea

0 comments: