Friday 31 May 2013

HOFU YA UGONJWA WA KIMETA NCHINI TANZANIA, MIFUGO YAKATAZWA KUINGIZWA ROMBO

Friday, May 31, 2013

K'NJARO UPDATE: HOFU YA KIMETA, MIFUGO YAKATAZWA KUINGIZWA ROMBO



http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/16/Rombo.svg/200px-Rombo.svg.pngSERIKALI imeweka zuio la mifugo kutoka nchini Kenya na maeneo mengine ya Tanzania kuingizwa wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro kutokana na hofu ya kuwepo kwa ugonjwa wa kimeta unaoshambulia wanyama kama ng’ombe.

Mbali na zuio hilo, pia serikali imepiga marufuku uchinjaji wa nguruwe ambao wanadaiwa kulishwa chakula chenye sumu aina ya polad ambao tayari wamesababisha kifo cha mtu mmoja na wengine wanne kulazwa.

Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Elinas Parangyo, alisema hivi karibuni kuwa nguruwe wengi wamekufa na kwamba uchunguzi uliofanywa na wataalamu kutoka jijini Arusha umegundua sababu ya vifo hivyo ni chakula walichokuwa wakipewa.

“Tulipata tukio la kimeta ndani ya wilaya na daktari wa mifugo aliyesajiliwa alipiga karantini ya kutochinja hovyohovyo kama nyama haijapimwa na wataalamu na hiyo inahusu mifugo kama ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe,” alisema Parangyo.

Uchunguzi uliofanywa unaonyesha zaidi ya nguruwe 70 wamekufa na kwamba licha ya zuio hilo, wako baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakiwasafirisha kwa kificho na kwenda kuuzwa katika mikoa mbalimbali nchini.

Mwandishi wetu:Rombo  DIXON BUSAGAGA

0 comments: